< Mika 4 >

1 Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
And it will be - at [the] end of the days it will be [the] mountain of [the] house of Yahweh established at [the] head of the mountains and it will be lifted up it more than [the] hills and they will stream to it peoples.
2 Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
And they will come nations many and they will say come - so we may go up to [the] mountain of Yahweh and to [the] house of [the] God of Jacob so he may teach us from ways his so we may walk in paths his for from Zion it will go out instruction and [the] word of Yahweh from Jerusalem.
3 Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
And he will judge between peoples many and he will decide for nations mighty to far away and they will beat swords their into plowshares and spears their into pruning knives not they will lift up nation against nation a sword and not they will learn! again warfare.
4 Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
And they will dwell everyone under own vine his and under own fig tree his and there not [will be one who] terrifies for [the] mouth of Yahweh of hosts it has spoken.
5 Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
For all the peoples they walk everyone in [the] name of own god his and we we will walk in [the] name of Yahweh God our for ever and ever.
6 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
In the day that [the] utterance of Yahweh I will gather the [one who is] lame and the [one who is] outcast I will assemble and [those] whom I have done harm to.
7 Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
And I will make the [one who was] lame into a remnant and the [one who was] straying into a nation mighty and he will reign Yahweh over them in [the] mountain of Zion from now and until perpetuity.
8 Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
And you O Migdal Eder O hill of [the] daughter of Zion to you it will come and it will come the dominion former a kingdom to [the] daughter of Jerusalem.
9 Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
Now why? do you shout shouting ¿ a king [is] there not in you or? counselor your has he perished that it has taken hold of you anguish like [woman] giving birth.
10 Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
Writhe in pain and burst forth O daughter of Zion like [woman] giving birth for now you will go out from [the] town and you will dwell in the open country and you will go to Babylon there you will be delivered there he will redeem you Yahweh from [the] hand of enemies your.
11 Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
And now they have gathered on you nations many that are saying let her be polluted and let it look on Zion eyes our.
12 Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
And they not they know [the] thoughts of Yahweh and not they understand counsel his that he has gathered them like cut grain [the] threshing floor towards.
13 “Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.
Arise and thresh O daughter of Zion for horn your I will make iron and hooves your I will make bronze and you will crush peoples many and I will dedicate to destruction to Yahweh unjust gain their and wealth their to [the] lord of all the earth.

< Mika 4 >