< Yeremia 42 >

1 Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
Alors tous les chefs des troupes, Jochanan, fils de Karéach, Jézania, fils d'Hoshaïa, et tout le peuple, depuis le plus petit jusqu'au plus grand, s'approchèrent,
2 Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
et dirent à Jérémie, le prophète: « Laisse, je te prie, notre supplication être présentée devant toi, et prie pour nous Yahvé ton Dieu, même pour tout ce reste, car nous ne sommes plus qu'un petit nombre parmi beaucoup, comme tes yeux le voient,
3 Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
afin que Yahvé ton Dieu nous montre le chemin que nous devons suivre et les choses que nous devons faire. »
4 Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
Alors Jérémie, le prophète, leur dit: « Je vous ai entendus. Voici, je vais prier Yahvé votre Dieu selon vos paroles, et il arrivera que tout ce que Yahvé vous répondra, je vous l'annoncerai. Je ne vous cacherai rien. »
5 Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
Et ils dirent à Jérémie: « Que Yahvé soit au milieu de nous un témoin vrai et fidèle, si nous n'agissons pas selon toute la parole que Yahvé, ton Dieu, t'envoie nous dire.
6 Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
Qu'elle soit bonne ou qu'elle soit mauvaise, nous obéirons à la voix de l'Éternel, notre Dieu, vers qui nous t'envoyons, afin que tout aille bien pour nous, quand nous obéissons à la voix de l'Éternel, notre Dieu. »
7 Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
Dix jours après, la parole de Yahvé fut adressée à Jérémie.
8 Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
Il appela Johanan, fils de Karéa, tous les chefs de troupes qui étaient avec lui, et tout le peuple, depuis le plus petit jusqu'au plus grand,
9 Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
et leur dit: « Yahvé, le Dieu d'Israël, à qui tu m'as envoyé présenter tes supplications devant lui, dit:
10 ‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
Si vous vivez encore dans ce pays, je vous bâtirai et ne vous abattrai pas, je vous planterai et ne vous arracherai pas, car je m'afflige de la détresse que je vous ai causée.
11 Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
Ne craignez pas le roi de Babylone, dont vous avez peur. N'aie pas peur de lui, dit Yahvé, car je suis avec toi pour te sauver et te délivrer de sa main.
12 Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
Je te ferai grâce, afin qu'il ait pitié de toi et que tu retournes dans ton pays.
13 “Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
« Mais si vous dites: Nous n'habiterons pas dans ce pays, et que vous n'obéissez pas à la voix de Yahvé votre Dieu,
14 nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
en disant: Non, mais nous irons au pays d'Égypte, où nous ne verrons pas la guerre, où nous n'entendrons pas le son de la trompette, où nous n'aurons pas faim de pain, et c'est là que nous habiterons »
15 basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
écoutez donc la parole de Yahvé, reste de Juda! Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Si vous vous décidez à entrer en Égypte et à y vivre,
16 basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
l'épée que vous craignez vous atteindra dans le pays d'Égypte, et la famine que vous redoutez vous suivra de près dans ce pays, et vous y mourrez.
17 Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
Il en sera de même pour tous les hommes qui auront pris le parti d'entrer en Égypte pour y vivre. Ils mourront par l'épée, par la famine et par la peste. Aucun d'eux ne restera ou n'échappera au malheur que je ferai venir sur eux'.
18 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
Car Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « De même que ma colère et ma fureur se sont déversées sur les habitants de Jérusalem, de même ma fureur se déversera sur vous, quand vous entrerez en Égypte; vous serez un objet d'horreur, d'étonnement, de malédiction et d'opprobre, et vous ne verrez plus ce lieu.
19 “Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
« Yahvé a parlé à votre sujet, reste de Juda: « N'allez pas en Égypte! ». Sachez bien que je vous ai rendu aujourd'hui ce témoignage.
20 kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
Car vous avez agi de façon trompeuse contre vos propres âmes; vous m'avez envoyé vers l'Éternel, votre Dieu, en disant: Priez pour nous l'Éternel, notre Dieu; et, selon tout ce que dit l'Éternel, notre Dieu, déclarez-le-nous, et nous le ferons.
21 Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
Je vous l'ai annoncé aujourd'hui, mais vous n'avez pas écouté la voix de l'Éternel, votre Dieu, dans tout ce pour quoi il m'a envoyé vers vous.
22 Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”
Maintenant, sachez donc avec certitude que vous mourrez par l'épée, par la famine et par la peste dans le lieu où vous voulez aller vivre. »

< Yeremia 42 >