< Waamuzi 1 >
1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
After the death of Joshua, the people of Israel asked Yahweh, saying, “Who first will attack the Canaanites for us, to fight against them?”
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
Yahweh said, “Judah will attack. See, I have given them control of this land.”
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
The men of Judah said to men of Simeon, their brothers, “Come up with us into our territory that was assigned to us that together we may fight against the Canaanites. We will likewise go with you to the territory that was assigned to you.” So the tribe of Simeon went with them.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
The men of Judah attacked, and Yahweh gave them victory over the Canaanites and the Perizzites. They killed ten thousand of them at Bezek.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
They found Adoni-Bezek at Bezek, and they fought against him and defeated the Canaanites and the Perizzites.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
But Adoni-Bezek fled, and they pursued him and caught him, and they cut off his thumbs and his big toes.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Adoni-Bezek said, “Seventy kings, who had their thumbs and their big toes cut off, gathered their food from under my table. As I have done, even so God has done to me.” They brought him to Jerusalem, and he died there.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
The men of Judah fought against the city of Jerusalem and took it. They attacked it with the edge of the sword and they set the city on fire.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
After that, the men of Judah went down to fight against the Canaanites who lived in the hill country, in the Negev, and the western foothills.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Judah advanced against the Canaanites who lived in Hebron (the name of Hebron was previously Kiriath Arba), and they defeated Sheshai, Ahiman, and Talmai.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
From there the men of Judah advanced against the inhabitants of Debir (the name of Debir was previously Kiriath Sepher).
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Caleb said, “Whoever attacks Kiriath Sepher and takes it, I will give him Aksah, my daughter, to be his wife.”
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Othniel, son of Kenaz (Caleb's younger brother) captured Debir, so Caleb gave him Aksah, his daughter, to be his wife.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Soon Aksah came to Othniel, and she urged him to ask her father to give her a field. As she was getting off her donkey, Caleb asked her, “What can I do for you?”
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
She said to him, “Give me a blessing. Since you have given me the land of the Negev, also give me springs of water.” So Caleb gave her the upper springs and the lower springs.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
The descendants of Moses' father-in-law the Kenite went up from the City of Palms with the people of Judah, into the wilderness of Judah, which is in the Negev, to live with the people of Judah near Arad.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
The men of Judah went with the men of Simeon their brothers and they attacked the Canaanites who inhabited Zephath and they completely destroyed it. The name of the city was called Hormah.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
The people of Judah also captured Gaza and the land around it, Ashkelon and the land around it, and Ekron and the land around it.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
Yahweh was with the people of Judah and they took possession of the hill country, but they could not drive out the inhabitants of the plains because they had iron chariots.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
Hebron was given to Caleb (like Moses had said), and he drove out from there the three sons of Anak.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
But the people of Benjamin did not drive out the Jebusites who inhabited Jerusalem. So the Jebusites have lived with the people of Benjamin in Jerusalem to this day.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
The house of Joseph prepared to attack Bethel, and Yahweh was with them.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
They sent out men to spy on Bethel (the city that was formerly called Luz).
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
The spies saw a man coming out of the city, and they said to him, “Show us, please, how to get into the city, and we will be kind to you.”
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
He showed them a way into the city, and so they attacked the city with the edge of the sword, but they let the man and all his family get away.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
Then the man went to the land of the Hittites and built a city and called it Luz, which is its name to this day.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
The people of Manasseh did not drive out the people living in the cities of Beth Shan and its villages, or Taanach and its villages, or those who lived in Dor and its villages, or those who lived in Ibleam and its villages, or those who lived in Megiddo and its villages, because the Canaanites were determined to live in that land.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
When Israel became strong, they forced the Canaanites to serve them with hard labor, but they never drove them out completely.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Ephraim did not drive out the Canaanites who lived in Gezer, so the Canaanites continued to live in Gezer among them.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Zebulun did not drive out the people living in Kitron, or the people living in Nahalol, and so the Canaanites continued to live among them, but Zebulun forced the Canaanites to serve them with hard labor.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Asher did not drive out the people living in Akko, or the people living in Sidon, or those living in Ahlab, Akzib, Helbah, Aphek, or Rehob.
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
So the tribe of Asher lived among the Canaanites (those who lived in the land), because they did not drive them out.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
The tribe of Naphtali did not drive out those who were living in Beth Shemesh, or those living in Beth Anath. So the tribe of Naphtali lived among the Canaanites (the people who were living in that land). However, the inhabitants of Beth Shemesh and Beth Anath were forced into hard labor for Naphthali.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
The Amorites forced the tribe of Dan to live in the hill country, not allowing them to come down to the plain.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
So the Amorites lived at Mount Heres, in Aijalon, and in Shaalbim, but the military might of the house of Joseph conquered them, and they were forced to serve them with hard labor.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
The border of the Amorites ran from the hill of Akrabbim at Sela up into the hill country.