< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
Por lo cual también se estremece mi corazón y salta fuera de su lugar.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
¡Escuchen atentamente el trueno de su voz y el estruendo que sale de su boca!
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Suelta sus relámpagos por debajo de todo el cielo, que llegan hasta los confines de la tierra.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Tras ellos ruge su voz. Truena ʼEL con voz majestuosa, y aunque sea oída su voz, no los detiene.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
ʼEL truena con voz maravillosa y hace cosas que no podemos comprender.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
A la nieve dice: Cae a la tierra. También a la lluvia y al aguacero torrencial.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Así hace que todo hombre se retire, para que todos los hombres reconozcan su obra.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Las bestias se meten en lugar de descanso y permanecen en sus guaridas.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
De su cámara viene la tormenta y el frío de los vientos del norte.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Por el soplo de ʼEL se forma el hielo y se congelan las amplias aguas.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Carga de humedad la densa nube. Dispersa las nubes con sus relámpagos,
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
que giran según su designio para cumplir sus órdenes sobre la superficie de la tierra habitada.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Las hace venir, unas veces como azote, otras, a favor de su tierra y otras por misericordia.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Oh Job, escucha esto. Detente y considera las maravillas de ʼEL.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
¿Sabes cuándo ʼEloah las establece y hace fulgurar la luz de su nube?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
¿Conoces tú el equilibrio de las nubes, las obras prodigiosas de Aquél que es perfecto en conocimiento?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
¿Por qué están calientes tus ropas cuando la tierra está tranquila a causa del viento del sur?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
¿Extendiste con Él la bóveda celeste, sólida como un espejo fundido?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Muéstranos qué le diremos. Porque no podemos ordenar nuestras ideas a causa de las tinieblas.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
¿Será necesario informarle lo que yo digo? ¿O debe un hombre desear que sea tragado?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Ciertamente no es posible mirar la luz oscurecida por las nubes, pero un viento pasa, y la despeja.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Del norte asoma un dorado resplandor. ¡En ʼEloha hay una asombrosa majestad!
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
¡ʼEL-Shadday, a Quien no alcanzamos! Exaltado en poder, Él no hará violencia a la equidad. Es abundante en justicia.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Por tanto, los hombres le temen. Él no estima a alguno que cree en su corazón ser sabio.

< Ayubu 37 >