< Yeremia 9 >
1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Oh, si ma tête était des eaux, et mes yeux une source de larmes, pour que je puisse pleurer jour et nuit pour les morts de la fille de mon peuple!
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Oh que j'ai eu dans le désert un lieu d'hébergement pour les voyageurs, pour que je puisse quitter mon peuple et partir d'eux! Car ils sont tous adultères, une assemblée d'hommes perfides.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
« Ils plient leur langue, comme leur arc, pour le mensonge. Ils sont devenus forts dans le pays, mais pas pour la vérité; car ils vont du mal au mal, et ils ne me connaissent pas », dit Yahvé.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
« Que chacun prenne garde à son prochain, et n'ayez pas confiance en un frère; pour chaque frère supplantera complètement, et chaque voisin se promènera comme un calomniateur.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
Les amis se trompent les uns les autres, et ne veulent pas dire la vérité. Ils ont appris à leur langue à dire des mensonges. Ils se fatiguent à commettre l'iniquité.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Ta demeure est au milieu de la tromperie. Par la tromperie, ils refusent de me connaître, dit Yahvé.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
C'est pourquoi Yahvé des Armées dit, « Voici, je vais les faire fondre et les mettre à l'épreuve; car comment dois-je traiter la fille de mon peuple?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
Leur langue est une flèche mortelle. Il parle de tromperie. On parle pacifiquement à son prochain avec sa bouche, mais dans son cœur, il attend de lui tendre une embuscade.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Ne devrais-je pas les punir pour ces choses? dit l'Éternel. « Mon âme ne devrait-elle pas être vengée sur une nation telle que celle-ci?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
Je pleurerai et gémirai sur les montagnes, et se lamenter sur les pâturages du désert, car ils sont brûlés, de sorte que personne ne passe; Les hommes ne peuvent pas entendre la voix du bétail. Les oiseaux du ciel et les animaux ont fui. Ils sont partis.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
« Je ferai des monceaux de Jérusalem, un lieu de résidence pour les chacals. Je ferai des villes de Juda une désolation, sans habitant. »
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Qui est assez sage pour comprendre cela? Qui est celui à qui la bouche de Yahvé a parlé, pour qu'il l'annonce? Pourquoi le pays a-t-il péri et s'est-il consumé comme un désert, pour que personne n'y passe?
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
Yahvé dit: « Parce qu'ils ont abandonné la loi que j'avais mise devant eux, parce qu'ils n'ont pas écouté ma voix et n'ont pas marché dans mes voies,
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
mais parce qu'ils ont marché selon l'obstination de leur cœur et selon les Baals que leurs pères leur ont enseignés. »
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
C'est pourquoi l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici, je vais nourrir ce peuple d'absinthe et lui donner à boire de l'eau empoisonnée.
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
Je les disperserai parmi les nations, que ni eux ni leurs pères n'ont connues. J'enverrai l'épée après eux, jusqu'à ce que je les aie consumés. »
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Yahvé des Armées dit, « Réfléchis, et appelle les femmes en deuil, pour qu'elles viennent. Faites venir les femmes habiles, qu'elles viennent.
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
Qu'ils se hâtent et se lamenter pour nous, que nos yeux puissent couler de larmes et nos paupières jaillissent d'eau.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
Car une voix de gémissement se fait entendre de Sion, Comme nous sommes ruinés! Nous sommes très déconcertés parce que nous avons abandonné le pays, parce qu'ils ont détruit nos maisons. »
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Pourtant, écoutez la parole de Yahvé, vous les femmes. Que ton oreille reçoive la parole de sa bouche. Apprenez à vos filles à gémir. Chacun apprend à son voisin une lamentation.
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
Car la mort est montée à nos fenêtres. Il est entré dans nos palais pour couper les enfants de l'extérieur, et les jeunes hommes de la rue.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Parlez: « Yahvé dit, "'Les cadavres des hommes tomberont comme du fumier sur le champ, et comme la poignée après la moissonneuse. Personne ne les rassemblera. »
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Yahvé dit, « Ne laissez pas le sage se glorifier de sa sagesse. Ne laissez pas l'homme puissant se glorifier de sa puissance. Ne laissez pas l'homme riche se glorifier de ses richesses.
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
Mais que celui qui se glorifie se glorifie de ceci, qu'il a de l'intelligence, et qu'il me connaît, que je suis Yahvé qui exerce la bonté, la justice et la droiture sur la terre, car je me réjouis de ces choses, dit Yahvé.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
« Voici, les jours viennent, dit Yahvé, où je punirai tous ceux qui ne sont circoncis que dans leur chair:
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
l'Égypte, Juda, Édom, les enfants d'Ammon, Moab, et tous ceux qui ont les coins de leurs cheveux coupés, qui habitent dans le désert; car toutes les nations sont incirconcises, et toute la maison d'Israël est incirconcise de cœur. »