< Yohana 9 >

1 Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
And as Iesus passed by he sawe a man which was blynde from his birth.
2 Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
And his disciples axed him sayinge. Master who dyd synne: this man or his father and mother that he was borne blynde?
3 Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
Iesus answered: Nether hath this man synned nor yet his father and mother: but that the workes of God shuld be shewed on him.
4 Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
I must worke the workes of him that sent me whyll it is daye. The nyght cometh when no man can worke.
5 Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
As longe as I am in the worlde I am the lyght of the worlde.
6 Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
Assone as he had thus spoken he spate on the grounde and made claye of the spetle and rubbed the claye on the eyes of the blynde
7 Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
and sayde vnto him: Goo wesshe the in ye pole of Syloe which by interpretacion signifieth sent. He went his waye and wasshed and cam agayne seinge.
8 Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
The neghboures and they that had sene him before how that he was a begger sayde: is not this he that sate and begged?
9 Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
Some sayde: this is he. Other sayd: he is lyke him. But he him selfe sayde: I am even he.
10 Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
They sayde vnto him: How are thyne eyes opened then?
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
He answered and sayde. The ma that is called Iesus made claye and anoynted myne eyes and sayd vnto me: Goo to the pole Syloe and wesshe. I went and wesshed and receaved my syght.
12 Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
They sayde vnto him: where is he? He sayde: I cannot tell.
13 Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
Then brought they to ye pharises him that a lytell before was blynde:
14 Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
for it was the Saboth daye when Iesus made the claye and opened his eyes.
15 Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
Then agayne the pharises also axed him how he had receaved his syght. He sayde vnto the: He put claye apon myne eyes and I wasshed and do se.
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
Then sayde some of the pharises: this man is not of God because he kepeth not the saboth daye. Other sayde: how can a man yt is a synner do suche myracles? And ther was stryfe amonge the.
17 Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
Then spake they vnto the blynde agayne: What sayst thou of him because he hath openned thyne eyes? And he sayd: He is a Prophet.
18 Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
But the Iewes dyd not beleve of the felowe how that he was blynde and receaved his syght vntyll they had called the father and mother of him that had receaved his syght.
19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
And they axed the saying: Is this youre sonne whome ye saye was borne blynde? How doth he now se then?
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
His father and mother answered them and sayde: we wote well that this is oure sonne and that he was borne blynde:
21 Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
but by what meanes he now seith that can we not tell or who hath opened his eyes can we not tell. He is olde ynough axe him let him answer for him selfe.
22 Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
Suche wordes spake his father and mother because they feared the Iewes. For the Iewes had conspyred all redy that yf eny man dyd confesse that he was Christ he shuld be excommunicat out of the synagoge.
23 Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
Therefore sayde his father and mother: he is olde ynough axe him.
24 Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
Then agayne called they the man that was blynde and sayd vnto him: Geve God the prayse: we knowe that this man is a synner.
25 Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
He answered and sayde: Whyther he be a synner or noo I cannot tell: One thinge I am sure of that I was blynde and now I se.
26 Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Then sayde they to him agayne. What dyd he to the? How opened he thyne eyes?
27 Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
He answered them I tolde you yerwhyle and ye dyd not heare. Wherfore wolde ye heare it agayne? Will ye also be his disciples?
28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
Then rated they him and sayde: Thou arte his disciple. We be Moses disciples.
29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
We are sure that God spake with Moses. This felowe we knowe not from whence he is.
30 Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
The man answered and sayde vnto them: this is a merveleous thinge that ye wote not whence he is seinge he hath opened myne eyes.
31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
For we be sure that God heareth not synners. But yf eny man be a worshipper of God and do his will him heareth he.
32 Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
Sence ye worlde beganne was it not hearde yt eny man opened the eyes of one that was borne blynd. (aiōn g165)
33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
If this man were not of God he coulde have done no thinge.
34 Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
They answered and sayd vnto him: thou arte altogeder borne in synne: and dost thou teache vs? And they cast him out.
35 Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
Iesus hearde that they had excommunicate him: and assone as he had founde him he sayd vnto him: doest thou beleve on the sonne of God?
36 Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
He answered and sayde: Who is it Lorde that I myght beleve on him?
37 Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
And Iesus sayde vnto him: Thou hast sene him and he it is that talketh with the.
38 Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
And he sayde: Lorde I beleve: and worshipped him.
39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
Iesus sayde: I am come vnto iudgement into this worlde: that they which se not myght se and they which se myght be made blynde.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
And some of the pharises which were with him hearde these wordes and sayde vnto him: are we then blynde?
41 Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
Iesus sayde vnto them: yf ye were blynde ye shuld have no synne. But now ye saye we se therfore youre synne remayneth.

< Yohana 9 >