< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
And if [is] a sacrifice of peace offering present his if one of the herd he [is] presenting whether a male or a female unblemished he will present it before Yahweh.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
And he will lean hand his on [the] head of present his and he will cut throat its [the] entrance of [the] tent of meeting and they will sprinkle [the] sons of Aaron the priests the blood on the altar all around.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
And he will present from [the] sacrifice of the peace offering a fire offering to Yahweh the fat which covers the entrails and all the fat which [is] on the entrails.
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
And [the] two the kidneys and the fat which [is] on them which [is] on the loins and the lobe on the liver on the kidneys he will remove it.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And they will make smoke it [the] sons of Aaron the altar towards on the burnt offering which [is] on the wood which [are] on the fire a fire offering of an odor of soothing to Yahweh.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
And if [is] one of the flock present his to a sacrifice of peace offering to Yahweh a male or a female unblemished he will present it.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
If a young ram he [is] presenting present his and he will present it before Yahweh.
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And he will lean hand his on [the] head of present his and he will cut [the] throat of it before [the] tent of meeting and they will sprinkle [the] sons of Aaron blood its on the altar all around.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
And he will present from [the] sacrifice of the peace offering a fire offering to Yahweh fat its the fat tail complete close to the backbone he will remove it and the fat which covers the entrails and all the fat which [is] on the entrails.
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
And [the] two the kidneys and the fat which [is] on them which [is] on the loins and the lobe on the liver on the kidneys he will remove it.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And he will make smoke it the priest the altar towards food of a fire offering to Yahweh.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
And if [is] a goat present his and he will present it before Yahweh.
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And he will lean hand his on head its and he will cut [the] throat of it before [the] tent of meeting and they will sprinkle [the] sons of Aaron blood its on the altar all around.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
And he will present from it present his a fire offering to Yahweh the fat which covers the entrails and all the fat which [is] on the entrails.
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
And [the] two the kidneys and the fat which [is] on them which [is] on the loins and the lobe on the liver on the kidneys he will remove it.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
And he will make smoke them the priest the altar towards food of a fire offering to an odor of soothing all fat [belongs] to Yahweh.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
A statute of perpetuity to generations your in all dwelling places your any fat and any blood not you must eat.

< Mambo ya Walawi 3 >