< Ayubu 31 >
1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
« J'ai fait un pacte avec mes yeux; comment dois-je alors regarder avec convoitise une jeune femme?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Car quelle est la part du Dieu d'en haut, et l'héritage du Tout-Puissant en haut?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
N'est-ce pas une calamité pour les injustes, et le désastre pour les ouvriers de l'iniquité?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Ne voit-il pas mes manières, et compter tous mes pas?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
« Si j'ai marché dans le mensonge, et mon pied s'est précipité vers la tromperie
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
(que je sois pesé dans une balance égale, afin que Dieu connaisse mon intégrité);
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
si mon pas s'est détourné du chemin, si mon cœur marchait après mes yeux, si une souillure s'est collée à mes mains,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Alors, que je sème, et qu'un autre mange. Oui, que le produit de mon champ soit arraché.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
« Si mon cœur a été séduit par une femme, et j'ai attendu à la porte de mon voisin,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
puis laisser ma femme moudre pour un autre, et laisser les autres dormir avec elle.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Car ce serait un crime odieux. Oui, ce serait une iniquité d'être puni par les juges,
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
car c'est un feu qui consume jusqu'à la destruction, et déracinerait toute mon augmentation.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
« Si j'ai méprisé la cause de mon serviteur masculin ou de ma servante, quand ils se sont disputés avec moi,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Que ferai-je donc quand Dieu se lèvera? Quand il me rendra visite, que lui répondrai-je?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
N'est-ce pas celui qui m'a fait dans le ventre de ma mère qui l'a fait? On ne nous a pas façonnés dans le ventre de notre mère?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
« Si j'ai privé les pauvres de leur désir, ou ont fait perdre les yeux de la veuve,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
ou avoir mangé mon morceau seul, et l'orphelin n'en a pas mangé
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(non, dès ma jeunesse, il a grandi avec moi comme avec un père, Je l'ai guidée depuis le ventre de ma mère);
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
si j'ai vu quelqu'un périr faute de vêtements, ou que les nécessiteux n'avaient pas de couverture;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
si son cœur ne m'a pas béni, s'il n'a pas été réchauffé avec la toison de mon mouton;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
si j'ai levé la main sur l'orphelin, parce que j'ai vu mon aide dans le portail;
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
puis j'ai laissé tomber mon épaule à partir de l'omoplate, et que mon bras soit brisé jusqu'à l'os.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Car la calamité de Dieu est pour moi une terreur. A cause de sa majesté, je ne peux rien faire.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
« Si j'ai fait de l'or mon espoir, et ont dit à l'or fin: « Tu es ma confiance ».
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
Si je me suis réjoui parce que ma richesse était grande, et parce que ma main était devenue beaucoup;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
si j'ai vu le soleil quand il brillait, ou la lune qui se déplace dans la splendeur,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
et mon cœur a été secrètement séduit, et ma main a jeté un baiser de ma bouche;
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
ce serait aussi une iniquité à punir par les juges, car j'aurais renié le Dieu qui est là-haut.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
« Si je me suis réjoui de la destruction de celui qui me haïssait, ou soulevé moi-même quand le mal l'a trouvé
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
(Je n'ai certes pas permis à ma bouche de pécher en demandant sa vie avec une malédiction);
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
si les hommes de ma tente n'ont pas dit, Qui peut trouver quelqu'un qui n'a pas été rassasié de sa viande?
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
(l'étranger n'a pas campé dans la rue, mais j'ai ouvert mes portes au voyageur);
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
si, comme Adam, j'ai couvert mes transgressions, en cachant mon iniquité dans mon cœur,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
car je craignais la grande foule, et le mépris des familles me terrifiait, alors j'ai gardé le silence, et je n'ai pas franchi la porte...
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
oh que j'en ai un pour m'entendre! Voici ma signature! Que le Tout-Puissant me réponde! Laissez l'accusateur écrire mon acte d'accusation!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Je la porterais sûrement sur mon épaule, et je l'attacherais à moi comme une couronne.
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Je lui déclarais le nombre de mes pas. Je m'approcherais de lui comme un prince.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Si mon pays crie contre moi, et ses sillons pleurent ensemble;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
si j'ai mangé ses fruits sans argent, ou ont causé la mort de leurs propriétaires,
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
laisser pousser des roncesà la place du blé, et du tabouret des champs à la place de l'orge. » Les paroles de Job sont terminées.