< Luka 12 >
1 Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
In these [times] when were gathering the myriads of the crowd so as to trample upon one another He began to say to the disciples of Him first; do take heed to yourselves of the leaven which is hypocrisy of the Pharisees.
2 Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
No [thing] now concealed is which not will be revealed, nor hidden which not will be known.
3 Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
Instead that as much as in the darkness you have said in the light will be heard, and what into the ear you have spoken in the inner rooms will be proclaimed upon the housetops.
4 “Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
I say now to you those friends of Mine; not you may fear because of those killing the body and after these things not being able more excessive anything to do.
5 Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna )
I will show however you whom you may fear: do fear the [One who] after the killing has authority to cast into hell. Yes I say to you; Him do fear. (Geenna )
6 Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
Surely five sparrows (are being sold for *N(k)O*) assarion two? And one of them not is forgotten before God;
7 Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
But even the hairs of the head of you all have been numbered. Not (therefore *K*) do fear; than many sparrows you are more valuable.
8 “Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
I say now to you; everyone who maybe (may confess *NK(o)*) in Me myself before the men, also the Son of Man will confess in him before the angels of God;
9 Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
the [one] now having denied Me before men will be denied before the angels of God.
10 Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
And everyone who will speak a word against the Son of Man, it will be forgiven to him; to the [one] however [who] against the Holy Spirit having blasphemed not will be forgiven.
11 “Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
When then (they may bring in *N(k)O*) you before the synagogues and the rulers and the authorities, not (may be anxious *N(k)O*) how or what you may present a defense or what you may say;
12 Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
the for Holy Spirit will teach you in same the hour what it behooves [you] to say.
13 Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
Said then one from the crowd to Him: Teacher, do say to the brother of mine to divide with me the inheritance.
14 Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
And He said to him; Man, who Me appointed (a judge *N(k)O*) or partitioner over you?
15 Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
He said then to them; do watch and do keep yourselves from (all *N(k)O*) covetousness, for not in the abounding to anyone the life (to him *NK(o)*) is of the possessions (of him. *N(k)O*)
16 Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
He spoke then a parable to them saying; Of a man certain rich brought forth abundantly the ground.
17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
And he was reasoning within himself saying; What shall I do for not I have where I will store up the fruits of mine?
18 “Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
And he said; This will I do: I will tear down my barns and greater will build and will store up there all (the grain *N(k)O*) (of mine *k*) and the goods of mine
19 Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
And I will say to the soul of mine; Soul, you have many good things laid up for years many. do rest yourself do eat, do drink, do be merry.
20 “Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Said then to him God; Fool! On this night the soul of you (is required *NK(o)*) of you. what now you did prepare — to whom will [it] be?
21 “Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
So [is] the [one] treasuring up for himself and not toward God being rich.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
He said then to the disciples of Him; Because of this I say to you: not do be anxious for the life (of you *k*) what you may eat, nor [be anxious] for the body (of you *o*) what you may put on.
23 Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
The (for *no*) life more is than the food, and the body than the clothing.
24 Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
do consider the ravens that not they sow nor they reap to them not there is a storehouse nor [is] barn — and God feeds them; How much more you yourselves are valuable than the birds?
25 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
Which now of you being anxious is able to the lifespan of him to add hour (one? *ko*)
26 Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
If then (not even *N(k)O*) [the] least you are able [to do], why about the rest are you anxious?
27 “Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
do consider the lilies how they grow: Not do they labor nor do they spin. I say however to you; not even Solomon in all the glory of him was arrayed as one of these.
28 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
If however in [the] (*ko*) field the grass being [here] today and tomorrow into [the] furnace being thrown God thus (dresses, *N(k)O*) how much more you, O [you] of little faith?
29 Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
And you yourselves not do seek what you may eat (and *N(k)O*) what you may drink, and not do worry yourself.
30 Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
these things for all the nations of the world (seek for; *N(k)O*) of you now the Father knows that you have need of these.
31 Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
But do seek the kingdom (*k*) (of Him *N(K)O*) and these things (all things *K*) will be added to you.
32 “Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
Not do fear, O little flock, for took delight the Father of you to give you the kingdom.
33 Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
do sell the possessions of you and do give alms; do make to yourselves purses not growing old, a treasure unfailing in the heavens where thief not does draw near nor moth destroy;
34 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
Where for is the treasure of you, there also the heart of you will be.
35 “Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
should be your waist girded and the lamps burning,
36 kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
and you yourselves like to men waiting for the master of themselves whenever (he may return *N(k)O*) from the wedding feasts, that having come and having knocked immediately they may open to him.
37 Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
Blessed [are] the servants those whom having come the master will find watching; Amen I say to you that he will gird himself and he will make recline them, and having come up he will serve them.
38 Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
And if And if (he may come *k*) in the second (watch *k*) (and if and if *N(k)O*) in the third watch he may come and he may find [them] thus, blessed are (*ko*) (servants *KO*) those!
39 Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
This however do know that if had known the master of the house in what hour the thief is coming, not (he watched *KO*) (maybe *K*) (and *KO*) maybe he have allowed (to be broken into *N(k)O*) the house of him.
40 Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
Also you yourselves (therefore *K*) do be ready, for in the hour not you expect the Son of Man comes.
41 Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
Said then (to him *k*) Peter; Lord, to us parable this speak You or also to all?
42 Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
(And *no*) said (now *k*) the Lord; Who then is the faithful manager (the *N(k)O*) wise whom will set the master over the care [of servants] of him to give [them] in season the measure of food?
43 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Blessed [is] the servant that [one] whom having come the master of him will find doing thus.
44 Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
Of a truth I say to you that over all the possessions of him he will set him.
45 Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
If however shall say the servant that [one] in the heart of him; Delays the master of Me to come, and shall begin to beat the men-servants and the maid-servants to eat also and to drink and to get drunk,
46 Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
will come the master of the servant that [one] in a day in which not he does expect and in an hour that not he knows and he will cut in two him and the place of him with the unbelievers will appoint.
47 “Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
That [very] now servant the [one] having known the will of the master (of him *N(k)O*) and not having prepared (or *N(k)O*) having done according to the will of him will be beaten with many [blows].
48 Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
the [one] however not having known having done however [things] worthy of stripes will be beaten with few. Everyone now to whom has been given much, much will be required from him; and to whom has been committed much, more excessive will they ask of him.
49 “Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
Fire I came to cast (upon *N(k)O*) the earth and how I wish if already it be kindled!
50 Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
Baptism however I have to be baptized [with] and how I am distressed until (while *N(k)O*) it may be accomplished!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
Think you that peace I came to give on the earth? No, I say to you, but rather division.
52 Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
There will be for from now five in one house divided, three against two and two against three
53 Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
(They will be divided *N(k)O*) father against son and son against father, mother against (*no*) (daughter *N(k)O*) and daughter against (*no*) (mother, *N(k)O*) mother-in-law against the daughter-in-law of her and daughter-in-law against mother-in-law (of her. *k*)
54 Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
He was saying now also to the crowds; When you may see a cloud rising up (from *N(k)O*) [the] west, immediately you say (that *no*) A shower is coming, and it happens so.
55 Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
And when a south wind is blowing, you say that Heat there will be, and it happens.
56 Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
Hypocrites! The appearance of the earth and of the sky you know [how] to discern, the time however this how not (do you know *no*) (to discern? *N(k)O*)
57 “Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
Why now even for yourselves not judge you what [is] right?
58 Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
As for you are going with the adversary of you before a magistrate, in the way do give earnestness to have been set free from him otherwise otherwise he may drag away you to the judge, and the judge you (will deliver *N(k)O*) to the officer, and the officer you (will cast *N(k)(o)*) into prison.
59 Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”
I say to you; certainly not shall you come out from there until (of which *k*) even (the *N(k)O*) last lepton you may have paid.