< Ayubu 32 >
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Ona tri čovjeka prestadoše Jobu odgovarati, jer je on sebe smatrao nevinim.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Nato se rasrdi Elihu, sin Barakeelov, iz Buza, od plemena Ramova: planu gnjevom na Joba zato što je sebe držao pravednim pred Bogom;
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
a planu gnjevom i na tri njegova prijatelja jer nisu više našli ništa što bi odgovorili te su tako Boga osudili.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Dok su oni govorili s Jobom, Elihu je šutio, jer su oni bili stariji od njega.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Ali kad vidje da ona tri čovjeka nisu više imala odgovora u ustima, planu od srdžbe.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
I progovorivši, Elihu, sin Barakeelov, iz Buza, reče: “Po godinama svojim još mlad sam ja, a u duboku vi ste ušli starost; bojažljivo se zato ja ustezah znanje svoje pokazati pred vama.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Mišljah u sebi: 'Govorit će starost, mnoge godine pokazat će mudrost.'
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Uistinu, dah neki u ljudima, duh Svesilnog mudrim čini čovjeka.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Dob poodmakla ne daje mudrosti a niti starost pravednosti uči.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Zato vas molim, poslušajte mene da vam i ja znanje svoje izložim.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
S pažnjom sam vaše besjede pratio i razloge sam vaše saslušao dok ste tražili što ćete kazati.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Na vama moja sva bijaše pažnja, al' ne bi nikog da Joba pobije ni da mu od vas tko riječ opovrgne.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Nemojte reći: 'Na mudrost smo naišli! Bog će ga pobit jer čovjek ne može.'
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Nije meni on besjedu upravio: odvratit mu neću vašim riječima.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Poraženi, otpovrgnut ne mogu, riječi zapeše u grlu njihovu.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Čekao sam! Al', gle, oni ne zbore. Umukoše, ni riječ više da kažu!
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Na meni je da progovorim sada, znanje ću svoje i ja izložiti.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Riječi mnoge u meni naviru dok iznutra moj duh mene nagoni.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Gle, nutrina mi je k'o mošt zatvoren, k'o nova će se raspući mješina.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Da mi odlane, govorit ću stoga, otvorit ću usne i odvratit' vama.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Nijednoj strani priklonit se neću niti laskat ja namjeravam kome.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Laskati ja ne umijem nikako, jer smjesta bi me Tvorac moj smaknuo.