< Mambo ya Walawi 9 >
1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
I stało się dnia ósmego, wezwał Mojżesz Aarona i synów jego, i starszych Izraelskich.
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
I rzekł do Aarona: Weźmij sobie cielca młodego na ofiarę za grzech, i barana na ofiarę całopalenia, oboje zupełne, i ofiaruj je przed obliczem Pańskiem.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
Do synów zaś Izraelskich rzeczesz, mówiąc: Weźmijcie kozła z kóz na ofiarę za grzech, i cielca, i barana, roczniaki zupełne, zdrowe, na ofiarę całopalenia;
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
Także wołu, i barana na ofiary spokojne ku ofiarowaniu przed Panem, i ofiarę śniedną nagniecioną z oliwą; albowiem się wam dziś Pan ukaże.
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
I przynieśli, co rozkazał Mojżesz, przed namiot zgromadzenia; a przystąpiwszy wszystek lud, stanął przed Panem.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Zatem rzekł Mojżesz: Tać jest rzecz, którą wam Pan rozkazał; czyńcież ją, a ukaże się wam chwała Pańska.
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
Rzekł zaś Mojżesz do Aarona: Przystąp do ołtarza, a uczyń ofiarę za grzech swój, i ofiarę paloną twoję, a wykonaj oczyszczenie za się i za lud; uczyń też ofiarę od ludu, i uczyń oczyszczenie za lud, jako rozkazał Pan.
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
Tedy przystąpił Aaron do ołtarza, i zabił cielca na ofiarę za grzech swój.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
I podali mu synowie Aaronowi krew, który omoczywszy palec swój we krwi pomazał rogi ołtarza, a ostatek krwi wylał u spodku ołtarza;
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Ale tłustość z nerkami, i odzieczkę z wątrobą z ofiary za grzech spalił na ołtarzu, jako był rozkazał Pan Mojżeszowi;
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
Mięso zaś i skórę spalił ogniem precz za obozem.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
Zabił też ofiarę całopalenia; i podali mu synowie Aaronowi krew, którą pokropił wierzch ołtarza w około.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
Przynieśli mu też ofiarę całopalenia, i sztuki jej i głowę jej; a spalił ją na ołtarzu;
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
Omył też wnętrzności, i nogi, i spalił je z ofiarą całopalenia na ołtarzu.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
Potem sprawował ofiarę wszystkiego ludu, i wziął kozła na ofiarę za grzech ludu, którego zabił, i ofiarował go, jako i pierwszego.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
Ofiarował też ofiarę całopalenia, i uczynił jej według zwyczaju.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
Ofiarował też ofiarę śniedną, a wziąwszy z niej pełną garść swoję, spalił na ołtarzu oprócz ofiary całopalenia porannej.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
Zabił też wołu, i barana na ofiarę spokojną, która była za lud; i podali mu synowie Aaronowi krew, którą pokropił ołtarz z wierzchu około.
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
Podali mu także tłustość z wołu, i z barana ogon, i tłustość okrywającą wnętrzności i nerki, i odzieczkę z wątroby.
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
Włożyli też tłustości na mostek, i spalili też tłustość na ołtarzu;
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Ale mostek i łopatkę prawą obracał Aaron tam i sam na ofiarę obracania przed obliczem Pańskiem, jako był Pan rozkazał Mojżeszowi.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
Tedy podniósłszy Aaron ręce swe do ludu błogosławił im, a zstąpił od ofiarowania ofiary za grzech, i ofiary całopalenia, i ofiary spokojnej.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
I wszedł Mojżesz i Aaron do namiotu zgromadzenia, a wszedłszy błogosławili ludowi; i okazała się chwała Pańska wszystkiemu ludowi;
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
Bo zstąpiwszy ogień od obliczności Pańskiej spalił na ołtarzu ofiarę całopalenia i tłustości; co gdy widział wszystek lud, wykrzykali a padali na twarzy swoje.