< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Inasmuch as many undertook to draw up a narration concerning the accomplished among us things,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
even as delivered [them] to us those from [the] beginning eyewitnesses and servants having been of the word,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
it seemed good also to me also to me having been acquainted from the first with all things carefully with method to you to write, most excellent Theophilus,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
so that you may know concerning which you were instructed [of the] things the certainty.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
There was in the days of Herod (*k*) king of Judea a priest certain named Zechariah of [the] division of Abijah, and (the *k*) wife (of him *N(k)O*) of the daughters of Aaron and the name of her Elizabeth.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
They were now righteous both (in front of *N(k)O*) God walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And no there was to them child, inasmuch as was Elizabeth barren and both having advanced in the years of them were.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
It came to pass now in the priestly serving of him in the order of the division of him before God,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
according to the custom of the priesthood the lot picked [him as] the [one] to burn incense entering into the temple of the Lord;
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
And all the multitude were of the people praying outside at the hour of the incense.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
Appeared then to him an angel of [the] Lord already standing at [the] right of the altar of the incense;
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And was troubled Zechariah having seen [him], and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
Said then to him the angel; Not do fear Zechariah; because has been heard the prayer of you, and the wife of You Elizabeth will bear a son to you, and you will call the name of him John.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And he will be joy to you and gladness, and many at the (birth *N(k)O*) of him will rejoice.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
He will be for great before the Lord, and wine and strong drink certainly not shall he drink, and [of the] Spirit Holy he will be filled even from [the] womb of [the] mother of him.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
And many of the sons of Israel he will turn to [the] Lord the God of them,
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
And he himself will go forth before Him in [the] spirit and power of Elijah to turn [the] hearts of [the] fathers to [the] children and [the] disobedient to [the] wisdom of [the] righteous, to make ready for [the] Lord a people prepared.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
And said Zechariah to the angel; By what will I know this? I myself for am an old man, and the wife of mine having advanced in the years of her.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And answering the angel said to him; I myself am Gabriel the [one] standing before God and I was sent to speak to you and to bring glad tidings to you these.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
And behold you will be silent and not able to speak until that day may happen these things, in return for that not you did believe in the words of mine which will be fulfilled in the season of them.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
And were the people expecting Zechariah and they were wondering at the delaying in the temple of him.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
Having come out then not he was able to speak to them; and they recognized that a vision he has seen in the temple. And he himself was making signs to them and was remaining mute.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
And it came to pass when were fulfilled the days of the service of him, he departed to the home of him.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
After then these days conceived Elizabeth the wife of him and was hiding herself months five saying
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
that Thus to me has done (the *k*) Lord in [the] days in which He looked upon [me] to take away (the *k*) disgrace of mine among men.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
In now the month sixth was sent the angel Gabriel (by *N(k)O*) God to a city of Galilee whose name [was] Nazareth
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
to a virgin betrothed to a man whose name [was] Joseph of [the] house of David, and the name of the virgin [was] Mary.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And having come (*ko*) (angel *KO*) to her he said; Greetings! you graciously favored; The Lord [is] with you. (blessed [are] you yourself among women. *KO*)
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
And (having seen [him] *K*) at the statement she was troubled (of him *k*) and was pondering what kind would be salutation this.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
And said the angel to her; Not do fear Mary, you have found for favor with God.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
and behold you will conceive in womb and will bring forth a son and you will call the name of Him Jesus.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He will be great and Son of [the] Most High He will be called, and will give to Him [the] Lord God the throne of David of the father of Him,
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
and He will reign over the house of Jacob to the ages, and of the kingdom of Him not there will be an end! (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Said then Mary to the angel; How will be this since a man not I know?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And answering the angel said to her; [the] Spirit Holy will come upon you and power of [the] Most High will overshadow you; therefore also the [one] being born Holy [One] will be called [the] Son of God.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
And behold Elizabeth the (relative *N(k)O*) of you also she (has conceived *N(k)O*) a son in old age of her, and this month [the] sixth is to her who [was] called barren
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
For not will be impossible with (God *N(k)O*) every declaration.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Said then Mary; Behold the handmaid of [the] Lord; Would [that] it happen to me according to the declaration of you. And departed from her the angel.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
Having risen up then Mary in days these she went into the hill country with haste to a town of Judah
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
and she entered into the house of Zechariah and greeted Elizabeth.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And it came to pass as heard the greeting of Mary Elizabeth, leaped the baby in the womb of her, and was filled with [the] Spirit Holy Elizabeth
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
and she cried out (in a shout *N(k)O*) loud and said; Blessed [are] you yourself among women, and blessed [is] the fruit of the womb of you.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And from where to me this that may come the mother of the Lord of mine to me myself?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
Behold for as came the voice of the greeting of you into the ears of mine, leaped in exultation the baby in the womb of mine.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
And blessed [is] the [one] having believed that there will be a fulfillment to the [things] spoken to her from [the] Lord.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
And said Mary: Magnifies the soul of Mine the Lord,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
and rejoices the spirit of mine in God the Savior of mine,
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
For He has looked upon the humiliation of the handmaiden of Him. Behold for from henceforth will count blessed me all the generations
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
For has done to me (great [things] *N(k)O*) the Mighty One; And holy [is] the name of Him;
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
And the mercy of Him [is] to generations (and *no*) (generations *N(k)O*) to those fearing Him;
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
He has shown strength with [the] arm of Him; He has scattered [the] proud in [the] thought of heart of them;
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
He has brought down rulers from thrones and exalted [the] humble;
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
[Those] hungering He has filled with good things and [those] being rich He has sent away empty;
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
He has helped Israel [the] servant of Him remembering mercy,
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
even as He spoke to the fathers of us, to Abraham and to the descendants of him to the age. (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
Dwelt then Mary with her (about *N(k)O*) months three and returned to the home of her.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Now Elizabeth was fulfilled the time to give birth for her and she bore a son.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
And heard the neighbours and the relatives of her that magnified [the] Lord the mercy of Him with her, and they were rejoicing with her.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
And it came to pass on day the eighth they came to circumcise the child and were calling it after the name of the father of him Zechariah.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
And answering the mother of him said; No, but he will be called John.
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
And they said to her that No [one] is (among the relatives *N(k)O*) of you who is called the name by this.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
They were making signs then to the father of him the what maybe he would wish to be called (him. *N(k)O*)
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
And having asked for a writing tablet he wrote saying; John is (the *ko*) name of him. And they marveled all.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
Was opened then the mouth of him immediately and the tongue of him and he was speaking blessing God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
And came upon all fear those dwelling around them; and in all the hill country of Judea were being talked about all declarations these,
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And laid [them] up all those having heard in the heart of them saying; What then child this will be? And (for *no*) [the] hand of [the] Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
And Zechariah the father of him was filled with [the] Spirit Holy and prophesied saying;
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
Blessed [be] [the] Lord the God of Israel, because He has visited and He has performed redemption [on] the people of Him,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
and has raised up a horn of salvation for us in (the *k*) house of David (the *k*) servant of Him,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
even as He spoke through [the] mouth of the holy (of the *k*) of [old] age prophets of Him; (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
salvation from [the] enemies of us and from [the] hand of all those hating us,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
to fulfill mercy toward the fathers of us, and to remember [the] covenant holy of Him,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
[the] oath that He swore to Abraham the father of us,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
to grant us without fear from [the] hand (of the *k*) enemies (of us *k*) having been saved to serve Him
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
in holiness and righteousness before Him (all the days *N(k)O*) (of the life *k*) of us.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And you yourself (now, *no*) child, prophet of [the] Most High will be called; you will go for (in front of *N(k)O*) ([the] face of *ko*) [the] Lord to prepare ways of Him,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
to give knowledge of salvation to the people of Him in forgiveness of [the] sins of them
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
through [the] affections of compassion of God of us in which (will visit *N(k)O*) us [the] Sunrise from on high,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
to shine upon those in darkness and in [the] shadow of death sitting, to direct the feet of us into [the] way of peace.
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the child was continuing to grow and he was strengthened in spirit and he was in the deserted places until [the] day of appearance of him to Israel.

< Luka 1 >