< Yohana 9 >
1 Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
And passing by He saw a man blind from birth.
2 Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
And asked Him the disciples of Him saying; Rabbi, who sinned, this [man] or the parents of him, that blind he may be born?
3 Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
Answered (*k*) Jesus; Neither this [man] sinned nor [sinned] the parents of him, but [it was] that may be displayed the works of God in him.
4 Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
(Us *N(K)O*) it behooves to work the works of the [One who] having sent Me while day it is; is coming night, when no [one] is able to work.
5 Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
While in the world I may be, [the] light I am of the world.
6 Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
These things having said He spat on [the] ground and He made clay of the spittle and (he rubbed *NK(O)*) (on him *no*) the clay to the eyes (of the blind *k*)
7 Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
And He said to him; do go do wash yourself in the pool of Siloam which means Sent. He went therefore and washed and came [back] seeing.
8 Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
The therefore neighbours and those having seen him before that (a beggar *N(K)O*) he was, were saying; Surely this is the [one] sitting and begging?
9 Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
Some were saying that He it is, but others were saying; (No, *no*) (but *N(k)O*) (that *k*) like as him he is. He was saying that I myself am [he].
10 Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
They were saying therefore to him; How (then *NO*) were opened of you the eyes?
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
Answered He (and said: *k*) (The *no*) man (who *no*) is being named Jesus clay made and He anointed my eyes and He said to me (that *no*) do go to (pool *k*) (*N(k)O*) Siloam and do wash. yourself Having gone (therefore *N(K)O*) and having washed I received sight.
12 Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
(And *N(k)O*) they said to him; Where is He? He says; Not I know.
13 Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
They bring him to the Pharisees who once [was] blind;
14 Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
Was now Sabbath (in which day *NO*) (when *k*) the clay made Jesus and opened of him the eyes.
15 Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
Again therefore were asking him also the Pharisees how he had received sight. And he said to them; Clay He put on my eyes and I washed and I see.
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
Were saying therefore of the Pharisees some; Not is this from (*k*) God the man for the Sabbath not He does keep. Others (however *no*) were saying; How is able a man sinful such signs to do? And division there was among them.
17 Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
They say (therefore *NO*) to the blind [man] again; What you yourself say concerning Him for He opened of you the eyes? And he said that A prophet He is.
18 Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
Not did believe then the Jews concerning him that he was being blind and received sight until when they called the parents of him who having received sight,
19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
And they asked them saying; This is the son of you of whom you yourselves say that blind he was born? How then does he see presently
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
Answered (therefore *N(k)*) (to them *k*) the parents of him and said; We know that this is the son of us and that blind he was born;
21 Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
How however presently he sees not we know, or who opened of him the eyes we ourselves not know; him do ask, (he himself *k*) [of] age is; He himself Concerning himself he will speak.
22 Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
These things said the parents of Him because they were afraid of the Jews; already for had agreed together the Jews that if anyone Him shall confess Christ, expelled from the synagogue he shall be.
23 Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
Because of this the parents of him said that Age he has, him (do question. *N(k)O*)
24 Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
They called therefore the man out a second time who were blind and they said to him; do give glory to God! We ourselves know that this man a sinner is.
25 Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
Answered then he (and said: *k*) Whether a sinner He is not I know; One [thing] I do know that blind being now I see.
26 Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
They said (therefore *N(k)O*) to him (again: *k*) What did He to you? How opened He of you the eyes?
27 Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
He answered them; I told you already, and not you did listen. Why again do you wish to hear? Surely not also you yourselves do wish His disciples to become?
28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
(And *n(o)*) ([they] now *o*) railed at (therefore *K*) him and said; You yourself a disciple are of that One, we ourselves however of Moses are disciples.
29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
We ourselves know that to Moses has spoken God, this [man] however not we know from where is.
30 Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
Answered the man and said to them; In this for (*no*) an amazing thing is that you yourselves not know from where He is, and yet (He opened *N(k)O*) my eyes.
31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
We know (now *k*) that to sinners God not does listen, but if anyone God-fearing shall be and the will of Him shall do, to him He listens.
32 Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn )
Out of the age never it has been heard that opened anyone [the] eyes of [one] blind born. (aiōn )
33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
only unless were this [man] from God, not He was able to do no [thing].
34 Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
They answered and they said to him; In sins you yourself were born entirely and you yourself teach us? And they cast him out.
35 Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
Heard (*ko*) Jesus that they had cast him out, and having found him He said (to him: *ko*) You yourself believe in the Son (of Man? *N(K)O*)
36 Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
Answered he and said; (And *no*) who is He, lord, that I may believe in Him?
37 Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
Said (now *k*) to him Jesus; Both You have seen Him, and the [One] speaking with you He is.
38 Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
And he was saying; I believe, Lord, And he worshiped Him.
39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
And said Jesus; For judgment I myself into world this came, that those not seeing may see and those seeing blind may become.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
(and *k*) Heard from the Pharisees these things who with Him being and they said to Him; Surely not also we ourselves blind are?
41 Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
Said to them Jesus; If blind you were, not then would you have sin. since however you say that We see, the (therefore *K*) sin of you remains.