< Yeremia 49 >
1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Des enfants d'Ammon. Yahvé dit: « Israël n'a-t-il pas de fils? N'a-t-il pas d'héritier? Pourquoi donc Malcam possède-t-il Gad, et son peuple habite dans ses villes?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
C'est pourquoi, voici que les jours viennent, » dit Yahvé, « que je ferai entendre une alarme de guerre contre Rabbah des enfants d'Ammon, et elle deviendra un tas de ruines, et ses filles seront brûlées par le feu; alors Israël possédera ceux qui l'ont possédé, » dit Yahvé.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
« Gémis, Hesbon, car Aï est dévastée! Pleurez, filles de Rabbah! Habille-toi d'une toile de sac. Se lamenter, et courir d'avant en arrière entre les clôtures; car Malcam ira en captivité, ses prêtres et ses princes ensemble.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Pourquoi vous vantez-vous dans les vallées, ta vallée fluide, fille rebelle? Vous avez fait confiance à ses trésors, en disant: « Qui viendra à moi?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Voici, je vais faire venir la terreur sur vous, » dit le Seigneur, Yahvé des Armées, « de tous ceux qui vous entourent. Vous serez tous chassés complètement, et il n'y aura personne pour rassembler les fugitifs.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
« Mais ensuite, je renverserai la captivité des enfants d'Ammon, » dit Yahvé.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Sur Edom, Yahvé des Armées dit: « La sagesse n'existe-t-elle plus à Teman? Le conseil a-t-il péri chez les prudents? Leur sagesse a-t-elle disparu?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Fuyez! Faites demi-tour! Habitez dans les profondeurs, habitants de Dedan; car je ferai venir sur lui la calamité d'Ésaü quand je le visiterai.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
Si des vendangeurs venaient chez vous, ne laisseraient-ils pas quelques raisins à glaner? Si les voleurs venaient la nuit, ne voleraient-ils pas jusqu'à ce qu'ils en aient assez?
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Mais j'ai dépouillé Ésaü, J'ai découvert ses endroits secrets, et il ne pourra pas se cacher. Sa progéniture est détruite, avec ses frères et ses voisins; et il n'est plus.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Laissez vos enfants sans père. Je vais les préserver en vie. Que vos veuves se confient en moi. »
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
Car Yahvé dit: « Voici, ceux à qui il n'appartenait pas de boire de la coupe vont certainement boire; et toi, es-tu celui qui restera impuni? Tu ne resteras pas impuni, mais tu boiras certainement.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
Car je l'ai juré par moi-même, dit l'Éternel, que Bozra sera un objet d'étonnement, d'opprobre, de désolation et de malédiction. Toutes ses villes seront des ruines perpétuelles. »
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
J'ai entendu des nouvelles de Yahvé, et un ambassadeur est envoyé parmi les nations, en disant: « Rassemblez-vous! Venez contre elle! Levez-vous pour la bataille! »
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
« Car voici, je t'ai rendu petit parmi les nations, et méprisé parmi les hommes.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Quant à ta terreur, l'orgueil de ton cœur t'a trompé, O vous qui habitez dans les fentes du rocher, qui détiennent la hauteur de la colline, mais tu devrais faire ton nid aussi haut que l'aigle, Je te ferai descendre de là, dit Yahvé.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
« Edom deviendra un objet d'étonnement. Tous ceux qui passeront devant seront étonnés, et sifflera à tous ses fléaux.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Comme lors du renversement de Sodome et Gomorrhe et de ses villes voisines, dit Yahvé, « aucun homme n'y habitera, aucun fils de l'homme n'y vivra.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
« Voici qu'il monte comme un lion de l'orgueil du Jourdain contre la demeure forte; car je les ferai fuir soudainement, et celui qui est choisi, Je le nommerai à ce poste. Car qui est comme moi? Qui me fixera une heure? Qui est le berger qui se tiendra devant moi? »
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Écoutez donc le conseil de l'Éternel, qu'il a pris contre Édom, et les desseins qu'il a conçus contre les habitants de Teman: Ils vont sûrement les traîner loin, les petits du troupeau. Il fera de leur habitation une désolation.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
La terre tremble au bruit de leur chute; il y a un cri, le bruit que l'on entend dans la Mer Rouge.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Voici qu'il s'élève et vole comme l'aigle, et il a déployé ses ailes contre Bozrah. Le cœur des puissants d'Édom, en ce jour, sera comme le cœur d'une femme en proie aux douleurs.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
de Damas: « Hamath et Arpad sont confondus, car ils ont entendu de mauvaises nouvelles. Ils ont fondu. Il y a du chagrin sur la mer. Ça ne peut pas être tranquille.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damas s'est affaiblie, elle se tourne vers la fuite, et le tremblement l'a saisie. L'angoisse et la tristesse se sont emparées d'elle, comme d'une femme en travail.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
Comment la ville de la louange n'est pas abandonnée, la ville de ma joie?
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
C'est pourquoi ses jeunes gens tomberont dans ses rues, et tous les hommes de guerre seront réduits au silence en ce jour-là, » dit Yahvé des Armées.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
« Je vais allumer un feu dans la muraille de Damas, et il dévorera les palais de Ben Hadad. »
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Sur Kédar et sur les royaumes de Hatsor, que Nebucadnetsar, roi de Babylone, a frappés, Yahvé dit: « Lève-toi, monte à Kedar, et détruire les enfants de l'est.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Ils prendront leurs tentes et leurs troupeaux. ils emporteront pour eux-mêmes leurs rideaux, tous leurs vaisseaux, et leurs chameaux; et ils leur crient: « Terreur de tous les côtés!
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Fuyez! Partez au loin! Habitez dans les profondeurs, habitants de Hatsor, dit Yahvé; « car Nebuchadnezzar, roi de Babylone, a pris conseil contre vous, et a conçu un dessein contre vous.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Levez-vous! Montez vers une nation qui est à l'aise, qui habite sans souci », dit Yahvé; « qui n'a ni portes ni barreaux, qui habite seul.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
Leurs chameaux seront un butin, et la multitude de leur bétail un butin. Je disperserai à tous les vents ceux qui ont les coins de leur barbe coupés; et j'amènerai leur calamité de chaque côté d'eux, » dit Yahvé.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Hatsor sera un repaire de chacals, une désolation pour toujours. Aucun homme n'y habitera, aucun fils de l'homme n'y vivra. »
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
Parole de Yahvé qui fut adressée à Jérémie, le prophète, au sujet d'Élam, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, en ces termes:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
« Yahvé des armées dit: « Voici, je vais briser l'arc d'Elam. le chef de leur force.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
Je ferai venir sur Élam les quatre vents des quatre coins du ciel, et les dispersera vers tous ces vents. Il n'y aura pas de nation où les parias d'Élam ne viendront pas.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
Je ferai en sorte que l'Élam soit consterné devant ses ennemis, et devant ceux qui cherchent leur vie. Je ferai venir sur eux le malheur, mon ardente colère, dit Yahvé; et j'enverrai l'épée après eux, jusqu'à ce que je les aie consommés.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
Je placerai mon trône en Élam, et je détruirai de là le roi et les princes, dit Yahvé.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
« Mais cela arrivera dans la suite des temps ». que je renverserai la captivité d'Élam, dit Yahvé. »