< Yeremia 40 >

1 Neno likamjia Yeremia kutoka kwa Bwana baada ya Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme kumfungua huko Rama. Alikuwa amemkuta Yeremia akiwa amefungwa kwa minyororo miongoni mwa mateka wote kutoka Yerusalemu na Yuda waliokuwa wakipelekwa uhamishoni Babeli.
The word which it came to Jeremiah from with Yahweh after - set free him Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards from Ramah when took he him and he [was] bound with chains in among all [the] exile[s] of Jerusalem and Judah who were being taken into exile Babylon towards.
2 Kiongozi wa walinzi alipomwona Yeremia, akamwambia, “Bwana Mungu wako aliamuru maafa haya kwa mahali hapa.
And he took [the] chief of [the] bodyguards Jeremiah and he said to him Yahweh God your he spoke the harm this against the place this.
3 Sasa Bwana ameyaleta haya, amefanya sawasawa na vile alivyosema angefanya. Yote haya yametokea kwa sababu ninyi mlifanya dhambi dhidi ya Bwana na hamkumtii.
And he has brought [it] and he has done Yahweh just as he said for you sinned to Yahweh and not you listened to voice his and it has happened to you (the thing *Q(K)*) this.
4 Lakini leo ninakufungua minyororo iliyo kwenye viwiko vya mikono yako. Twende pamoja mpaka Babeli ikiwa unataka, nami nitakutunza. Lakini kama hutaki, basi usije. Tazama, nchi yote iko mbele yako, nenda kokote unakotaka.”
And now here! I have set free you this day from the chains which [are] on hand your if it is good in view your to come with me Babylon come so I may set eye my on you and if [is] displeasing in view your to come with me Babylon refrain see all the land [is] before you to [the place] good and to the [place] right in view your to go there towards go.
5 Lakini kabla Yeremia hajageuka kuondoka, Nebuzaradani akaongeza kusema, “Rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ambaye mfalme wa Babeli amemchagua awe juu ya miji ya Yuda, ukaishi naye miongoni mwa watu, au uende popote panapokupendeza.” Kisha huyo kiongozi akampa posho yake na zawadi, akamwacha aende zake.
And still he not he will return and return! to Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan whom he has appointed [the] king of Babylon over [the] cities of Judah and remain with him in among the people or to any [place] right in view your to go go and he gave to him [the] chief of [the] bodyguards a food allowance and a present and he let go him.
6 Kwa hiyo Yeremia akaenda kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa, na kuishi naye miongoni mwa watu walioachwa katika nchi.
And he went Jeremiah to Gedaliah [the] son of Ahikam Mizpah towards and he remained with him in among the people who remained in the land.
7 Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliokuwa bado wapo kwenye eneo la wazi waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia mwana wa Ahikamu kuwa mtawala wa nchi, na amemweka kuwa kiongozi wa wanaume, wanawake na watoto waliokuwa maskini zaidi katika nchi ambao hawakuchukuliwa kwenda uhamishoni Babeli,
And they heard all [the] commanders of the armies which [were] in the open country they and men their that he had appointed [the] king of Babylon Gedaliah [the] son of Ahikam over the land and that - he had appointed with him men and women and little one[s] and some of [the] poor people of the land from [those] who not they had been taken into exile Babylon towards.
8 wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani na Yonathani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi, wana wa Efai Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
And they came to Gedaliah Mizpah towards and Ishmael [the] son Nethaniah and Johanan and Jonathan [the] sons of Kareah and Seraiah [the] son of Tanhumeth and [the] sons of - (Ephai *Q(K)*) the Netophathite and Jezaniah [the] son of the Maacathite they and men their.
9 Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema: “Msiogope kuwatumikia Wakaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.
And he swore an oath to them Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan and to men their saying may not you be afraid from serving the Chaldeans remain in the land and serve [the] king of Babylon so it may go well for you.
10 Mimi mwenyewe nitakaa Mispa ili kuwawakilisha mbele ya Wakaldayo wanaotujia, lakini ninyi mtavuna divai, matunda ya kiangazi na mafuta, nanyi mtaweka katika vyombo vyenu vya kuhifadhia, na kuishi katika miji mliyojitwalia.”
And I here I [will be] dwelling at Mizpah to stand before the Chaldeans who they will come to us and you gather wine and summer fruit and oil and put [them] in vessels your and dwell in cities your which you have taken hold of.
11 Wayahudi wote waliokuwa Moabu, Amoni, Edomu na nchi nyingine zote waliposikia kwamba mfalme wa Babeli ameacha mabaki ya watu katika Yuda na amemweka Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kuwa mtawala wao,
And also all the Jews who [were] in Moab - and among [the] people of Ammon and in Edom and who [were] in all the lands they heard that he had given [the] king of Babylon a remnant to Judah and that he had appointed over them Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan.
12 wakarudi wote katika nchi ya Yuda kwa Gedalia huko Mispa, kutoka nchi zote ambazo walikuwa wametawanywa. Nao wakavuna divai na matunda tele wakati wa kiangazi.
And they returned all the Jews from all the places where they had been driven away there and they came [the] land of Judah to Gedaliah Mizpah towards and they gathered wine and summer fruit much exceedingly.
13 Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa bado wapo kwenye eneo la wazi wakamjia Gedalia huko Mispa
And Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies which [were] in the open country they came to Gedaliah Mizpah towards.
14 na kumwambia, “Je, hujui kwamba Baalisi mfalme wa Waamoni amemtuma Ishmaeli mwana wa Nethania akuue?” Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuwaamini.
And they said to him ¿ really do you know that Baalis - [the] king of [the] people of Ammon he has sent Ishmael [the] son of Nethaniah to strike you life and not he believed them Gedaliah [the] son of Ahikam.
15 Kisha Yohanani mwana wa Karea akamwambia Gedalia kwa siri huko Mispa, “Acha niende nikamuue Ishmaeli mwana wa Nethania, wala hakuna atakayejua. Kwa nini akuue na kusababisha Wayahudi wote waliokuzunguka watawanyike, na mabaki wa Yuda waangamie?”
And Johanan [the] son of Kareah he said to Gedaliah in secrecy at Mizpah saying let me go please and let me strike down Ishmael [the] son of Nethaniah and anyone not he will know why? will he strike you life and will they be scattered all Jews who have gathered to you and will it perish [the] remnant of Judah.
16 Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu akamwambia Yohanani mwana wa Karea, “Usifanye jambo kama hilo! Unalosema kuhusu Ishmaeli si kweli.”
And he said Gedaliah [the] son of Ahikam to Johanan [the] son of Kareah may not (you do *Q(k)*) the thing this for falsehood you [are] speaking concerning Ishmael.

< Yeremia 40 >