< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
And it came out the lot second for Simeon for [the] tribe of [the] descendants of Simeon to clans their and it was inheritance their in [the] midst of [the] inheritance of [the] descendants of Judah.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
And it belonged to them inheritance their Beer Sheba and Sheba and Moladah.
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
And Hazar Shual and Balah and Ezem.
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
And Eltolad and Bethul and Hormah.
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
And Ziklag and Beth Marcaboth and Hazar Susah.
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
And Beth Lebaoth and Sharuhen cities thir-teen and villages their.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Ain - Rimmon and Ether and Ashan cities four and villages their.
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
And all the villages which [were] around the cities these to Baalath Beer of Ramah Negev this [was] [the] inheritance of [the] tribe of [the] descendants of Simeon to clans their.
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
[was] from [the] portion of [the] descendants of Judah [the] inheritance of [the] descendants of Simeon for it was [the] portion of [the] descendants of Judah [too] great for them and they received their inheritance [the] descendants of Simeon in [the] midst of inheritance their.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
And it came up the lot third for [the] descendants of Zebulun to clans their and it was [the] border of inheritance their to Sarid.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
And it goes up border their - to the west and Maralah and it touches Dabbesheth and it touches the wadi which [is] on [the] face of Jokneam.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
And it turns back from Sarid east-ward [the] rising of the sun to [the] border of Kisloth Tabor and it goes out to Daberath and it goes up Japhia.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
And from there it passes on east-ward east-ward Gath towards Hepher Eth towards Kazin and it goes out Rimmon which is turned Neah.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
And it turns itself the border from [the] north Hannathon and they are extremities its [the] valley of Iphtah El.
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
And Kattah and Nahalal and Shimron and Idalah and Beth-lehem cities two [plus] ten and villages their.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
This [was] [the] inheritance of [the] descendants of Zebulun to clans their the cities these and villages their.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
For Issachar it came out the lot fourth for [the] descendants of Issachar to clans their.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
And it was border their Jezreel towards and Kesulloth and Shunem.
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
And Hapharaim and Shion and Anaharath.
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
And Rabbith and Kishion and Ebez.
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
And Remeth and En Gannim and En Haddah and Beth Pazzez.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
And it touches the border Tabor (and to Shahazayim *Q(K)*) and Beth Shemesh and they are [the] extremities of territory their the Jordan cities six-teen and villages their.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
This [was] [the] inheritance of [the] tribe of [the] descendants of Issachar to clans their the cities and villages their.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
And it came out the lot fifth for [the] tribe of [the] descendants of Asher to clans their.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
And it was border their Helkath and Hali and Beten and Acshaph.
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
And Alammelech and Amad and Mishal and it touches Carmel west-ward and Shihor Libnath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
And it turns back [the] rising of the sun Beth Dagon and it touches Zebulun and [the] valley of Iphtah El north-ward Beth Emek and Neiel and it goes out to Cabul from [the] left.
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
And Ebron and Rehob and Hammon and Kanah to Sidon great.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
And it turns back the border Ramah and to [the] city of fortification of Tyre and it turns back the border Hosah (and they are *Q(K)*) extremities its the sea towards from [the] region Aczib towards.
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
And Umah and Aphek and Rehob cities twenty and two and villages their.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
This [was] [the] inheritance of [the] tribe of [the] descendants of Asher to clans their the cities these and villages their.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
For [the] descendants of Naphtali it came out the lot sixth for [the] descendants of Naphtali to clans their.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
And it was border their from Heleph from [the] great tree in Zaanannim and Adami Nekeb and Jabneel to Lakkum and it was extremities its the Jordan.
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
And it turns back the border west-ward Aznoth Tabor and it goes out from there Hukok towards and it touches Zebulun from [the] south and Asher it touches from [the] west and Judah the Jordan [the] rising of the sun.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
And [the] cities of fortification [are] Ziddim Zer and Hammath Rakkath and Kinnereth.
36 Adama, Rama, Hazori,
And Adamah and Ramah and Hazor.
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
And Kedesh and Edrei and En Hazor.
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
And Yiron and Migdal El Horem and Beth Anath and Beth Shemesh cities nine-teen and villages their.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
This [was] [the] inheritance of [the] tribe of [the] descendants of Naphtali to clans their the cities and villages their.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
For [the] tribe of [the] descendants of Dan to clans their it came out the lot seventh.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
And it was [the] territory of inheritance their Zorah and Eshtaol and Ir-Shemesh.
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
And Shaalabbin and Aijalon and Ithlah.
43 Eloni, Timna, Ekroni,
And Elon and Timnah and Ekron.
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
And Eltekeh and Gibbethon and Baalath.
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
And Jehud and Bene Berak and Gath Rimmon.
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
And [the] waters of Jarkon and Rakkon with the territory opposite to Joppa.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
And it went out [the] territory of [the] descendants of Dan from them and they went up [the] descendants of Dan and they waged war with Leshem and they captured it - and they struck it to [the] mouth of [the] sword and they took possession of it and they dwelt in it and they called Leshem Dan according to [the] name of Dan ancestor their.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
This [was] [the] inheritance of [the] tribe of [the] descendants of Dan to clans their the cities these and villages their.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
And they finished to divide for possession the land to borders its and they gave [the] people of Israel an inheritance to Joshua [the] son of Nun in midst of them.
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
On [the] mouth of Yahweh they gave to him the city which he asked for Timnath Serah in [the] hill country of Ephraim and he built the city and he dwelt in it.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
These [are] the inheritances which they gave as a possession Eleazar the priest - and Joshua [the] son of Nun and [the] leaders of the fathers of [the] tribes of [the] people of Israel - by lot - at Shiloh before Yahweh [the] entrance of [the] tent of meeting and they finished from apportioning the land.

< Yoshua 19 >