< Yeremia 16 >

1 Kisha neno la Bwana likanijia:
I stało się słowo Pańskie do mnie, mówiąc:
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
Nie pojmuj sobie żony, ani miej synów ani córek na tem miejscu.
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
Albowiem tak mówi Pan o synach i o córkach spłodzonych na tem miejscu, i o matkach ich, które ich zrodziły, i o ojcach ich, którzy ich spłodzili w tej ziemi:
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
Śmierciami ciężkiemi pomrą; nie będą ich płakać, ani ich pochowają, ale miasto gnoju na wierzchu ziemi będą; a mieczem i głodem wytraceni będą; i będą trupy ich pokarmem ptastwu niebieskiemu i i zwierzowi ziemskiemu.
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
Bo tak mówi Pan: Nie wchodź do domu żałoby, ani chodź na płacz, ani ich żałuj; bom odjął pokój mój od ludu tego, miłosierdzie i litość, mówi Pan.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
Gdy pomrą wielcy i mali w tej ziemi, nie będą pogrzebieni, ani ich płakać będą; i nie będą się rzezać, ani sobie łysiny czynić dla nich;
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
Ani im dadzą jeść, aby ich w smutku cieszyli nad umarłym; ani im dadzą pić z kubka pocieszenia po ojcu ich i po matce ich;
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
Także do domu uczty nie wchodź, abyś zasiadał z nimi, i jadł, i pił.
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
Albowiem tak mówi Pan zastępów, Bóg Izraelski: Oto Ja sprawię, iż ustanie na tem miejscu przed oczyma waszemi, i za dni waszych głos wesela, i głos radości, głos oblubieńca, i głos oblubienicy.
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
A gdy opowiesz ludowi temu wszystkie te słowa, a rzekliby do ciebie: Przecz Pan wyrzekł przeciwko nam to wszystko wielkie złe? I cóż jest za nieprawość nasza, i co za grzech nasz, którymeśmy zgrzeszyli przeciwko Panu, Bogu naszemu?
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
Tedy rzeczesz do nich: Przeto, iż mię opuścili ojcowie wasi, (mówi Pan) a chodzili za bogami cudzymi, i służyli im, i kłaniali się im, lecz mnie opuścili, i zakonu mego nie przestrzegali.
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
A wy dalekoście gorzej czynili, niż ojcowie wasi; albowiem oto każdy chodzi za uporem złego serca swego, nie słuchając mię;
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
Dlatego wyrzucę was z tej ziemi do ziemi, którejście nie znali, wy i ojcowie wasi, a tam służyć będziecie bogom cudzym we dnie i w nocy, dokąd wam nie okażę miłosierdzia.
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
Przetoż oto dni idą, mówi Pan, że nie rzeką więcej: Jako żyje Pan, który wywiódł synów Izraelskich z ziemi Egipskiej.
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
Ale: Jako żyje Pan, który wywiódł synów Izraelskich z ziemi północnej, i ze wszystkich ziem, do których ich był wygnał, gdy ich zasię przywiodę do ziemi ich, którąm dał ojcom ich.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
Oto Ja poślę do wielu rybitwów, (mówi Pan) aby ich łowili; potem poślę do wielu łowców, aby ich łapali na wszelkiej górze i na wszelkim pagórku, i w dziurach skalnych.
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
Oczy moje patrzą na wszystkie drogi ich; nie są utajone przed obliczem mojem, ani jest zakryta nieprawość ich przed oczyma mojemi.
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
I oddam im pierwej w dwójnasób za nieprawości ich, i za grzechy ich, przeto, że ziemię moję splugawili trupami obrzydliwości swojej, i sprosnościami swemi napełnili dziedzictwo moje.
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
Panie, mocy moja i siło moja, i ucieczko moja w dzień utrapienia! do ciebie przyjdą narody od kończyn ziemi, i rzekną: Zaiste się fałszu trzymali ojcowie nasi, i marności, w których żadnego pożytku nie było.
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
Izali sobie człowiek uczynić może bogów? ponieważ sami nie są bogami.
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
Dlatego oto Ja sprawię, aby poznali tym razem; sprawię, mówię, aby poznali rękę moję i moc moję, i dowiedzieli się, że imię moje jest Pan.

< Yeremia 16 >