< Luka 2 >
1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
一天,凯撒·奥古斯都颁发命令,要对罗马帝国所有民众进行一次人口登记。
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
自从居里纽斯担任叙利亚总督以来,这还是首次人口普查。
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
众人回到自己的城市进行登记。
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
约瑟是大卫王的后人,于是他离开加利利的拿撒勒,前往犹太的大卫之城伯利恒。
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
他与订立婚约的玛利亚一同前往,此时玛利亚即将分娩。
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
他们来到目的地后,玛利亚的产期也到了,
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
诞下她的长子,但因为客栈中没有空房间,他们只能用布包好婴儿,放在马槽中。
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
当晚在伯利恒附近,有几名牧羊人正在看守羊群。
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
主派来的天使现身于他们面前,周身环绕着主的荣光,这让他们吓得魂飞魄散!
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
天使说:“不要怕!看!我为你们带来了好消息,这也会让所有人感受到真正的喜悦。
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
就在今天,在这大卫之城,你们的救世主已经诞生,他就是主基督。
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
当你们在马槽内看到一个被布包裹的婴孩,就代表你们找到他了。”
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
这时忽然出现了很多来自天堂的生命,开始赞美上帝。
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
“赞颂天堂的上帝,人间令他喜悦之人都将获得安宁!”
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
众天使离开他们返回天堂。牧人彼此说:“我们去伯利恒吧,看看主所说的事情,哪些已经成真。”
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
于是他们匆忙赶去,找到了玛利亚、约瑟和放在马槽里的婴孩。
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
在亲眼目睹这一切后,他们就将天使关于这婴儿的讲述告诉其他人。
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
对牧羊人所说的这些事,所有人都感到惊奇万分。
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
玛利亚将所发生的一切牢记心中,反复思量。
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
牧羊人因亲眼见到天使所言成真,于是便赞美和感谢上帝,回去继续看管他们的羊群。
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
婴儿诞生后第八天,需要进行割礼,将他起名为耶稣,这也是玛利亚尚未怀胎之时,天使为其提供的名字。
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
按摩西律法,玛丽和月色还需要进行净化仪式。这一天,约瑟和玛利亚带孩子去耶路撒冷,打算将其展示给主。
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
就像主的律法所述:“所有长子婴儿都应先献给主。”
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
随后他们进行了献祭,因为上帝的律法还说:应献祭“一对斑鸠或两只雏鸽。”
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
在耶路撒冷有一人名叫西蒙,时刻遵循正道行事,非常虔诚。他期待能看到以色列的希望,希望圣灵降临于他。
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
圣灵曾向他显现,告诉他在有生之年必会见到主的基督。
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
他遵循圣灵的指引来到神庙,这时耶稣的父母抱着孩子走进来,打算按照律法献上婴儿。
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
西蒙用双臂抱住耶稣,一边感谢上帝,一边说:
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
“主啊,我的主人,现在可以按照你的承诺,让你的仆人离开了!
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
因为我已亲眼见到
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
你为所有人准备的救赎。
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
他就是将你显现给全世界的光,是你以色列子民的荣耀。”
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
西蒙的话让耶稣的父母很震惊。
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
西蒙向他们祝福,对耶稣的母亲玛利亚说:“这孩子必定会让很多以色列人倒下,也让很多人崛起。他就是上帝的信号,但很多人都会反对他,
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
这也揭露了他们心中的想法。对你而言,这感觉就像被刀剑刺穿。”
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
亚拿是耶路撒冷的一位年事已高的女先知,是亚什部落法内利的女儿,曾有过一段七年的婚姻。
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
丈夫去世后,她便独自寡居,如今已八十四岁,经常会到神庙中膜拜、禁食和祷告。
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
此刻她刚好走近他们,于是开始赞美上帝,然后向所有期待上帝拯救耶路撒冷的众人,讲述耶稣的事情。
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
耶稣的父母完成了上帝律法要求的一切,于是就返回加利利,回到位于拿撒勒的家中。
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
婴儿逐渐长大,愈发强壮和睿智,因为他已获得上帝的赐福。
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
每年逾越节,耶稣的父母都会去耶路撒冷。
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
在他十二岁那年,他们按着惯例再次去参加这个节日。
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
节日结束后本应该回家,但年幼的耶稣仍留在耶路撒冷,他父母却没有意识到这一点,
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
以为他在返回家园的人群之中。一天后,他们开始在亲戚朋友中寻找他。
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
但一直没有找到,于是就回到耶路撒冷继续寻找。
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
三天后,才发现他在神庙里,身边是几位宗教老师。他一面听他们说的话,一面向他们提出问题。
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
所有听过他讲话的人,都对他深刻的理解和回答而惊讶万分。
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
看到眼前这一切,他父母非常不解。他母亲说:“孩子,你怎么能这样对我们?你看,我和你父亲如此担心你,到处找你!”
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
耶稣回答:“你们为什么找我?难道你们不知道,我应该在这里,在我父的家中?”
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
但他父母并不理解他这番话。
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
于是他就顺从父母之意回到拿撒勒,但他母亲把这一切都记在心上。
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
耶稣的智慧和力量不断增长,上帝和民众都喜欢他。