< Malaki 1 >

1 Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.
[the] oracle of [the] word of Yahweh to Israel by [the] hand of Malachi.
2 Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.” “Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’” Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo,
I have loved you he says Yahweh and you say how? have you loved us ¿ not [did] a brother Esau [belong] to Jacob [the] utterance of Yahweh and I loved Jacob.
3 lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
And Esau I hated and I have made mountains his a waste and inheritance his for jackals of [the] wilderness.
4 Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.” Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana.
For it will say Edom we have been shattered and we may return so we may rebuild [the] ruins thus he says Yahweh of hosts they they will build and I I will tear down and people will call them a territory of wickedness and the people which he was indignant Yahweh until perpetuity.
5 Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’
And eyes your they will see and you you will say he is great Yahweh over [the] border of Israel.
6 “Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu. “Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’
A son he honors a father and a servant master his and if [am] a father I where? [is] honor my and if [am] a master I where? [is] fear my he says - Yahweh of hosts to you O priests [who] despise name my and you say how? have we despised name your.
7 “Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu. “Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’ “Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa.
[you are] bringing near On altar my food defiled and you say how? have we defiled you by saying you [the] table of Yahweh [is] despicable it.
8 Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And if you bring near! a blind [animal] to sacrifice not? [is it] evil and if you bring near a lame [animal] and a sick [animal] [is it] not? evil bring near it please to governor your ¿ will he be pleased with you or ¿ will he lift up face your he says Yahweh of hosts.
9 “Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And now entreat please [the] face of God so he may show favor to us from hand your it was this ¿ will he lift up any of you face he says Yahweh of hosts.
10 “Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu.
Who? also [is] among you so he may shut [the] doors and not you will set light to altar my in vain not [belongs] to me pleasure in you he says Yahweh of hosts and an offering not I will accept from hand your.
11 Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
For from [the] rising of [the] sun and to setting its [is] great name my among the nations and in every place incense [is being] brought near to name my and an offering a pure for [is] great name my among the nations he says Yahweh of hosts.
12 “Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’
And you [are] profaning it by saying you [the] table of [the] Lord [is] defiled it and fruit its [is] despicable food its.
13 Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana.
And you say there! what weariness! and you sniff at it he says Yahweh of hosts and you bring a stolen [animal] and the lame [animal] and the sick [animal] and you bring the offering ¿ will I accept it from hand your he says Yahweh.
14 “Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And [be] cursed [one who] deals deceptively and there among flock his [is] a male and [one who] makes a vow and [one who] sacrifices a blemished [animal] to [the] Lord for [am] a king great I he says Yahweh of hosts and name my [is] feared among the nations.

< Malaki 1 >