< Mika 2 >
1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Malheur à ceux qui conçoivent l'iniquité. et travailler le mal sur leurs lits! Quand le matin est clair, ils le pratiquent, parce que c'est au pouvoir de leur main.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Ils convoitent les champs et les saisissent, et les maisons, alors emmenez-les. Ils oppriment un homme et sa maison, même un homme et son héritage.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
C'est pourquoi Yahvé dit: « Voici que je prépare contre ce peuple un désastre, dont vous ne sortirez pas le cou, vous ne marcherez pas non plus de manière hautaine, car c'est un mauvais moment.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
En ce jour-là, ils inventeront une parabole contre toi, et se lamenter avec une lamentation lugubre, en disant, Nous sommes complètement ruinés! Les biens de mon peuple sont divisés. En effet, il me le prend et attribue nos champs à des traîtres! »
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
C'est pourquoi, dans l'assemblée de l'Éternel, vous n'aurez pas de personne qui partage le pays par tirage au sort.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
« Ne prophétisez pas! » - ils prophétisent... « Ne prophétisez pas sur ces choses. La disgrâce ne nous rattrapera pas. »
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
On dira: Maison de Jacob, « L'Esprit de Yahvé est-il en colère? Est-ce que ce sont ses actes? Mes paroles ne font-elles pas du bien à celui qui marche sans reproche? »
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
Mais ces derniers temps, mon peuple s'est levé comme un ennemi. Vous dépouillez la robe et les vêtements de ceux qui passent sans s'en soucier, au retour de la bataille.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Vous chassez les femmes de mon peuple de leurs maisons agréables; de leurs jeunes enfants, vous enlevez ma bénédiction pour toujours.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Levez-vous, et partez! Car ceci n'est pas votre lieu de repos, à cause de l'impureté qui détruit, même avec une grave destruction.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
Si un homme, marchant dans un esprit de mensonge, ment en disant, « Je vous prophétiserai du vin et des boissons fortes, » il serait le prophète de ce peuple.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
Je vous rassemblerai tous, Jacob. Je rassemblerai le reste d'Israël. Je les rassemblerai comme les moutons de Bozrah, comme un troupeau au milieu de leur pâturage. Ils vont grouiller de monde.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
Celui qui ouvre le chemin monte devant eux. Ils franchissent la porte et sortent. Leur roi s'éteint avant eux, avec Yahvé à leur tête.