< Mambo ya Walawi 10 >
1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
Alors Nadab et Abiu ayant pris les encensoirs, mirent du feu et de l’encens dessus, offrant devant le Seigneur un feu étranger; ce qui ne leur avait pas été ordonné.
2 Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
Et un feu sorti du Seigneur les dévora, et ils moururent devant le Seigneur.
3 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
Et Moïse dit à Aaron: Voilà ce qu’a dit le Seigneur: Je serai sanctifié dans ceux qui m’approchent, et je serai glorifié devant tout le peuple. Ce qu’entendant, Aaron se tut.
4 Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
Or, Moïse ayant appelé Misaël et Elisaphan fils d’Oziel, oncle d’Aaron, leur dit: Allez et prenez vos frères de devant le sanctuaire, et emportez-les hors du camp.
5 Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
Et aussitôt allant, il les prient, comme ils gisaient, vêtus de leurs tuniques de lin, et ils les jetèrent dehors, comme il leur avait été commandé.
6 Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
Alors Moïse dit à Aaron, et à Eléazar et à Ithamar ses fils: Ne découvrez pas vos têtes, et ne déchirez pas vos vêtements, de peur que vous ne mouriez, et que l’indignation ne s’élève contre toute l’assemblée. Que vos frères et toute la maison d’Israël pleurent l’incendie que le Seigneur a suscité;
7 Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
Mais vous, vous ne sortirez peint de la porte du tabernacle; autrement vous périrez; car l’huile de la sainte onction est sur vous. Ceux-ci firent tout selon l’ordre de Moïse.
8 Kisha Bwana akamwambia Aroni,
Le Seigneur dit aussi à Aaron:
9 “Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
Vous ne boirez point de vin et de tout ce qui peut enivrer, toi et tes fils, quand vous entrerez dans le tabernacle de témoignage, de peur que vous ne mouriez; parce que c’est un précepte perpétuel pour vos générations,
10 Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
Et afin que vous ayez la science de discerner entre le saint et le profane, entre ce qui est souillé et ce qui est pur,
11 na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
Et que vous enseigniez aux enfants d’Israël tout ce qui concerne mes lois que le Seigneur a proclamées par l’entremise de Moïse.
12 Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
Moïse dit alors à Aaron, à Eléazar et à Ithamar, ses fils qui lui étaient restés: Prenez le sacrifice qui est resté de l’oblation du Seigneur, et mangez-le sans levain près de l’autel, parce que c’est une chose très sainte.
13 Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
Or, vous le mangerez dans un lieu saint, parce qu’il vous a été donné, à toi et à tes fils, des oblations du Seigneur, comme il m’a été ordonné.
14 Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
La poitrine aussi qui a été offerte, et l’épaule qui a été séparée, vous les mangerez dans un lieu très pur, toi et tes fils et tes filles avec toi; car c’est pour toi et pour tes enfants qu’elles ont été réservées, des hosties salutaires des enfants d’Israël;
15 Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
Parce qu’ils ont élevé devant le Seigneur l’épaule, la poitrine et les graisses qui sont brûlées sur l’autel, et qu’elles t’appartiennent à toi et à tes fils par une loi perpétuelle, comme a ordonné le Seigneur.
16 Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
Cependant, comme Moïse cherchait le bouc qui avait été offert pour le péché, il le trouva entièrement brûlé; or, irrité contre Eléazar et Ithamar, fils d’Aaron, qui lui étaient restés, il dit:
17 “Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
Pourquoi n’avez-vous pas mangé dans le lieu saint l’hostie pour le péché, qui est très sainte, et qui vous a été donnée, afin que vous portiez l’iniquité de la multitude, et que vous priiez pour elle en la présence du Seigneur,
18 Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
Surtout puisqu’on n’a pas porté de son sang dans les lieux saints, et que vous auriez dû la manger dans le sanctuaire comme il m’a été ordonné?
19 Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
Aaron répondit: La victime pour le péché a été offerte aujourd’hui, et l’holocauste devant le Seigneur; mais pour moi, il m’est arrivé ce que tu vois. Comment aurais-je pu la manger, ou plaire au Seigneur dans les cérémonies, avec un esprit profondément affligé?
20 Mose aliposikia haya, akaridhika.
Ce qu’ayant entendu Moïse, il reçut son excuse.