< Nehemia 11 >

1 Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
And they dwelt [the] leaders of the people in Jerusalem and [the] rest of the people they cast lots to bring - one of the ten to dwell in Jerusalem [the] city of holiness and nine the hands [were] in the cities.
2 Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
And they blessed the people all the men who volunteered to dwell in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
And these [are] [the] leaders of the province who they dwelt in Jerusalem and in [the] cities of Judah they dwelt each one on own property his in own cities their Israel the priests and the Levites and the temple servants and [the] descendants of [the] servants of Solomon.
4 ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
And in Jerusalem they dwelt some of [the] descendants of Judah and some of [the] descendants of Benjamin of [the] descendants of Judah Athaiah [the] son of Uzziah [the] son of Zechariah [the] son of Amariah [the] son of Shephatiah [the] son of Mahalalel of [the] descendants of Perez.
5 Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
And Maaseiah [the] son of Baruch [the] son of Col-Hozeh [the] son of Hazaiah [the] son of Adaiah [the] son of Joiarib [the] son of Zechariah [the] son of the Shilonite.
6 Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
All [the] descendants of Perez who were dwelling in Jerusalem four hundred sixty and eight men of strength.
7 Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
And these [are] [the] descendants of Benjamin Sallu [the] son of Meshullam [the] son of Joed [the] son of Pedaiah [the] son of Kolaiah [the] son of Maaseiah [the] son of Ithiel [the] son of Jeshaiah.
8 na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
And after him Gabbai Sallai nine hundred twenty and eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
And Joel [the] son of Zikri [was] overseer over them and Judah [the] son of Senaah over the city [was] second in command.
10 Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Of the priests Jedaiah [the] son of Joiarib Jakin.
11 Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
Seraiah [the] son of Hilkiah [the] son of Meshullam [the] son of Zadok [the] son of Meraioth [the] son of Ahitub [the] supervisor of [the] house of God.
12 pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
And brothers their [who] did the work of the house eight hundred twenty and two and Adaiah [the] son of Jeroham [the] son of Pelaliah [the] son of Amzi [the] son of Zechariah [the] son of Pashhur [the] son of Malkijah.
13 na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
And brothers his leaders of fathers two hundred forty and two and Amashsai [the] son of Azarel [the] son of Ahzai [the] son of Meshillemoth [the] son of Immer.
14 na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
And brothers their mighty [men] of strength one hundred twenty and eight and [was] overseer over them Zabdiel [the] son of (Haggedolim. *L(F)*)
15 Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
And of the Levites Shemaiah [the] son of Hasshub [the] son of Azrikam [the] son of Hashabiah [the] son of Bunni.
16 Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
And Shabbethai and Jozabad over the work external of [the] house of God [were] of [the] leaders of the Levites.
17 Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
And Mattaniah [the] son of Micah [the] son of Zabdi [the] son of Asaph [the] leader of the beginning he gave thanks to the prayer and Bakbukiah [the] second from brothers his and Abda [the] son of Shammua [the] son of Galal [the] son of (Jeduthun. *Q(K)*)
18 Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
All the Levites in [the] city of holiness two hundred eighty and four.
19 Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
And the gatekeepers Akkub Talmon and brothers their who kept watch at the gates one hundred seventy and two.
20 Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
And [the] rest of Israel the priests the Levites [were] in all [the] cities of Judah each one on own inheritance his.
21 Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
And the temple servants [were] dwelling on Ophel and Ziha and Gishpa [were] over the temple servants.
22 Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
And [the] overseer of the Levites in Jerusalem [was] Uzzi [the] son of Bani [the] son of Hashabiah [the] son of Mattaniah [the] son of Mica one of [the] descendants of Asaph the singers to before [the] work of [the] house of God.
23 Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
For [the] commandment of the king [was] on them and a firm ordinance [was] on the singers [the] matter of a day in day its.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
And Pethahiah [the] son of Meshezabel one of [the] descendants of Zerah [the] son of Judah [was] to [the] side of the king to every matter of the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
And to the villages with fields their some of [the] people of Judah they dwelt in Kiriath Arba and daughters its and in Dibon and daughters its and in Jekabzeel and villages its.
26 katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
And in Jeshua and in Moladah and in Beth Pelet.
27 katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
And in Hazar Shual and in Beer Sheba and daughters its.
28 katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
And in Ziklag and in Meconah and in daughters its.
29 katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
And in En Rimmon and in Zorah and in Jarmuth.
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
Zanoah Adullam and villages their Lachish and fields its Azekah and daughters its and they encamped from Beer Sheba to [the] valley of [Ben] Hinnom.
31 Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
And [the] descendants of Benjamin [were] from Geba Micmash and Aija and Beth-el and daughters its.
32 katika Anathothi, Nobu na Anania,
Anathoth Nob Ananiah.
33 katika Hazori, Rama na Gitaimu,
Hazor - Ramah Gittaim.
34 katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
Hadid Zeboim Neballat.
35 katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
Lod and Ono valley of the craftsmen.
36 Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.
And some of the Levites [the] divisions of Judah [belonged] to Benjamin.

< Nehemia 11 >