< Yeremia 37 >

1 Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini mwana wa Yehoyakimu.
Sédécias, fils de Josias, régna comme roi à la place de Conias, fils de Jojakim, que Nebucadnetsar, roi de Babylone, avait établi roi dans le pays de Juda.
2 Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.
Mais ni lui, ni ses serviteurs, ni le peuple du pays n'écoutèrent les paroles de Yahvé, qu'il avait prononcées par le prophète Jérémie.
3 Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”
Le roi Sédécias envoya Jehucal, fils de Shelemia, et Sophonie, fils de Maaséja, le prêtre, au prophète Jérémie, pour lui dire: « Priez maintenant Yahvé notre Dieu pour nous. »
4 Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani.
Or Jérémie entrait et sortait au milieu du peuple, car on ne l'avait pas mis en prison.
5 Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.
L'armée de Pharaon était sortie d'Égypte; et lorsque les Chaldéens qui assiégeaient Jérusalem en eurent vent, ils se retirèrent de Jérusalem.
6 Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema:
Alors la parole de Yahvé fut adressée au prophète Jérémie, en ces termes:
7 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri.
« Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: Tu diras au roi de Juda, qui t'a envoyé vers moi pour me consulter: « Voici l'armée de Pharaon qui est venue à ton secours: « Voici que l'armée de Pharaon, qui est sortie pour te secourir, retournera en Égypte dans son pays.
8 Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’
Les Chaldéens reviendront et combattront cette ville. Ils la prendront et la brûleront par le feu. »''
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha!
« Yahvé dit: « Ne vous faites pas d'illusions en disant: « Les Chaldéens s'éloigneront de nous », car ils ne s'éloigneront pas.
10 Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”
Car si vous aviez frappé toute l'armée des Chaldéens qui vous combattent, et qu'il ne restât parmi eux que des blessés, chacun se lèverait dans sa tente et brûlerait cette ville par le feu.'"
11 Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,
Lorsque l'armée des Chaldéens se fut retirée de Jérusalem par crainte de l'armée de Pharaon,
12 Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko.
Jérémie sortit de Jérusalem pour aller au pays de Benjamin, afin d'y recevoir sa part, au milieu du peuple.
13 Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”
Lorsqu'il fut à la porte de Benjamin, il y avait là un chef de la garde, nommé Irija, fils de Shelemia, fils de Hanania, qui saisit Jérémie, le prophète, en disant: « Tu passes aux Chaldéens! »
14 Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa.
Jérémie dit alors: « C'est faux! Je ne fais pas défection aux Chaldéens. » Mais il ne l'écouta pas; alors Irija se saisit de Jérémie, et l'amena aux princes.
15 Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.
Les princes s'irritèrent contre Jérémie, le frappèrent et le mirent en prison dans la maison de Jonathan, le scribe, car ils avaient fait de cette maison une prison.
16 Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu.
Lorsque Jérémie fut entré dans le cachot et dans les cellules, et que Jérémie y fut resté plusieurs jours,
17 Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?” Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”
le roi Sédécias l'envoya chercher et le fit sortir. Le roi l'interrogea secrètement dans sa maison: « Y a-t-il une parole de Yahvé? » Jérémie a dit: « Il y en a un. » Il a aussi dit: « Vous serez livrés aux mains du roi de Babylone. »
18 Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani?
Jérémie dit au roi Sédécias: « En quoi ai-je péché contre toi, contre tes serviteurs ou contre ce peuple, pour que tu me mettes en prison?
19 Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’
Où sont maintenant tes prophètes qui t'ont prophétisé en disant: Le roi de Babylone ne viendra pas contre toi ni contre ce pays?
20 Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”
Écoute maintenant, mon seigneur le roi, et permets que ma supplique soit présentée devant toi, afin que tu ne me fasses pas retourner dans la maison de Jonathan, le scribe, de peur que je n'y meure. »
21 Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.
Alors le roi Sédécias donna ses ordres, et on enferma Jérémie dans la cour des gardes. On lui donna chaque jour une miche de pain de la rue des boulangers, jusqu'à ce qu'il n'y ait plus de pain dans la ville. Jérémie resta ainsi dans la cour des gardes.

< Yeremia 37 >