< Yeremia 47 >

1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:
Which it came [the] word of Yahweh to Jeremiah the prophet concerning [the] Philistines before he struck Pharaoh Gaza.
2 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini, yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana. Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake, miji na wale waishio ndani yake. Watu watapiga kelele; wote waishio katika nchi wataomboleza
Thus - he says Yahweh here! waters [are] rising from [the] north and they will become a torrent overflowing and they may overflow a land and what fills it a city and [those who] dwell in it and they will cry out everyone and he will wail every inhabitant of the land.
3 kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio, kwa sauti ya magari ya adui na mngurumo wa magurudumu yake. Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao, mikono yao italegea.
From [the] sound of [the] stamping of [the] hooves of mighty [horses] its from [the] rattling of chariotry its [the] din of wheels its not they have turned back fathers to children from slackness of hands.
4 Kwa maana siku imewadia kuwaangamiza Wafilisti wote na kuwakatilia mbali walionusurika wote ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni. Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti, mabaki toka pwani za Kaftori.
On the day which is coming to devastate all [the] Philistines to cut off to Tyre and to Sidon every survivor helping for [is] about to devastate Yahweh [the] Philistines [the] remnant of [the] coastland of Caphtor.
5 Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza, Ashkeloni atanyamazishwa. Enyi mabaki kwenye tambarare, mtajikatakata wenyewe mpaka lini?
It will come baldness to Gaza it will be silent Ashkelon O remnant of valley their until when? will you cut yourself.
6 “Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana, utaendelea mpaka lini ndipo upumzike? Rudi ndani ya ala yako; acha na utulie.’
Alas! O sword of Yahweh until when? not you will be inactive gather yourself to sheath your rest and be still.
7 Lakini upanga utatuliaje wakati Bwana ameuamuru, wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni pamoja na pwani yake?”
How? will you be inactive and Yahweh he has commanded it against Ashkelon and against [the] coast of the sea there he has appointed it.

< Yeremia 47 >