< Mambo ya Walawi 9 >
1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
Then, the eighth day having arrived, Moses called Aaron and his sons, and those greater by birth from Israel, and he said to Aaron:
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
“Take a calf for sin from the herd, and a ram as a holocaust, both immaculate, and offer them in the sight of the Lord.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
And to the sons of Israel, you shall say: ‘Take a he-goat for sin, and a calf as well as a lamb, both one-year-old and without blemish, as a holocaust.
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
Take also an ox and a ram for peace offerings. And immolate them before the Lord, offering with the sacrifice of each one fine wheat flour sprinkled with oil. For today the Lord will appear to you.’”
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
And so they brought everything that Moses had ordered before the door of the tabernacle, where, when all the multitude stood together,
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Moses said: “This is the word, which the Lord has instructed. Accomplish it, and his glory will appear to you.”
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
And he said to Aaron: “Approach toward the altar, and immolate on behalf of your sin. Offer the holocaust, and pray for yourself and for the people. And when you have slain the victim for the people, pray for them, just as the Lord has instructed.”
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
And immediately Aaron, approaching toward the altar, immolated the calf for his sin.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
And his sons brought its blood to him, and dipping his finger in it, he touched the horns of the altar, and he poured out the remainder at its base.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And the fat, and the little kidneys, and the mesh of the liver, which are for sin, he burned upon the altar, just as the Lord had instructed Moses.
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
Yet truly, the flesh and its skins he burned with fire beyond the camp.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
He also immolated the victim of holocaust. And his sons brought its blood to him, which he poured out all around the altar.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
And when the victim itself was cut into pieces, they brought him the head and each of the limbs, all of which he burned with fire upon the altar,
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
having first washed the intestines and the feet with water.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
And making an offering for the sin of the people, he slew the he-goat. And expiating the altar,
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
he accomplished the holocaust,
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
adding to it the sacrifice of the libations, which are to be offered together, and burning them upon the altar, separately from the ceremonies of the morning holocaust.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
He also immolated the ox, as well as the ram, as peace offerings for the people. And his sons brought him the blood, which he poured out upon the altar all around.
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
Then the fat of the ox, and the rump of the ram, and the two little kidneys with their fat, and the mesh of the liver,
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
they placed upon the breasts. And when the fat had been burned upon the altar,
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Aaron separated their breasts and the right shoulders, lifting them up in the sight of the Lord, as Moses had instructed.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
And extending his hands to the people, he blessed them. And so, the victims for sin, and the holocausts, and the peace offerings being completed, he descended.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
Then Moses and Aaron entered the tabernacle of the testimony, and afterwards came out and blessed the people. And the glory of the Lord appeared to the entire multitude.
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
And, behold, a fire from the Lord devoured the holocaust, and the fat which was on the altar. When the crowd had seen this, they praised the Lord, falling on their faces.