< Yeremia 16 >

1 Kisha neno la Bwana likanijia:
Yahweh gave me another message. [He said to me],
2 “Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
“Do not get married and have children in this land,
3 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
because this is what [I], Yahweh, say about the children who are born in this city, and about their mothers and fathers:
4 “Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
[Many of] them will die from terrible diseases. And no one will mourn for them. No one will even bury their corpses; the corpses will lie on the ground, [scattered] like manure. [Others] will die in wars or from hunger, and [then] their corpses will become food for vultures and wild animals.”
5 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
This is [also] what Yahweh said to me: “Do not go to funerals to mourn or to show [those whose relatives have died] that you feel sorry for them, because I have stopped protecting them, and I have caused that things will not go well for them. I have stopped faithfully loving them and acting mercifully toward them.
6 “Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
[Very many people] will die in this land, [including] those who are important and those who are not important. And no one will mourn for them, or [even] bury [their corpses]. No one will cut himself or shave his head [to show that he is very sad].
7 Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
No one will bring food to comfort those who are mourning, not even if it is their father or their mother [who has died]. No one will give them a cup [of wine] to cheer them up.
8 “Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
And do not go into the houses where people are feasting. Do not eat or drink anything with them.
9 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
[I want you to do this] because this is what [I], the Commander of the armies of angels, say: ‘While you are still alive and seeing it happen, I will cause there to be no more singing and laughing in this land. There will be no more joyful voices of bridegrooms and brides.’
10 “Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
When you tell these things to the people, they will ask, ‘Why has Yahweh declared that these terrible things will happen to us? What have we done [for which we deserve to be punished like this]? What sin have we committed against Yahweh our God?’
11 Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
Then this is what you must tell them [that I am replying to them]: ‘It is because your ancestors turned away from me, Yahweh. They worshiped other gods and served them. They abandoned me and did not obey my commands.
12 ‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
But you [who are living now] have done more wicked things than your ancestors did! Each of you stubbornly does the evil things that he desires and refuses to pay attention to what I say.
13 Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
So, I will throw you out of this land, and I will send you to a land that you and your ancestors have never known about. There you will worship other gods day and night. And I will not act mercifully toward you.’
14 “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
But there will be a time when people [who are solemnly promising to do something] will no longer say, ‘[I will do this], [just as surely] as Yahweh lives—the one who brought the Israeli people here from Egypt.’
15 bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
Instead, they will say ‘[I will do this, just as surely] as Yahweh lives—the one who brought [us] Israeli people back to our own land, from the lands to the north and from all the other lands to which he had (exiled us/forced us to go).’ [They will be able to say that] because [some day] I will bring your descendants back to this land that I gave to your ancestors.
16 “Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
But now I am summoning [your enemies who will seize the people of Judah like] [MET] fishermen [catch fish]. I am summoning those who will search for them on every mountain and hill, and in every cave, [like] [MET] hunters [search for animals to kill].
17 Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
I am watching them carefully. I see every sin [that they commit]. They will not [be able to] hide from me [MTY].
18 Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
Because of all the wicked things that they have done [DOU], I will punish them twice as much [as I would punish other people. I will do that] because they have caused my land to become unacceptable to me because of their [worshiping] lifeless statues of detestable gods, and [also because they] have done many other evil things throughout my land.”
19 Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
[Then I prayed, saying], “Yahweh, you are the one who strengthens me and protects me [MET]; you are the one to whom I go when I have [troubles]. [Some day people from] nations all over the world will come to you and say, ‘Our ancestors left/gave us only something that was false; [they worshiped idols] that are completely worthless [DOU].
20 Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
No one can [RHQ] make their own gods; the gods that they make are [only idols]; they are not real gods.’”
21 “Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.
[Then Yahweh said], “Now I will show my power to [the people of Judah]; I will show them that I am truly very powerful [DOU]. Then, finally, they will know that I, Yahweh, [am the true God].”

< Yeremia 16 >