< Yohana 9 >

1 Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
Jésus vit, en passant, un aveugle de naissance.
2 Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
« Maître, lui demandèrent ses disciples, est-ce que cet homme a péché, ou ses parents, pour qu’il soit né aveugle? »
3 Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
Jésus répondit: « Ni lui, ni ses parents n’ont péché, mais c’est afin que les œuvres de Dieu soient manifestées en lui.
4 Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
Il faut, tandis qu’il est jour, que je fasse les œuvres de celui qui m’a envoyé; la nuit vient, où personne ne peut travailler.
5 Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
Pendant que je suis dans le monde, je suis la lumière du monde. » —
6 Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
Ayant ainsi parlé, il cracha à terre, fit de la boue avec sa salive, puis il l’étendit sur les yeux de l’aveugle,
7 Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
et lui dit: « Va, lave-toi dans la piscine de Siloé (mot qui se traduit: Envoyé). » Il partit, se lava, et s’en retourna voyant clair.
8 Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
Les voisins, et ceux qui l’avaient vu auparavant demander l’aumône, disaient: « N’est-ce pas là celui qui était assis et mendiait? »
9 Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
Les uns répondaient: « C’est lui »; d’autres: « Non, mais il lui ressemble. » Mais lui disait: « C’est moi. »
10 Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
Ils lui dirent donc: « Comment tes yeux ont-ils été ouverts? »
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
Il répondit: « Un homme, celui qu’on appelle Jésus, a fait de la boue, il l’a étendue sur mes yeux, et m’a dit: Va à la piscine de Siloé et lave-toi. J’y ai été, et, m’étant lavé, j’ai recouvré la vue. —
12 Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
Où est cet homme? « lui dirent-ils. Il répondit: « Je ne sais pas. »
13 Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
Ils menèrent aux Pharisiens celui qui avait été aveugle.
14 Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
Or, c’était un jour de sabbat que Jésus avait ainsi fait de la boue et ouvert les yeux de l’aveugle.
15 Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
À leur tour, les Pharisiens lui demandèrent comment il avait recouvré la vue, et il leur dit: « Il m’a mis sur les yeux de la boue, je me suis lavé, et je vois. »
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
Sur cela, quelques-uns des Pharisiens disaient: « Cet homme n’est pas envoyé de Dieu, puisqu’il n’observe pas le sabbat. » D’autres disaient: « Comment un pécheur peut-il faire de tels prodiges? » Et la division était entre eux.
17 Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
Ils dirent donc de nouveau à l’aveugle: « Et toi, que dis-tu de lui, de ce qu’il t’a ouvert les yeux? » Il répondit: « C’est un prophète. »
18 Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
Les Juifs ne voulurent donc pas croire que cet homme eut été aveugle et qu’il eût recouvré la vue, jusqu’à ce qu’ils eussent fait venir les parents de celui qui avait recouvré la vue.
19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
Ils leur demandèrent: « Est-ce là votre fils, que vous dites être né aveugle? Comment donc voit-il maintenant? »
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
Ses parents répondirent: « Nous savons que c’est bien là notre fils, et qu’il est né aveugle;
21 Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
mais comment il voit maintenant, nous l’ignorons, et qui lui a ouvert les yeux, nous ne le savons pas. Interrogez-le lui-même; il a de l’âge, lui-même parlera de ce qui le concerne. »
22 Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
Ses parents parlèrent ainsi, parce qu’ils craignaient les Juifs. Car déjà les Juifs étaient convenus que quiconque reconnaîtrait Jésus pour le Christ serait exclu de la synagogue.
23 Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
C’est pourquoi ses parents dirent: « Il a de l’âge, interrogez-le. »
24 Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
Les Pharisiens firent venir une seconde fois l’homme qui avait été aveugle, et lui dirent: « Rends gloire à Dieu. Nous savons que cet homme est un pécheur. »
25 Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
Celui-ci répondit: « S’il est un pécheur, je l’ignore; je sais seulement que j’étais aveugle, et qu’à présent je vois. »
26 Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Ils lui dirent: « Qu’est-ce qu’il t’a fait? Comment t’a-t-il ouvert les yeux? »
27 Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
Il leur répondit: « Je vous l’ai déjà dit et vous ne l’avez pas écouté: pourquoi voulez-vous l’entendre encore? Est-ce que, vous aussi, vous voulez devenir ses disciples? »
28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
Ils le chargèrent alors d’injures, et dirent: « C’est toi qui es son disciple; pour nous, nous sommes disciples de Moïse.
29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
Nous savons que Dieu a parlé à Moïse; mais celui-ci, nous ne savons d’où il est. »
30 Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
Cet homme leur répondit: « Il est étonnant que vous ne sachiez pas d’où il est, et cependant il m’a ouvert les yeux.
31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
Nous savons que Dieu n’exauce point les pécheurs; mais si quelqu’un l’honore et fait sa volonté, c’est celui-là qu’il exauce.
32 Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
Jamais on n’a ouï dire que quelqu’un ait ouvert les yeux d’un aveugle-né. (aiōn g165)
33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
Si cet homme n’était pas de Dieu, il ne pourrait rien faire. »
34 Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
Ils lui répondirent: « Tu es né tout entier dans le péché, et tu nous fais la leçon? » Et ils le chassèrent.
35 Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
Jésus apprit qu’ils l’avaient ainsi chassé, et l’ayant rencontré, il lui dit: « Crois-tu au Fils de l’homme? »
36 Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
Il répondit: « Qui est-il, Seigneur, afin que je croie en lui? »
37 Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
Jésus lui dit: « Tu l’as vu; et celui qui te parle, c’est lui-même. » —
38 Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
« Je crois, Seigneur » dit-il; et se jetant à ses pieds, il l’adora.
39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
Alors Jésus dit: « Je suis venu dans ce monde pour un jugement, afin que ceux qui ne voient pas voient, et que ceux qui voient deviennent aveugles. »
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
Quelques Pharisiens qui étaient avec lui, lui dirent: « Sommes-nous, nous aussi des aveugles? »
41 Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
Jésus leur répondit: « Si vous étiez des aveugles, vous n’auriez point de péché; mais maintenant vous dites: Nous voyons; votre péché demeure. »

< Yohana 9 >