< Yeremia 4 >
1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
Si tu reviens, ô Israël, dit l’Éternel, reviens à moi; et si tu ôtes tes abominations de devant moi, tu ne seras plus errant,
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
et tu jureras en vérité, en jugement et en justice: L’Éternel est vivant! Et les nations se béniront en lui, et en lui elles se glorifieront.
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
Car ainsi dit l’Éternel aux hommes de Juda et à Jérusalem: Défrichez pour vous un terrain neuf, et ne semez pas au milieu des épines.
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Circoncisez-vous pour l’Éternel, et ôtez le prépuce de vos cœurs, hommes de Juda et habitants de Jérusalem, de peur que ma fureur ne sorte comme un feu et ne brûle, sans qu’il y ait personne pour l’éteindre, à cause de l’iniquité de vos actions.
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Annoncez en Juda, et faites entendre dans Jérusalem, et dites, … et sonnez de la trompette dans le pays; criez à plein gosier et dites: Assemblez-vous, et entrons dans les villes fortes.
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Élevez l’étendard vers Sion, fuyez, et ne vous arrêtez pas; car je fais venir du nord le mal et une grande ruine.
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
Le lion est monté de son fourré, et le destructeur des nations s’est mis en chemin; il est sorti de son lieu pour mettre ton pays en désolation: tes villes seront dévastées, de sorte qu’il n’y aura pas d’habitant.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
C’est pourquoi ceignez-vous de sacs, lamentez-vous, et hurlez; car l’ardeur de la colère de l’Éternel ne s’est point détournée de nous.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
Et il arrivera en ce jour-là, dit l’Éternel, que le cœur du roi défaillira et le cœur des princes, et que les sacrificateurs seront étonnés, et les prophètes stupéfaits.
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
Et je dis: Ah, Seigneur Éternel! certainement tu as bien trompé ce peuple et Jérusalem, en disant: Vous aurez la paix!… et l’épée est venue jusqu’à l’âme.
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
En ce temps-là, il sera dit à ce peuple et à Jérusalem: Un vent sec [vient] des hauteurs du désert, dans le chemin de la fille de mon peuple, non pour vanner, ni pour purifier.
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
Un vent plus véhément que celui-là viendra de par moi; maintenant, moi aussi je prononcerai [mes] jugements sur eux.
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Voici, il monte comme des nuées, et ses chars sont comme un tourbillon; ses chevaux, plus rapides que les aigles. Malheur à nous! car nous sommes détruits.
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
Lave ton cœur de l’iniquité, Jérusalem, afin que tu sois sauvée! Jusques à quand tes vaines pensées demeureront-elles au-dedans de toi?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
Car une voix annonce de Dan, et, de la montagne d’Éphraïm, publie l’affliction.
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
Faites savoir aux nations; voici, faites entendre à Jérusalem: Des assiégeants viennent d’un pays lointain et font retentir leur voix contre les villes de Juda.
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
Ils sont tout autour d’elle comme ceux qui gardent un champ; car elle s’est rebellée contre moi, dit l’Éternel.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
Ta voie et tes actions ont amené sur toi ces choses, c’est là ton iniquité; oui, c’est [une chose] amère; oui, elle pénètre jusqu’à ton cœur.
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
Mes entrailles! mes entrailles! je suis dans la douleur! Les parois de mon cœur! Mon cœur bruit au-dedans de moi, je ne puis me taire; car, mon âme, tu entends le son de la trompette, la clameur de la guerre!
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
Ruine sur ruine se fait entendre, car tout le pays est dévasté: soudain mes tentes sont dévastées, en un moment, mes courtines.
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
Jusques à quand verrai-je l’étendard, entendrai-je la voix de la trompette?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
Car mon peuple est fou, ils ne m’ont pas connu; ce sont des fils insensés, ils n’ont pas d’intelligence; ils sont sages pour faire le mal, mais ils ne savent pas faire le bien.
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
J’ai regardé la terre, et voici, elle était désolation et vide, et vers les cieux, et leur lumière n’était pas.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
J’ai regardé les montagnes, et voici, elles se remuaient, et toutes les collines branlaient.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
J’ai regardé, et voici, il n’y avait pas d’homme, et tous les oiseaux des cieux avaient fui.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
J’ai regardé, et voici, le Carmel était un désert, et toutes ses villes étaient renversées devant l’Éternel, devant l’ardeur de sa colère.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
Car ainsi dit l’Éternel: Tout le pays sera une désolation, mais je ne le détruirai pas entièrement.
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
À cause de cela, la terre mènera deuil, et, au-dessus, les cieux seront noirs, parce que je l’ai dit, je l’ai pensé, et je ne m’en repentirai point et je n’en reviendrai point.
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Devant le bruit des cavaliers et des tireurs d’arc toute ville fuit: ils entrent dans les fourrés et montent sur les rochers; toute ville est abandonnée, et aucun homme n’y habite.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
Et toi, dévastée, que feras-tu? Tu as beau te revêtir d’écarlate, te parer d’ornements d’or, te déchirer les yeux avec du fard, tu te fais belle en vain: les amants te méprisent, ils cherchent ta vie.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
Car j’ai entendu une voix comme celle d’une femme en travail, une angoisse comme d’une femme enfantant son premier-né, la voix de la fille de Sion; elle soupire, elle étend ses mains: Malheur à moi! car mon âme a défailli à cause des meurtriers!