< Yeremia 51 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.
Thus he says Yahweh here I [am] about to rouse on Babylon and against [the] inhabitants Leb-qamai a wind a destroyer.
2 Nitawatuma wageni Babeli kumpepeta na kuiharibu nchi yake; watampinga kila upande katika siku ya maafa yake.
And I will send to Babylon - strangers and they will winnow it and they may lay waste land its for they will be on it from round about on [the] day of calamity.
3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake, wala usimwache avae silaha zake. Usiwaonee huruma vijana wake; angamiza jeshi lake kabisa.
May not he bend (*Q(K)*) the [one] bending bow his and may not he lift in armor his and may not you spare young men its totally destroy all army its.
4 Wataanguka waliouawa katika Babeli, wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.
And they will fall slain in [the] land of [the] Chaldeans and pierced through in streets its.
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ingawa nchi yao imejaa uovu mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
For not [is] forsaken Israel and Judah from God its from Yahweh of hosts for land their it is full guilt from [the] holy [one] of Israel.
6 “Kimbieni kutoka Babeli! Okoeni maisha yenu! Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake. Ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa kile anachostahili.
Flee - from [the] midst of Babylon and save everyone life his may not you be destroyed in iniquity its for [is] a time of vengeance it for Yahweh recompense he [is] about to repay to it.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana; aliufanya ulimwengu wote ulewe. Mataifa walikunywa mvinyo wake; kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.
[was] a cup of Gold Babylon in [the] hand of Yahweh making drunk all the earth some of wine its they have drunk nations there-fore they are acting like mad people nations.
8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika. Mwombolezeni! Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake, labda anaweza kupona.
Suddenly it will fall Babylon and it was broken wail on it get balm for pain its perhaps it will be healed.
9 “‘Tungemponya Babeli, lakini hawezi kuponyeka; tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake inafika angani, inapanda juu hadi mawinguni.’
(We healed *Q(k)*) Babylon and not it was healed leave it so we may go everyone to own land his for it has reached to the heavens judgment its and it has been lifted up to [the] clouds.
10 “‘Bwana amethibitisha haki yetu; njooni, tutangaze katika Sayuni kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’
He has brought forth Yahweh righteousness our come so let us recount in Zion [the] work of Yahweh God our.
11 “Noeni mishale, chukueni ngao! Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi, kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli. Bwana atalipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Sharpen the arrows fill the shields he has roused Yahweh [the] spirit of [the] kings of Media for on Babylon purpose his [is] to destroy it for [is] [the] vengeance of Yahweh it [the] vengeance of temple his.
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli! Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi, andaeni waviziao! Bwana atatimiza kusudi lake, amri yake juu ya watu wa Babeli.
Against [the] walls of Babylon lift up a standard strengthen the watch station watchmen prepare the ambushers for both he has purposed Yahweh as well as he will do [that] which he spoke concerning [the] inhabitants of Babylon.
13 Wewe uishiye kando ya maji mengi na uliye na wingi wa hazina, mwisho wako umekuja, wakati wako wa kukatiliwa mbali.
(O [one who] dwells *Q(k)*) at waters many greatness of treasures it has come end your [the] cubit of cutting off your.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: ‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige, nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’
He swears Yahweh of hosts by self his that except I will fill you person[s] like locust and they will sing to you a shout.
15 “Aliiumba dunia kwa uweza wake; akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.
[he] made [the] earth By power his [he] established [the] world by wisdom his and by understanding his he stretched out [the] heavens.
16 Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma, huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia. Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua, naye huuleta upepo kutoka ghala zake.
To [the] sound of giving forth he a tumult of waters in the heavens and he brought up clouds from [the] end of [the] earth lightning for the rain he makes and he brought out [the] wind from storehouses his.
17 “Kila mtu ni mjinga na hana maarifa; kila sonara ameaibishwa na sanamu zake. Vinyago vyake ni vya udanganyifu, havina pumzi ndani yavyo.
He is stupid every person from knowledge he is put to shame every metalsmith from [the] idol for [is] deception molten image his and not breath [is] in them.
18 Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha, hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.
[are] futility They a work of mockery at [the] time of punishment their they will perish.
19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo, kwani ndiye Muumba wa vitu vyote, pamoja na kabila la urithi wake: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
Not [is] like these [the] portion of Jacob for [is [the] one who] formed everything he and [the] tribe of inheritance his [is] Yahweh of hosts name his.
20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita, silaha yangu ya vita: kwa wewe navunjavunja mataifa, kwa wewe naangamiza falme,
[are] a war-club You of me weapons of war and I smash by you nations and I destroy by you kingdoms.
21 kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake,
And I smash by you horse and rider its and I smash by you chariotry and rider[s] its.
22 kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke, kwa wewe napondaponda mzee na kijana, kwa wewe napondaponda kijana wa kiume na mwanamwali,
And I smash by you man and woman and I smash by you old [man] and young man and I smash by you young man and young woman.
23 kwa wewe nampondaponda mchungaji na kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa.
And I smash by you shepherd and flock his and I smash by you a farmer and team his and I smash by you governors and officials.
24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.
And I will repay to Babylon and to all - [the] inhabitants of Chaldea all evil their which they did in Zion to eyes your [the] utterance of Yahweh.
25 “Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu, wewe uangamizaye dunia yote,” asema Bwana. “Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako, nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba, na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.
Here I [am] against you O mountain of destruction [the] utterance of Yahweh who destroys all the earth and I will stretch out hand my on you and I will roll you from the crags and I will make you into a mountain of burning.
26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni, wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi, kwa maana utakuwa ukiwa milele,” asema Bwana.
And not people will take from you stone for a corner and stone for foundations for wastes of perpetuity you will be [the] utterance of Yahweh.
27 “Twekeni bendera katika nchi! Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa! Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, iteni falme hizi dhidi yake: Ararati, Mini na Ashkenazi. Wekeni jemadari dhidi yake, pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.
Lift up a standard in the land blow a trumpet among the nations consecrate on it nations summon on it [the] kingdoms of Ararat Minni and Ashkenaz appoint on it an official bring up horse[s] like a locust bristly.
28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, wafalme wa Wamedi, watawala wao na maafisa wao wote, pamoja na nchi zote wanazotawala.
Consecrate on it nations [the] kings of Media governors its and all officials its and all [the] land of dominion his.
29 Nchi inatetemeka na kugaagaa, kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama: yaani, kuangamiza nchi ya Babeli ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.
And it quaked the land and it writhed for it will be fulfilled on Babylon [the] plans of Yahweh to make [the] land of Babylon into a waste from not inhabitant.
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana, wamebaki katika ngome zao. Nguvu zao zimekwisha, wamekuwa kama wanawake. Makazi yake yameteketezwa kwa moto, makomeo ya malango yake yamevunjika.
They will cease [the] warriors of Babylon to fight they will remain in the strongholds it will be dry strength their they will become women they will be set on fire dwellings its they will be broken bars its.
31 Tarishi mmoja humfuata mwingine, na mjumbe humfuata mjumbe, kumtangazia mfalme wa Babeli kwamba mji wake wote umetekwa,
A runner to meet a runner he will run and a messenger to meet a messenger to tell to [the] king of Babylon that it has been captured city his from [the] end.
32 Vivuko vya mito vimekamatwa, mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto, nao askari wameingiwa na hofu kuu.”
And the fords they have been seized and the reed-marshes they have burned with fire and [the] men of war they are terrified.
33 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria wakati inapokanyagwa; wakati wa kumvuna utakuja upesi.”
For thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel [the] daughter of Babylon [will be] like a threshing floor a time [when] someone treads down it yet a little and it will come [the] time of the harvest to it.
34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula, ametufanya tuchangayikiwe, ametufanya tuwe gudulia tupu. Kama nyoka ametumeza na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri, kisha akatutapika.
(He devoured me he confused me *Q(K)*) Nebuchadnezzar [the] king of Babylon (he set down me *Q(K)*) a vessel of emptiness (he swallowed me *Q(K)*) like sea monster he filled belly his from delicacies my (he rinsed out me. *Q(K)*)
35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetu na iwe juu ya Babeli,” ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni. “Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,” asema Yerusalemu.
Violence my and flesh my [be] on Babylon she will say [the] inhabitant[s] of Zion and blood my [be] to [the] inhabitants of Chaldea it will say Jerusalem.
36 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo: “Tazama, nitatetea shauri lako na kulipiza kisasi kwa ajili yako; nitaikausha bahari yake na kuzikausha chemchemi zake.
Therefore thus he says Yahweh here I [am] about to conduct case your and I will avenge vengeance your and I will dry up sea its and I will make dry spring its.
37 Babeli utakuwa lundo la magofu na makao ya mbweha, kitu cha kutisha na kudharauliwa, mahali asipoishi mtu.
And it will become Babylon - heaps of stones - a habitation of jackals a horror and a hissing from not inhabitant.
38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo, wanakoroma kama wana simba.
Together like young lions they roar they growl like cubs of lions.
39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa, nitawaandalia karamu na kuwafanya walewe, ili wapige kelele kwa kicheko, kisha walale milele na wasiamke,” asema Bwana.
When getting heated they I will make feast their and I will make drunk them so that they may celebrate and they will sleep a sleep of perpetuity and not they will awake [the] utterance of Yahweh.
40 “Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi.
I will bring down them like lambs to slaughter like rams with goats.
41 “Tazama jinsi Sheshaki atakamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!
How! it will be captured Sheshach and it has been seized [the] praise of all the earth how! it will become a horror Babylon among the nations.
42 Bahari itainuka juu ya Babeli; mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.
It will go up over Babylon the sea with [the] tumult of waves its it will be covered.
43 Miji yake itakuwa ukiwa, kame na jangwa, nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake, ambayo hakuna mtu anayepita humo.
They will become cities its a waste a land dry and a desert plain a land [where] not he will dwell in them any person and not he will pass in them a child of humankind.
44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli, na kumfanya atapike kile alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kwake. Nao ukuta wa Babeli utaanguka.
And I will visit [judgment] on Bel in Babylon and I will bring out swallowed thing his from mouth his and not they will stream to him again nations also [the] wall of Babylon it will fall.
45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu! Okoeni maisha yenu! Ikimbieni hasira kali ya Bwana.
Come out from [the] midst of it O people my and save everyone life his from [the] burning of [the] anger of Yahweh.
46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi zitakaposikika katika nchi; tetesi moja inasikika mwaka huu, nyingine mwaka unaofuata; tetesi juu ya jeuri katika nchi, na ya mtawala dhidi ya mtawala.
And lest it should be weak heart your so you may fear at the report which is being heard in the land and it will come in the year the report and after it in the year the report and violence [will be] in the land and ruler [will be] on ruler.
47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia nitakapoziadhibu sanamu za Babeli; nchi yake yote itatiwa aibu, na watu wake wote waliouawa wataangukia ndani yake.
Therefore here! days [are] coming and I will visit [judgment] on [the] images of Babylon and all land its it will be ashamed and all slain [ones] its they will fall in [the] midst of it.
48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli, kwa kuwa kutoka kaskazini waharabu watamshambulia,” asema Bwana.
And they will cry out for joy on Babylon heaven and earth and all that [is] in them for from [the] north he will come to it the destroyers [the] utterance of Yahweh.
49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli, kama vile waliouawa duniani kote walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.
Both Babylon [is] to fall [those] slain of Israel as well as for Babylon they have fallen [those] slain of all the earth.
50 Wewe uliyepona upanga, ondoka wala usikawie! Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali, na utafakari juu ya Yerusalemu.”
O escapees from [the] sword go may not you stand still remember from a distant [land] Yahweh and Jerusalem let it come up on heart your.
51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa na aibu imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”
We are ashamed for we have heard scorn it has covered ignominy faces our for they have gone strangers to [the] holy places of [the] house of Yahweh.
52 “Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapoadhibu sanamu zake, na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.
Therefore here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and I will visit [judgment] on images its and in all land its he will groan [the] fatally wounded.
53 Hata kama Babeli ikifika angani na kuziimarisha ngome zake ndefu, nitatuma waharabu dhidi yake,” asema Bwana.
If it will go up Babylon the heavens and if it will fortify [the] height of strength its from with me they will come destroyers to it [the] utterance of Yahweh.
54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli, sauti ya uharibifu mkuu kutoka nchi ya Wakaldayo.
[the] sound of A cry of distress from Babylon and destruction great from [the] land of [the] Chaldeans.
55 Bwana ataiangamiza Babeli, atanyamazisha makelele ya kishindo chake. Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu, ngurumo ya sauti zao itavuma.
For [is] about to destroy Yahweh Babylon and he will destroy from it a sound great and they will roar waves their like waters many it will be given [the] uproar of voice their.
56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli, mashujaa wake watakamatwa, nazo pinde zao zitavunjwa. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi, yeye atalipiza kikamilifu.
For [is] about to come on it on Babylon a destroyer and they will be captured warriors its it will be shattered bows their for [is] a God of recompense Yahweh fully he will repay.
57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe, watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao; watalala milele na hawataamka,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will make drunk officials its and wise [people] its governors its and officials its and warriors its and they will sleep a sleep of perpetuity and not they will awake [the] utterance of the king [is] Yahweh of hosts name his.
58 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa, na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto; mataifa yanajichosha bure, taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”
Thus he says Yahweh of hosts [the] walls of Babylon broad utterly it will be demolished and gates its high with fire they will be kindled and they may labor peoples for [the] sufficiency of emptiness and peoples for [the] sufficiency of fire and they grow weary.
59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
The word which he commanded - Jeremiah the prophet Seraiah [the] son of Neriah [the] son of Mahseiah when went he with Zedekiah [the] king of Judah Babylon in [the] year fourth of reigning his and Seraiah [was] an official of a resting place.
60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.
And he wrote Jeremiah all the calamity which it will come to Babylon to a scroll one all the words these which were written concerning Babylon.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.
And he said Jeremiah to Seraiah when coming you Babylon and you will see and you will read aloud all the words these.
62 Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’
And you will say O Yahweh you you have spoken concerning the place this to cut off it to not to be in it an inhabitant from humankind and unto animal for desolations of perpetuity it will be.
63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati.
And it will be when finishing you to read aloud the scroll this you will tie on it a stone and you will throw it into [the] middle of [the] Euphrates.
64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
And you will say thus it will sink Babylon and not it will rise because of the calamity which I [am] about to bring on it and they will grow weary [are] to here [the] words of Jeremiah.

< Yeremia 51 >