< Waamuzi 2 >

1 Malaika wa Bwana akakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.
And he went up [the] angel of Yahweh from Gilgal to Bokim. And he said I brought up you from Egypt and I brought you into the land which I swore to ancestors your and I said not I will break covenant my with you for ever.
2 Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu yao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?
And you not you must make a covenant to [the] inhabitants of the land this altars their you will pull down! and not you have listened to voice my what? this have you done.
3 Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”
And also I say not I will drive out them from before you and they will become for you sides and gods their they will become for you a snare.
4 Malaika wa Bwana alipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.
And it was when spoke [the] angel of Yahweh the words these to all [the] people of Israel and they lifted up the people voice their and they wept.
5 Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtolea Bwana sadaka.
And they called [the] name of the place that Bokim and they sacrificed there to Yahweh.
6 Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.
And he sent away Joshua the people and they went [the] people of Israel everyone to own inheritance his to take possession of the land.
7 Watu wakamtumikia Bwana siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, waliokuwa wameona mambo makuu ambayo Bwana alikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.
And they served the people Yahweh all [the] days of Joshua and all - [the] days of the old [men] who they made long days after Joshua who they had seen all [the] work of Yahweh great which he had done for Israel.
8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.
And he died Joshua [the] son of Nun [the] servant of Yahweh a son of a hundred and ten years.
9 Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresi katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.
And people buried him in [the] territory of inheritance his in Timnath Heres in [the] hill country of Ephraim from [the] north of [the] mountain of Gaash.
10 Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjua Bwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.
And also all the generation that they gathered to ancestors its and it arose a generation another after them which not they knew Yahweh and also the work which he had done for Israel.
11 Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Bwana na kuwatumikia Mabaali.
And they did [the] people of Israel the evil in [the] eyes of Yahweh and they served the Baals.
12 Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. Wakamkasirisha Bwana,
And they forsook Yahweh - [the] God of ancestors their who brought out them from [the] land of Egypt and they went after - gods other some of [the] gods of the peoples which [were] around them and they bowed down to them and they provoked to anger Yahweh.
13 kwa sababu walimwacha na kutumikia Baali na Maashtorethi.
And they forsook Yahweh and they served the Baal and the Ashtaroth.
14 Hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.
And it burned [the] anger of Yahweh on Israel and he gave them in [the] hand of plunderers and they plundered them and he sold them in [the] hand of enemies their from round about and not they were able still to stand before enemies their.
15 Popote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.
In every - where they went out [the] hand of Yahweh it was on them for harm just as he had spoken Yahweh and just as he had sworn Yahweh to them and it was distress to them exceedingly.
16 Ndipo Bwana akawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.
And he raised up Yahweh judges and they delivered them from [the] hand of plunderers their.
17 Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri za Bwana.
And also to judges their not they listened for they acted as prostitutes after gods other and they bowed down to them they turned aside quickly from the way which they had walked fathers their to obey [the] commandments of Yahweh not they did so.
18 Kila mara Bwana alipowainulia mwamuzi, Bwana alikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwa Bwana aliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.
And if he raised up Yahweh - for them judges and he was Yahweh with the judge and he delivered them from [the] hand of enemies their all [the] days of the judge for he had compassion Yahweh from groaning their because of [those who] oppressed them and [those who] oppressed them.
19 Lakini kila mara mwamuzi alipofariki, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.
And it was - when died the judge they turned back and they acted corruptly more than fathers their by walking after gods other to serve them and to bow down to them not they let drop any of deeds their and any of way their stubborn.
20 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,
And it burned [the] anger of Yahweh on Israel and he said because that they have transgressed the nation this covenant my which I commanded ancestors their and not they have listened to voice my.
21 mimi nami sitafukuza taifa lolote ambalo Yoshua aliliacha alipofariki.
Also I not I will increase to dispossess anyone from before them any of the nations which he left Joshua and he died.
22 Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia ya Bwana na kuenenda katika hiyo kama njia baba zao walivyofanya.”
So as to put to [the] test by them Israel ¿ [be] keeping [will] they [the] way of Yahweh by walking in them just as they kept [it] ancestors their or? not.
23 Bwana alikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.
And he left Yahweh the nations these to not to dispossess them quickly and not he gave them in [the] hand of Joshua.

< Waamuzi 2 >