< Mathayo 7 >

1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
“不可判断其他人,否则你也会被判断。
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
你们论断其他人的标准,其他人就会用这标准论断你,你们用什么标准衡量他人,他人也必同样衡量你。
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
为什么你只看到兄弟眼中的木屑,却不理会自己眼中的梁木?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
若你自己眼中有梁木,怎能对兄弟说:‘让我除掉你眼中的木屑’呢?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
这就是伪君子的行为!要先拿走你眼中的梁木,才能看清楚,才有资格除掉兄弟眼中的木屑。
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
不要把圣物丢给狗,也不要把你们的珍珠丢给猪,这样猪就不会将其践踏,狗就不会转过来攻击你们。
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
如果你求,自会给你; 如果你寻找,就会找到; 如果你敲门,门就会为你打开。
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
因为凡祈求必得到,寻找必寻见,敲门必开门。
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
如果你的儿子向你要饼,你会给他石头吗?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
如果他要鱼,你会给他蛇吗?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
即使你们中的邪恶之人,尚且知道把好东西送给儿女,何况你们的天父,自然更会把好东西赐给祈求之人。
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
所以,在对待其他人时,要用你希望他们对待你的方式,这就是律法和先知们的律法。
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
进入必经窄门,只有通往灭亡之门才会大敞大开,道路宽阔,那是很多人都会走的路。
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
但通往生命之门狭窄,道路难行,那是寥寥几人会走的路。
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
小心假先知!他们披着羊皮出现,内心却是残暴的狼。
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
通过果实就可以辨认它们:荆棘中如何摘到葡萄?蒺藜中如何看到无花果?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
所以,好树结好果,坏树结坏果;
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
好树不能结坏果,坏树也不能结好果。
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
不结好果之树,必会被砍下丢在火中。
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
因此你们凭其果子就可以认出他们来。
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
不是每个人喊我‘主啊,主啊!’,就都能进入天国,唯有遵行天父圣意,才能进入。
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
到审判日那天,必有许多人对我说:‘主啊,主啊,难道我们没有以你的名预言,以你的名驱赶魔鬼,以你的名行神迹?’
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
但我会告诉他们:我从来不认识你们,你们这些作恶之人,走开吧!
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
所以,凡听见我的话并遵行之人,才是聪明之人,他们会在结实的岩石上修建房屋。
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
无论是倾盆大雨、大水泛滥、狂风呼啸,这房屋都不会倒塌,因为它稳稳修在结实的岩石之上。
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
凡听我这番言语却不遵行,就如将房屋盖在沙土上的愚人。
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
雨淋、水冲和风吹会摇撼他们的房屋,房子会倒塌,而且很彻底。”
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
耶稣讲完这番话,民众都惊奇他的训诫。
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
因为耶稣教导他们的样子更像权威之人,而非他们熟悉的宗教老师。

< Mathayo 7 >