< Yoshua 5 >

1 Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.
And it was when heard all [the] kings of the Amorite[s] who [were] on [the] other side of the Jordan west-ward and all [the] kings of the Canaanite[s] who [were] at the sea [they heard] this: he had dried up Yahweh [the] waters of the Jordan from before [the] people of Israel until (passing over they *Q(K)*) and it melted heart their and not it was in them still spirit because of [the] people of Israel.
2 Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.”
At the time that he said Yahweh to Joshua make for yourself knives of flint and return circumcise [the] people of Israel a second [time].
3 Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.
And he made for himself Joshua knives of flint and he circumcised [the] people of Israel to [the] hill of foreskins.
4 Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri.
And this [is] the reason why he circumcised Joshua all the people which had come out from Egypt the males all - [the] men of war they had died in the wilderness on the way when went out they from Egypt.
5 Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa.
For circumcised they had been all the people which came out and all the people born in the wilderness on the way when went out they from Egypt not people had circumcised.
6 Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali.
For - forty year[s] they had walked [the] people of Israel in the wilderness until was finished all the nation [the] men of war who came out from Egypt who not they had listened to [the] voice of Yahweh whom he had sworn Yahweh to them to not to let to see them the land which he had sworn Yahweh to fathers their to give to us a land flowing of milk and honey.
7 Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini.
And children their he raised up in place of them them he circumcised Joshua for uncircumcised they were for not people had circumcised them on the way.
8 Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.
And it was just when they had finished all the nation to be circumcised and they remained in place their in the camp until lived they.
9 Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.
And he said Yahweh to Joshua this day I have rolled away [the] reproach of Egypt from on you and he called [the] name of the place that Gilgal until the day this.
10 Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka.
And they encamped [the] people of Israel at Gilgal and they observed the passover on [the] four-teen day of the month in the evening on [the] plains of Jericho.
11 Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga.
And they ate some of [the] produce of the land from [the] next day of the passover unleavened bread and roasted [grain] on [the] substance of the day this.
12 Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.
And it ceased the manna from [the] next day when ate they some of [the] produce of the land and not it belonged again to [the] people of Israel manna and they ate some of [the] produce of [the] land of Canaan in the year that.
13 Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”
And it was when was Joshua at Jericho and he lifted up eyes his and he saw and there! a man [was] standing to before him and sword his [was] drawn in hand his and he went Joshua to him and he said to him ¿ for us [are] you or? for foes our.
14 Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?”
And he said - In-deed I [am] [the] commander of [the] army of Yahweh now I have come and he fell Joshua to face his [the] ground towards and he bowed down and he said to him what? [is] lord my saying servant his.
15 Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.
And he said [the] commander of [the] army of Yahweh to Joshua take off sandal your from on foot your for the place which you [are] standing on it [is] a holy place it and he did Joshua thus.

< Yoshua 5 >