< Nehemia 4 >

1 Sanbalati aliposikia kwamba tulikuwa tunajenga ukuta upya, alikasirika na akawa na uchungu sana. Aliwadhihaki Wayahudi
And it was just when he heard Sanballat that we [were] rebuilding the wall and it burned to him and he was angry greatly and he mocked the Jews.
2 mbele ya rafiki zake na jeshi la Samaria, akisema, “Hawa Wayahudi wanyonge wanafanya nini? Je, wataweza kuurudishia ukuta wao? Je, watatoa dhabihu? Je, wataweza kumaliza kuujenga kwa siku moja? Je, wataweza kufufua mawe kutoka malundo ya vifusi yaliyoungua hivyo?”
And he said - before brothers his and [the] army of Samaria and he said what? [are] the Jews feeble doing ¿ will they restore for themselves ¿ will they offer sacrifices ¿ will they finish in the day ¿ will they restore the stones from [the] heaps of debris and they [are] burned.
3 Tobia Mwamoni aliyekuwa upande wake akasema, “Wanachokijenga, hata kama mbweha angepanda juu yake, huo ukuta wao wa mawe angeliubomoa!”
And Tobiah the Ammonite [was] beside him and he said also [that] which they [are] building if it will go up a fox and it will break down [the] wall of stones their.
4 Ee Mungu wetu, utusikie, kwa kuwa tumedharauliwa. Warudishie matukano yao kwenye vichwa vyao wenyewe. Uwatoe ili wawe nyara katika nchi ya waliowateka.
Hear O God our for we are contempt and return reproach their to own head their and give them to plunder in a land of captivity.
5 Usiusitiri uovu wao, wala usifute dhambi zao mbele zako, kwa kuwa wamewatukana wajenzi mbele.
And may not you cover over iniquity their and sin their from to before you may not it be wiped out for they have provoked to anger to before the builders.
6 Basi tuliujenga upya ukuta mpaka wote ukafikia nusu ya kimo chake, kwa kuwa watu walifanya kazi kwa moyo wote.
And we rebuilt the wall and it was joined together all the wall to middle its and it belonged a heart to the people to work.
7 Lakini wakati Sanbalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na watu wa Ashdodi waliposikia kuwa ukarabati wa kuta za Yerusalemu ulikuwa umeendelea na mianya ilikuwa inazibwa, walikasirika sana.
And it was just when he heard Sanballat and Tobiah and the Arabs and the Ammonites and the Ashdodites that it had gone up [the] repair of [the] walls of Jerusalem that they had begun the broken down [parts] to be closed and it burned to them exceedingly.
8 Wote walifanya shauri pamoja kuja kupigana dhidi ya Yerusalemu, na kuchochea machafuko dhidi yake.
And they conspired all of them together to come to wage war against Jerusalem and to make for it confusion.
9 Lakini tulimwomba Mungu wetu, na tukaweka ulinzi usiku na mchana kupambana na tishio hili.
And we prayed to God our and we stationed a guard on them by day and night because of them.
10 Wakati ule ule, watu wa Yuda wakasema, “Nguvu za wafanyakazi zinapungua, nacho kifusi ni kingi mno, kiasi kwamba hatuwezi kuujenga upya ukuta.”
And it said Judah it has failed [the] strength of the burden-bearer[s] and the debris [is] much and we not we will be able to rebuild the wall.
11 Pia adui zetu walisema, “Kabla hawajajua au kutuona, tutakuwa palepale katikati yao, na tutawaua na kuikomesha hiyo kazi.”
And they said opponents our not they will know and not they will see until that we will come into [the] midst of them and we will kill them and we will put an end to the work.
12 Kisha Wayahudi ambao waliishi karibu nao walikuja zaidi ya mara kumi na kutuambia, “Popote mtakapoelekea, watatushambulia.”
And it was just when they came the Jews who were dwelling beside them and they said to us ten times from all the places which you will turn to us.
13 Kwa hiyo nikaweka baadhi ya watu nyuma ya sehemu za chini za ukuta kwenye sehemu zilizo wazi, nikawaweka kufuatana na jamaa zao, wakiwa na panga, mikuki na pinde zao.
And I stationed from [the] lower parts of the place from behind of the wall (in the open places *Q(K)*) and I stationed the people to clans with swords their spears their and bows their.
14 Baada ya kuona hali ilivyo, nikasimama na kuwaambia wakuu, maafisa na wengine wote, “Msiwaogope. Mkumbukeni Bwana, ambaye ni mkuu mwenye kuogofya. Piganeni kwa ajili ya ndugu zenu, wana wenu na binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”
And I saw and I arose and I said to the nobles and to the officials and to [the] rest of the people may not you be afraid of them [the] Lord great and awesome remember and fight on brothers your sons your and daughters your wives your and houses your.
15 Adui zetu waliposikia kwamba tumetambua hila yao, na kwamba Mungu amevuruga shauri lao, sote tulirudi kwenye ukuta, kila mmoja kwenye kazi yake.
And it was just when they heard enemies our that it was known to us and he had frustrated God purpose their (and we returned *Q(k)*) all of us to the wall each one to work his.
16 Kuanzia siku ile na kuendelea, nusu ya watu wangu walifanya kazi ya ujenzi, na nusu nyingine wakashika mikuki, ngao, pinde na dirii. Maafisa walijipanga nyuma ya watu wote wa Yuda
And it was - from the day that half of young men my [were] doing the work and half of them [were] holding and the spears the shields and the bows and the body armor and the commanders [were] behind all [the] house of Judah.
17 waliokuwa wakijenga ukuta. Wale waliobeba vifaa vya ujenzi walifanya kazi yao kwa mkono mmoja, na kushika silaha kwa mkono mwingine,
Who were rebuilding the wall and the [ones who] were carrying in burden [were] carrying [it] with [the] one hand his doing the work and one [hand] [was] holding the weapon.
18 na kila mjenzi alijifunga upanga wake upande mmoja akiwa anafanya kazi. Lakini mtu wa kupiga baragumu alikaa pamoja nami.
And the builders each one sword his [were] girded on hips his and [were] building and the [one who] gave a blast on the ram's horn [was] beside me.
19 Kisha nikawaambia wakuu, maafisa na watu wengine wote, “Kazi hii ni kubwa na imeenea sehemu kubwa, nasi tumetawanyika kila mmoja akiwa mbali na mwenzake juu ya ukuta.
And I said to the nobles and to the officials and to [the] rest of the people the work [is] much and extensive and we [are] separate on the wall distant each from brother his.
20 Popote mtakaposikia sauti ya baragumu, jiungeni nasi huko. Mungu wetu atatupigania!”
In [the] place where you will hear [the] sound of the ram's horn there towards you will assemble to us God our he will fight for us.
21 Basi tuliendelea na kazi, nusu ya watu wakishikilia mikuki, kuanzia mawio ya jua hadi nyota zilipoonekana.
And we [were] doing the work and half of them [were] keeping hold on spears from when came up the dawn until came out the stars.
22 Wakati huo pia niliwaambia watu, “Kila mtu na msaidizi wake wakae ndani ya Yerusalemu wakati wa usiku, ili waweze kutumika kama walinzi wakati wa usiku, na kufanya kazi wakati wa mchana.”
Also at the time that I said to the people each one and servant his let them spend [the] night in [the] midst of Jerusalem and they will be for us the night a guard and the day work.
23 Mimi, wala ndugu zangu, wala watu wangu, wala walinzi waliokuwa pamoja nami hatukuvua nguo zetu. Kila mmoja alikuwa na silaha yake, hata alipokwenda kuchota maji.
And not I and brothers my and servants my and [the] men of the guard who [were] behind me not we [were] stripping off clothes our each one weapon his the water.

< Nehemia 4 >