< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
The second/next tribe that was allotted land was the tribe of Simeon. Each clan in that tribe was allotted some land that was inside the area that had been allotted to the tribe of Judah.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
Their land included the towns of Beersheba ([which is also named] Sheba), Moladah,
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
Hazar-Shual, Balah, Ezem,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
Eltolad, Bethul, Hormah,
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
Ziklag, Beth-Marcaboth. Hazar-Susah,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
Beth-Lebaoth, and Sharuhen. Altogether there were 13 towns and the surrounding villages.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
The land allotted to them also included the four cities of Ain, Rimmon, Ether, and Ashan, and their surrounding villages.
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
They were also allotted some very small villages in an area that extended south to Baalath-Beer (which is [also named] Ramah, in the southern desert). That was the land allotted to the clans of the tribe of Simeon.
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
The tribe of Judah had been allotted much more land than they needed, so part of their land was given to the tribe of Simeon.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
The third/next tribe that was allotted land was the tribe of Zebulun. Each clan of that tribe was allotted some of the land. The southern border started at Sarid [city].
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
It extended west to Maralah [city] and on to Dabbesheth [city], and on to the brook just north of Jokneam [city].
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
The border extended east from Sarid to the area near Kisloth-Tabor [city] and on to Daberath [town] and on to Japhia [town].
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
From there it extended east to Gath-Hepher [city] and Eth-Kazin [town], and north to Rimmon [city]. From there the border extended [west] to Neah [town].
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
From Neah it extended south to Hannathon [city] and from there to Iphtah-El Valley.
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
Their area included the towns of Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah, and Bethlehem. Altogether there were twelve towns and the surrounding villages.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
That was the land that was allotted to the clans of the tribe of Zebulun.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
The fourth/next tribe that was allotted land was the tribe of Issachar. Each of the clans of that tribe was allotted some of the land.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
Their land included the cities of Jezreel, Kesulloth, Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
Hapharaim, Shion, Anaharath,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
Rabbith, Kishion, Ebez,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
Remeth, En-Gannim, En-Haddah, and Beth-Pazzez.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
The border of the area that was allotted to the tribe of Issachar was close to Tabor, Shahazumah, and Beth-Shemesh [cities], and ended [in the east] at the Jordan [River]. Altogether there were 16 cities and the surrounding villages.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
Those cities and villages were in the land allotted to the clans of the tribe of Issachar.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
The fifth/next tribe that was allotted land was the tribe of Asher. Each of the clans in that tribe was allotted some of the land.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
Their land included the towns of Helkath, Hali, Beten, Acshaph,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
Allammelech, Amad, and Mishal. The western border started at Carmel [Mountain] and Shihor-Libnath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
From there it extended [southeast] to Beth-Dagon [town], and then to [the area that was allotted to the tribe of] Zebulun and Iphtah-El Valley. From there the border extended east and then north to Beth-Emek [town] and Neiel and Cabul [towns].
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
From there it extended west to Abdon, Rehob, Hammon, and Kanah [cities], and continued to Sidon, which is a big city.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
From there the border extended south toward Ramah and to the big city of Tyre that had strong walls around it. From there the border extended [west] to Hosah [town] and ended at the [Mediterranean] Sea. Within their area were the towns of Aczib,
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Ummah, Aphek, and Rehob. Altogether there were 22 towns and their surrounding villages.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
Those cities and villages were within the land that was allotted to the clans of the tribe of Asher.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
The sixth/next tribe that was allotted land was the tribe of Naphtali. Each of the clans in that tribe was allotted some of the land.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
The border of their land started [in the west] at the [huge] oak tree at Zaanannim, near Heleph [town]. It extended [east] through Adami-Nekeb [city] and Jabneel, and then to Lakkum, and ended at the Jordan [River].
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
The western boundary extended through Aznoth-Tabor as far as Hukkok [city]. It extended to the borders of [the tribe of] Zebulun at the south, to [the border of the tribe of] Asher on the west, and the Jordan [River] at the east.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
[Within their land were] several cities with strong walls around them. They were Ziddim, Zer, Hammath, Rakkath, Kinnereth,
36 Adama, Rama, Hazori,
Adamah, Ramah, Hazor,
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
Kedesh, Edrei, En-Hazor,
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
Iron, Migdal-El, Horem, Beth-Anath, and Beth-Shemesh. Altogether there were 19 cities and the surrounding villages.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
Those cities and surrounding villages were in the land that was allotted to the clans of the tribe of Naphtali.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
The seventh/last tribe that was allotted land was the tribe of Dan. Each of the clans in that tribe was allotted some of the land.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
Their land included the towns of Zorah, Eshtaol, Ir-Shemesh,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
Shaalabbin, Aijalon, Ithlah,
43 Eloni, Timna, Ekroni,
Elon, Timnah, Ekron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
Jehud, Bene-Berak, Gath-Rimmon,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
Me-Jarkon, Rakkon, and the area near Joppa.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
But the people of the tribe of Dan were unable to take control of the land that had been allotted to them. So they went [northeast] and fought against the people in Leshem [city]. They defeated and killed all the people who lived there. Then they began to live in Leshem, and changed the name of the city to Dan, the man from whom their tribe descended.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
All of those towns and surrounding villages were in the land that was allotted to the clans in the tribe of Dan.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
After the Israeli leaders divided the land among the tribes, they allotted some land to Joshua.
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
They allotted to him Timnath-Serah. Yahweh had said that he could have whatever city he wanted, and that was the city that he chose. It was in the hilly region which was allotted to the tribe of Ephraim. Joshua rebuilt the city and lived there.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
Those were the areas that were allotted to the various tribes of Israel. Eleazar the Supreme Priest and Joshua and the leaders of each tribe divided up the land while they were all at Shiloh, by (casting lots/throwing marked stones) [to decide which area each tribe would receive]. They did that while Yahweh was watching, at the entrance of the Sacred Tent. In that way they completed dividing up the land.

< Yoshua 19 >