< Maombolezo 4 >

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
How! it is dimmed gold it is changed the gold fine they lie scattered stones of holiness at [the] head of all [the] streets.
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
[the] children of Zion precious who were weighed with pure gold how! they are considered to jars of earthenware [the] work of [the] hands of a potter.
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
Also (jackals *Q(K)*) they draw out a breast they suckle young their [the] daughter of people my [has become] cruel (like ostriches *Q(K)*) in the wilderness.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
It has cleaved [the] tongue of a suckling-child to (palate its *L(abh)*) by thirst children they have asked for bread [one who] breaks [it] not [belonged] to them.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
The [ones] eating delicacies they are desolate in the streets the [ones] brought up on crimson they have embraced ash heaps.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
And it has become great [the] iniquity of [the] daughter of people my more than [the] sin of Sodom which was overthrown like a moment and not they twisted on it hands.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
They were bright ones of high rank its more than snow they were dazzling more than milk they were red bone more than corals [was] sapphire polishing their.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
It is dark more than soot appearance their not they are recognized in the streets it has shriveled skin their on bone their dry it has become like wood.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Good they are [those] slain of a sword more than [those] slain of hunger who they they flow away pierced through from [the] produce of [the] field.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
[the] hands of Women compassionate they have boiled own children their they have been for eating for them in [the] brokenness of [the] daughter of people my.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
He has completed Yahweh rage his he has poured out [the] burning of anger his and he has kindled a fire in Zion and it has consumed foundations its.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
Not they believed [the] kings of [the] earth (all *Q(K)*) [the] inhabitants of [the] world that he will go opponent and enemy in [the] gates of Jerusalem.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
From [the] sins of prophets its [the] iniquities of priests its who shed in midst its [the] blood of righteous [people].
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
They wandered blind [people] in the streets they were defiled by the blood in not people were able people touched clothes their.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
Depart unclean people called out to them depart depart may not you touch for they fled also they wandered people said among the nations not they will increase to sojourn.
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
[the] presence of Yahweh it scattered them not he will repeat to pay attention to them [the] face of priests not they lifted up (and elders *Q(K)*) not they showed favor to.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
(Yet we *Q(K)*) they failed eyes our to help our futility in watchtower our we watched to a nation [which] not it will save.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
They hunted steps our from walking in open places our it drew near end our they were completed days our for it had come end our.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Swift they were pursuers our more than [the] eagles of heaven on the mountains they hotly pursued us in the wilderness they lay in wait for us.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
[the] breath of Nostrils our [the] [one] anointed of Yahweh he was captured in pits their whom we had said in shadow his we will live among the nations.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Exult and rejoice O daughter of Edom ([who] dwells *Q(K)*) in [the] land of Uz also to you it will pass on a cup you will become drunk and you may strip yourself naked.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
It will finish iniquity your O daughter of Zion not he will increase to take into exile you he will punish iniquity your O daughter of Edom he will make known on sins your.

< Maombolezo 4 >