< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
And he said Yahweh to Joshua may not you fear and may not you be dismayed take with you all [the] people of war and arise go up Ai see - I have given in hand your [the] king of Ai and people his and city his and land his.
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
And you will do to Ai and to king its just as you did to Jericho and to king its only booty its and livestock its you will plunder for yourselves set for yourself an ambush for the city behind it.
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
And he arose Joshua and all [the] people of war to go up Ai and he chose Joshua thirty thousand man [the] mighty [men] of strength and he sent out them night.
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
And he commanded them saying see you [are] lying in wait for the city behind the city may not you go far away from the city very and you will be all of you prepared.
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
And I and all the people which [is] with me we will draw near to the city and it will be that they will come out to meet us just as at the first [time] and we will flee before them.
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
And they will come out after us until have drawn out we them from the city for they will say [they are] fleeing before us just as at the first [time] and we will flee before them.
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
And you you will arise from the ambush and you will take possession of the city and he will give it Yahweh God your in hand your.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
And it will be when have captured you the city you will set on fire the city with fire according to [the] word of Yahweh you will do see I have commanded you.
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
And he sent out them Joshua and they went to the ambush and they remained between Beth-el and between Ai from [the] west of Ai and he stayed Joshua in the night that in among the people.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
And he rose early Joshua in the morning and he mustered the people and he went up he and [the] elders of Israel before the people Ai.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
And all the people of war which [was] with him they went up and they approached and they came before the city and they encamped from [the] north of Ai and the valley ([was] between it *Q(k)*) and between Ai.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
And he took about five thousand man and he set them an ambush between Beth-el and between Ai from [the] west of the city.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
And they set the people all the camp which [was] from [the] north of the city and rearguard its from [the] west of the city and he went Joshua in the night that in [the] middle of the valley.
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
And it was when saw [the] king of Ai and they hurried and they rose early and they went out [the] men of the city to meet Israel for battle he and all people his to the appointed place before the Arabah and he not he knew that an ambush for him [was] behind the city.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
And they were struck Joshua and all Israel before them and they fled [the] direction of the wilderness.
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
And they were called together all the people which ([was] in Ai *Q(K)*) to pursue after them and they pursued after Joshua and they were drawn out from the city.
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
And not he remained anyone in Ai and Beth-el who not they went out after Israel and they left the city open and they pursued after Israel.
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
And he said Yahweh to Joshua stretch out with the javelin which [is] in hand your to Ai for in hand your I will give it and he stretched out Joshua with the javelin which [was] in hand his to the city.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
And the ambush it arose quickly from place its and they ran when stretched out hand his and they went the city and they captured it and they hurried and they set on fire the city with fire.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
And they turned [the] men of Ai behind them and they saw and there! it went up [the] smoke of the city the heavens towards and not it was in them hands to flee hither and hither and the people which was fleeing the wilderness it turned back against the pursuer.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
And Joshua and all Israel they saw that it had captured the ambush the city and that it went up [the] smoke of the city and they turned back and they attacked [the] men of Ai.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
And these [men] they came out from the city to meet them and they were to Israel in the middle these from this and these from this and they struck down them until not he had left to him a survivor and a fugitive.
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
And [the] king of Ai they captured alive and they brought near him to Joshua.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
And it was when had finished Israel to kill all [the] inhabitants of Ai in the open country in the wilderness which they had pursued them in it and they had fallen all of them to [the] mouth of [the] sword until were finished they and they returned all Israel Ai and they attacked it to [the] mouth of [the] sword.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
And it was all those [who] fell on the day that from man and unto woman two [plus] ten thousand all [the] people of Ai.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
And Joshua not he drew back hand his which he had stretched out with the javelin until that he had totally destroyed all [the] inhabitants of Ai.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Only the livestock and [the] booty of the city that they plundered for themselves Israel according to [the] word of Yahweh which he had commanded Joshua.
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
And he burned Joshua Ai and he made it a mound of perpetuity a desolation until the day this.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
And [the] king of Ai he hanged on the tree until [the] time of the evening and just as went the sun he commanded Joshua and they took down corpse his from the tree and they threw it to [the] entrance of [the] gate of the city and they set up over him a heap of stones great until the day this.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Then he built Joshua an altar to Yahweh [the] God of Israel on [the] mountain of Ebal.
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
Just as he had commanded Moses [the] servant of Yahweh [the] people of Israel according to [what] is written in [the] book of [the] law of Moses an altar of stones complete which not anyone has wielded on them iron and they offered up on it burnt offerings to Yahweh and they sacrificed peace offerings.
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
And he wrote there on the stones copy of [the] law of Moses which he had written before [the] people of Israel.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
And all Israel and elders its and officials - and judges its [were] standing from this - and from this - of the ark before the priests the Levites [the] bearers of - [the] ark of [the] covenant of Yahweh as the sojourner as the native half of it to [the] front of [the] mountain of Gerizim and half of it to [the] front of [the] mountain of Ebal just as he had commanded Moses [the] servant of Yahweh to bless the people Israel at the former [time].
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
And after thus he read aloud all [the] words of the law the blessing and the curse according to every [thing] written in [the] book of the law.
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
Not it was anything from all that he had commanded Moses which not he read aloud Joshua before all [the] assembly of Israel and the women and the little one[s] and the sojourner[s] who went in midst their.

< Yoshua 8 >