< Nehemia 6 >

1 Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
Sanballat, Tobiah, Geshem, and our other enemies heard [a report] that we had finished rebuilding the wall, and that now there were no more (gaps/places where the wall was not finished) (although we had not yet put the doors in the gates).
2 Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
So Sanballat and Geshem sent [a message] to me, in which they said “Come and talk with us at a place in Ono Plain [north of Jerusalem].” But [I knew that] really they wanted to harm me [if I went there].
3 Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
So I sent messengers to them, to tell them, “I am doing an important work, and I cannot go down [there]. (Why should I stop doing this work just to go down to [talk with] you?/I do not want to stop doing this work just to go down to [talk with] you.)” [RHQ]
4 Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
They sent me the same message four times, and each time when I replied to them I said the same thing.
5 Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
Then Sanballat sent one of his servants to me, bringing a fifth message. This one was written, but it was not sealed. [He did that in order that others would read the message that the servant was carrying] in his hand.
6 iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
This is what was written in the message: “Some people in the nearby countries have heard a report that you and the other Jews are rebuilding the wall [in order to be able to resist attacks], because you are planning to revolt [against the king of Babylon]. And the report also says that you are planning to become the king [of the Israelis]. Geshem says that what they have reported is true.
7 na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
[People are also saying that] you have appointed some prophets to proclaim in Jerusalem that you, [Nehemiah, ] are now the king in Judea. King [Artaxerxes] will certainly hear these reports, [and then you will be in big trouble]. So I suggest that we should meet together to talk about this matter.”
8 Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
[When I read that message, ] I sent [the messenger] back to Sanballat to say, “None of what you are saying is true. You have (made this up/concocted this) in your own head/mind.”
9 Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
[I said that because I knew that] they were trying to cause us to be afraid, with the result that we would stop working [on the wall]. So I actually became more determined (OR, I prayed to God to help me) [to continue the work].
10 Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
[One day] I went to talk with Shemaiah, son of Delaiah and grandson of Mehetabel. I went to talk with him in his house, because he was not able (OR, allowed) to leave his house. He said to me, “You and I must enter the very sacred place in the temple and lock the doors, because people are going to come to kill you at night.”
11 Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
I replied, “I (am not that kind of person/do not do things like that) [RHQ]! I would not run and hide in the temple to save my life! No, I will not do that!”
12 Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
When I thought [about what he had said], I realized that God had not told Shemaiah to say that to me. I realized that Tobiah and Sanballat had bribed him [to say that to me].
13 Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
They had bribed him to cause me to be afraid. They wanted me to [disobey God’s commands and] sin [by hiding in the temple]. If I did that, they would be able to ruin my reputation [MTY] and discredit me.
14 Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
[So I prayed, ] “My God, do not forget what Tobiah and Sanballat have done. Punish them. And do not forget that the female prophet Noadiah and some of the other prophets have also tried to cause me to be afraid.”
15 Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
On October 2 we finished rebuilding the wall. We did it all in 52 days.
16 Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
When our enemies in the nearby countries heard about that, they realized that they had been humiliated, because everyone knew that it was because God helped us that we had been able to do this work [and that they had not been able to force us to quit].
17 Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
During this time, the Jewish leaders had been sending many messages/letters to Tobiah, and Tobiah had been sending messages back to them.
18 Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
Many people in Judea were closely associated with Tobiah, because he was the son-in-law of Shecaniah the son of Arah. Furthermore, Tobiah’s son Jehohanan had married the daughter of Meshullam the son of Berekiah.
19 Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.
People often talked in my presence about all the good things that Tobiah had done, and then they would tell him everything that I said. So Tobiah sent many letters to me to try to cause me to become afraid.

< Nehemia 6 >