< Luka 23 >
1 Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
Then the whole multitude of them arose, and led him vnto Pilate.
2 Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
And they began to accuse him, saying, We haue found this man peruerting the nation, and forbidding to pay tribute to Cesar, saying, That he is Christ a King.
3 Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
And Pilate asked him, saying, Art thou the King of the Iewes? And hee answered him, and sayd, Thou sayest it.
4 Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
Then sayd Pilate to the hie Priests, and to the people, I finde no fault in this man.
5 Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
But they were the more fierce, saying, He moueth the people, teaching throughout all Iudea, beginning at Galile, euen to this place.
6 Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
Nowe when Pilate heard of Galile, he asked whether the man were a Galilean.
7 Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
And when he knewe that he was of Herods iurisdiction, he sent him to Herod, which was also at Hierusalem in those dayes.
8 Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
And when Herod sawe Iesus, hee was exceedingly glad: for he was desirous to see him of a long season, because he had heard many things of him, and trusted to haue seene some signe done by him.
9 Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
Then questioned hee with him of many things: but he answered him nothing.
10 Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
The hie Priests also and Scribes stood forth, and accused him vehemently.
11 Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
And Herod with his men of warre, despised him, and mocked him, and arayed him in white, and sent him againe to Pilate.
12 Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
And the same day Pilate and Herod were made friends together: for before they were enemies one to another.
13 Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
Then Pilate called together the hie Priests and the rulers, and the people,
14 akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
And sayd vnto them, Ye haue brought this man vnto me, as one that peruerted the people: and beholde, I haue examined him before you, and haue found no fault in this man, of those things whereof ye accuse him:
15 Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
No, nor yet Herod: for I sent you to him: and loe, nothing worthy of death is done of him.
16 Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
I will therefore chastise him, and let him loose.
17 Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
(For of necessitie hee must haue let one loose vnto them at the feast.)
18 Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
Then all ye multitude cried at once, saying, Away with him, and deliuer vnto vs Barabbas:
19 (Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
Which for a certaine insurrection made in the citie, and murder, was cast in prison.
20 Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
Then Pilate spake againe to them, willing to let Iesus loose.
21 Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
But they cried, saying, Crucifie, crucifie him.
22 Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
And he sayd vnto them the third time, But what euill hath he done? I finde no cause of death in him: I will therefore chastise him, and let him loose.
23 Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
But they were instant with loude voyces, and required that he might be crucified: and the voyces of them and of the hie Priests preuailed.
24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
So Pilate gaue sentence, that it should be as they required.
25 Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
And he let loose vnto them him that for insurrection and murder was cast into prison, whome they desired, and deliuered Iesus to doe with him what they would.
26 Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
And as they led him away, they caught one Simon of Cyrene, comming out of the fielde, and on him they layde the crosse, to beare it after Iesus.
27 Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
And there followed him a great multitude of people, and of women, which women bewailed and lamented him.
28 Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
But Iesus turned backe vnto them, and said, Daughters of Hierusalem, weepe not for me, but weepe for your selues, and for your children.
29 Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
For behold, the dayes wil come, when men shall say, Blessed are the barren, and the wombes that neuer bare, and the pappes which neuer gaue sucke.
30 Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
Then shall they begin to say to the mountaines, Fall on vs: and to the hilles, Couer vs.
31 Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
For if they doe these things to a greene tree, what shalbe done to the drie?
32 Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
And there were two others, which were euill doers, led with him to be slaine.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
And when they were come to the place, which is called Caluarie, there they crucified him, and the euill doers: one at the right hand, and the other at the left.
34 Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
Then sayd Iesus, Father, forgiue them: for they know not what they doe. And they parted his raiment, and cast lottes.
35 Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
And the people stoode, and behelde: and the rulers mocked him with them, saying, He saued others: let him saue himselfe, if hee be that Christ, the Chosen of God.
36 Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
The souldiers also mocked him, and came and offered him vineger,
37 na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
And said, If thou be the King of the Iewes, saue thy selfe.
38 Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
And a superscription was also written ouer him, in Greeke letters, and in Latin, and in Hebrewe, THIS IS THAT KING OF THE JEWES.
39 Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
And one of the euill doers, which were hanged, railed on him, saying, If thou be that Christ, saue thy selfe and vs.
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
But the other answered, and rebuked him, saying, Fearest thou not God, seeing thou art in the same condemnation?
41 Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
We are in deede righteously here: for we receiue things worthy of that we haue done: but this man hath done nothing amisse.
42 Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
And he sayd vnto Iesus, Lord, remember me, when thou commest into thy kingdome.
43 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Then Iesus said vnto him, Verely I say vnto thee, to day shalt thou be with me in Paradise.
44 Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
And it was about the sixt houre: and there was a darkenes ouer all the land, vntill the ninth houre.
45 kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
And the Sunne was darkened, and the vaile of the Temple rent through the middes.
46 Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
And Iesus cryed with a loude voyce, and sayd, Father, into thine hands I commend my spirit. And when hee thus had sayd, hee gaue vp the ghost.
47 Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
Nowe when the Centurion saw what was done, he glorified God, saying, Of a suretie this man was iust.
48 Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
And all the people that came together to that sight, beholding the things, which were done, smote their brestes, and returned.
49 Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
And all his acquaintance stood a farre off, and the women that followed him from Galile, beholding these things.
50 Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
And beholde, there was a man named Ioseph, which was a counseller, a good man and a iust.
51 lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
Hee did not consent to the counsell and deede of them, which was of Arimathea, a citie of the Iewes: who also himselfe waited for the kingdome of God.
52 Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
He went vnto Pilate, and asked the body of Iesus,
53 Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
And tooke it downe, and wrapped it in a linnen cloth, and laide it in a tombe hewen out of a rocke, wherein was neuer man yet laide.
54 Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
And that day was the preparation, and the Sabbath drewe on.
55 Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
And the women also that followed after, which came with him from Galile, behelde the sepulchre, and how his body was layd.
56 Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.
And they returned and prepared odours, and ointments, and rested the Sabbath day according to the commandement.