< Yeremia 23 >
1 “Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
Malheur aux bergers qui détruisent et dispersent les brebis de mon pâturage, dit l'Éternel.
2 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
C'est pourquoi Yahvé, le Dieu d'Israël, dit contre les bergers qui font paître mon peuple: « Vous avez dispersé mes brebis, vous les avez chassées, et vous ne les avez pas visitées. Voici, je vais faire retomber sur vous la méchanceté de vos actions, dit Yahvé.
3 “Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
Je rassemblerai le reste de mon troupeau de tous les pays où je l'ai chassé, je le ramènerai dans ses replis, et il sera fécond et multipliera.
4 Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
J'établirai sur eux des bergers qui les paîtront. Ils n'auront plus peur, ils ne seront plus effrayés, ils ne manqueront de rien, dit Yahvé.
5 Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
« Voici, les jours viennent, dit Yahvé, « que je susciterai à David un rameau de justice; et il régnera en tant que roi et fera preuve de sagesse, et fera régner la justice et la droiture dans le pays.
6 Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
En ses jours, Juda sera sauvé, et Israël habitera en sécurité. C'est le nom par lequel il sera appelé: Yahvé notre justice.
7 “Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
« C'est pourquoi voici que les jours viennent, dit Yahvé, où l'on ne dira plus: « Yahvé est vivant, lui qui a fait monter les enfants d'Israël du pays d'Égypte »,
8 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
mais: « Yahvé est vivant, lui qui a fait monter et qui a conduit les rejetons de la maison d'Israël du pays du Nord et de tous les pays où je les avais chassés ». Alors ils habiteront dans leur pays. »
9 Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
Concernant les prophètes: Mon cœur en moi est brisé. Tous mes os tremblent. Je suis comme un homme ivre, et comme un homme que le vin a vaincu, à cause de Yahvé, et à cause de ses paroles saintes.
10 Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
« Car le pays est rempli d'adultères; car à cause de la malédiction, le pays est en deuil. Les pâturages du désert se sont asséchés. Leur parcours est mauvais, et leur pouvoir n'est pas juste;
11 “Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
car le prophète et le prêtre sont tous deux profanes. Oui, dans ma maison, j'ai trouvé leur méchanceté, dit Yahvé.
12 “Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
C'est pourquoi leur chemin sera pour eux comme des lieux glissants dans les ténèbres. Ils seront conduits sur, et y tomber; car je vais faire venir le malheur sur eux, même l'année de leur visite, dit Yahvé.
13 “Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
« J'ai vu la folie des prophètes de Samarie. Ils ont prophétisé par Baal, et fait errer mon peuple Israël.
14 Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
Dans les prophètes de Jérusalem, j'ai aussi vu une chose horrible: ils commettent des adultères et marchent dans le mensonge. Ils renforcent les mains des malfaiteurs, afin que personne ne revienne de sa méchanceté. Ils sont tous devenus pour moi comme Sodome, et ses habitants comme Gomorrhe. »
15 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
C'est pourquoi Yahvé des Armées dit à propos des prophètes: « Voici, je vais les nourrir d'absinthe, et leur faire boire de l'eau empoisonnée; car les prophètes de Jérusalem ont répandu l'impiété dans tout le pays. »
16 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
Yahvé des Armées dit, « N'écoutez pas les paroles des prophètes qui vous prophétisent. Ils vous apprennent la vanité. Ils parlent d'une vision de leur propre cœur, et non de la bouche de Yahvé.
17 Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
Ils disent continuellement à ceux qui me méprisent, Yahvé a dit: « Vous aurez la paix ». et à tous ceux qui marchent dans l'obstination de leur propre cœur, ils disent, « Aucun malheur ne viendra sur vous.
18 Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
Car qui s'est tenu dans le conseil de Yahvé, pour qu'il perçoive et entende sa parole? Qui a écouté ma parole, et l'a entendue?
19 Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
Voici que l'orage de Yahvé, sa colère, a éclaté. Oui, une tempête tourbillonnante! Elle éclatera sur la tête des méchants.
20 Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
La colère de Yahvé ne reviendra pas avant qu'il ait exécuté et a réalisé les intentions de son cœur. Dans les derniers jours, vous le comprendrez parfaitement.
21 Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
Je n'ai pas envoyé ces prophètes, et pourtant ils ont couru. Je ne leur ai pas parlé, mais ils ont prophétisé.
22 Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
Mais s'ils s'étaient tenus dans mon conseil, alors ils auraient fait en sorte que mon peuple entende mes paroles, et les aurait détournés de leur mauvaise voie, et de la méchanceté de leurs actes.
23 “Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
« Je suis un Dieu à portée de main », dit Yahvé, « et non un Dieu lointain?
24 Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
Quelqu'un peut-il se cacher dans des lieux secrets pour que je ne puisse pas le voir? » dit Yahvé. « Ne remplis-je pas le ciel et la terre? » dit Yahvé.
25 “Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
« J'ai entendu ce qu'ont dit les prophètes, qui prophétisent des mensonges en mon nom, disant: 'J'ai eu un rêve! J'ai eu un songe!
26 Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
Jusqu'à quand cela sera-t-il dans le cœur des prophètes qui prophétisent le mensonge, même les prophètes de la tromperie de leur propre cœur?
27 Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
Ils ont l'intention de faire oublier mon nom à mon peuple par les rêves qu'ils racontent chacun à son prochain, comme leurs pères ont oublié mon nom à cause de Baal.
28 Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
Que le prophète qui a un rêve raconte un rêve, et que celui qui a ma parole dise fidèlement ma parole. Qu'est-ce que la paille pour le blé? dit Yahvé.
29 “Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
« Ma parole n'est-elle pas comme un feu, dit Yahvé, et comme un marteau qui brise le rocher?
30 “Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
C'est pourquoi voici, j'en veux aux prophètes, dit l'Éternel, qui volent chacun mes paroles à leur prochain.
31 “Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
Voici, j'en veux aux prophètes, dit l'Éternel, qui se servent de leur langue et disent: « Il dit ».
32 Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
Voici, j'en veux à ceux qui prophétisent des songes mensongers, dit Yahvé, qui les racontent et égarent mon peuple par leurs mensonges et par leur vaine vantardise; pourtant je ne les ai ni envoyés ni commandés. Ils ne profitent pas du tout à ce peuple », dit Yahvé.
33 “Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
« Lorsque ce peuple, ou le prophète, ou un prêtre, t'interrogera en disant: « Quel est le message de Yahvé? Tu leur répondras: « Quel message? Je vous rejetterai, dit Yahvé ».
34 Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
Quant au prophète, au prêtre et au peuple qui diront: « Le message de Yahvé », je punirai même cet homme et sa famille.
35 Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
Vous direz chacun à son voisin, chacun à son frère: « Qu'est-ce que l'Éternel a répondu? » et « Qu'est-ce que l'Éternel a dit? »
36 Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
Vous ne parlerez plus du message de l'Éternel, car la parole de chacun est devenue son message, car vous avez perverti les paroles du Dieu vivant, de l'Éternel des armées, notre Dieu.
37 Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
Vous direz au prophète: « Que t'a répondu Yahvé? » et « Qu'a dit Yahvé?
38 Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
Si vous dites: « Le message de l'Éternel », l'Éternel dit: « Parce que vous dites cette parole: « Le message de l'Éternel », et que je vous ai envoyé dire de ne pas dire: « Le message de l'Éternel »,
39 Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
voici, je vous oublierai, et je vous rejetterai avec la ville que j'ai donnée à vous et à vos pères, loin de ma présence.
40 Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”
Je mettrai sur toi un opprobre éternel et une honte perpétuelle, qui ne s'oubliera pas.'"