< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
Then Elihu continued:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
“You [three] men who [think that you] [SAR] are very wise, hear me; listen to what I am saying, you men who [say that you] know so much.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
When we [SYN] hear what other people [like you] say, we [RHQ] think carefully about what they say [to determine what is good and what is bad], like we [SYN] taste food [to determine what is good].
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
We need to decide [who is saying] what is right and to determine among ourselves what is good/best.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Job has said, ‘I am innocent, but God has refused to judge me fairly/justly.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
Even though I have always done what is right, he is lying about me. Even though I have not done what is wrong, he has caused me to suffer, and I will certainly die.’
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
(Is there any person like Job, who insults others as easily as people accept a drink of water?/There is no person like Job, who insults others as easily as people accept a drink of water.) [RHQ]
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
He habitually associates with people who do what is evil and spends time with wicked people.
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
He has said, ‘It is useless for people to try to please God.’
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
“So, you men who [claim that you] understand everything, listen to me! Almighty God would never consider doing anything that is wicked or wrong [DOU]!
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
He (pays back/punishes) people for what they have done; he gives them what they deserve for the way that they have conducted their lives.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Truly, Almighty God never does what is wicked; he always [LIT] does what is fair/just.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
The authority that he has to rule everything on the earth, no one [RHQ] gave it to him; no one [RHQ] put him in control of the whole world. [He has always had that authority].
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
If he would take his spirit back to himself,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
everyone would die [immediately], and their corpses would soon become dirt again.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
“So, [Job], if [you say that you] understand everything, listen to what I am saying.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
God could certainly not [RHQ] govern the world if he hated doing what is fair/just. So, will you condemn God, who is righteous and powerful, [saying that what he has done is wrong]?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
He tells [some] kings that they are worthless, and he says to [some] officials that they are wicked.
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
He does not favor rulers [more than he favors others]; he does not favor rich people more than poor people, because he created all of them.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
People [often] die suddenly; he strikes them at midnight and they die; he even gets rid of mighty people without the help of any humans [SYN].
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
“He sees [MTY] everything that people do; [when we walk, ] he watches every step that we take.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
There is no gloom or darkness [DOU] that is so dark that sinners can hide [from him] in that darkness.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
God does not [need to] set a time when we will stand in front of him in order that he may judge us. [He can judge us whenever he wants to].
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
He destroys mighty people without [needing to] investigate [what they have done], and he appoints others to take their places.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Because he [already] knows what they have done, he removes them at night and gets rid of them.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Where [many] people can see it, he strikes/punishes them because of the wicked things that they have done;
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
he strikes them because they turned away from doing what he wanted them to do and did not pay attention to any of his commands.
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
They [mistreated] the poor people, with the result that those poor people cried out to God [for help], and he heard those afflicted people when they cried out [to him].
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
But if God decides to do nothing [to punish wicked people], no one can criticize/condemn him. If a godless/wicked man rules a nation, a man who tricks/deceives the people,
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
and if [God] hides his face [with the result that he does not see that ruler or punish him], no one will be able to prevent that ruler [from doing those things].
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
“Job, have you or anyone else ever said to God, ‘I have been punished [for my sins], and I will not sin any more;
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
so teach/show me what [sins I have committed]; if I have done anything that is evil, I will not do it any more’?
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
[Job, ] you object to what God has done to you, but do you think that he will do what you want him to do? It is you who must choose [what you say to God], not I; so tell me what you are thinking about this.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
“People who have good sense, those who are wise and who listen to what I say, will say to me,
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
‘Job is speaking ignorantly; what he says is nonsense.’
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
I think that Job should be taken to a court and (put on trial/judged), because he answers [us his friends] like wicked men would answer.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
To add to the [other] sins that he has committed, he is rebelling [against God]; he shows us that he does not respect God [IDM], making long speeches [saying that God has punished him unjustly].”

< Ayubu 34 >