< Yeremia 11 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word which it came to Jeremiah from with Yahweh saying.
2 “Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu.
Hear [the] words of the covenant this and you will speak them to everyone of Judah and to [the] inhabitants of Jerusalem.
3 Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili,
And you will say to them thus he says Yahweh [the] God of Israel [is] cursed the person who not he will hear [the] words of the covenant this.
4 maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
Which I commanded ancestors your on [the] day brought out I them from [the] land of Egypt from [the] furnace of iron saying listen to voice my and you will do them according to all that I will command you and you will become for me a people and I I will become for you God.
5 Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.” Nikajibu, “Amen, Bwana.”
So as to carry out the oath which I swore to ancestors your to give to them a land flowing of milk and honey like the day this and I answered and I said amen - O Yahweh.
6 Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata.
And he said Yahweh to me proclaim all the words these in [the] cities of Judah and in [the] streets of Jerusalem saying hear [the] words of the covenant this and you will do them.
7 Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”
For certainly I warned ancestors your on [the] day brought up I them from [the] land of Egypt and until the day this rising early and warning saying listen to voice my.
8 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’”
And not they listened and not they inclined ear their and they walked everyone in [the] stubbornness of own heart their evil and I brought on them all [the] words of the covenant this which I commanded to do and not they did.
9 Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu.
And he said Yahweh to me it has been found a conspiracy among everyone of Judah and among [the] inhabitants of Jerusalem.
10 Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao.
They have returned to [the] iniquities of ancestors their former who they refused to hear words my and they they have walked after gods other to serve them they have broken [the] house of Israel and [the] house of Judah covenant my which I made with ancestors their.
11 Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza.
Therefore thus he says Yahweh here I [am] about to bring to them a calamity which not they will be able to go out from it and they will cry out to me and not I will listen to them.
12 Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.
And they will go [the] cities of Judah and [the] inhabitants of Jerusalem and they will cry out to the gods which they [are] making smoke to them and certainly not they will deliver them at [the] time of calamity their.
13 Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’
For [the] number of cities your they are gods your O Judah and [the] number of [the] streets of Jerusalem you have made altars to the shameful thing altars to make smoke to Baal.
14 “Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.
And you may not you pray for the people this and may not you lift up for them a cry of entreaty and a prayer for not I [will be] listening at [the] time call out they to me for calamity their.
15 “Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu, anapofanya mashauri yake maovu na wengi? Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza kuondolea mbali adhabu yako? Unapojiingiza katika ubaya wako, ndipo unashangilia.”
What? to beloved [one] my in house my doing it plan the many [people] and flesh of holiness they will pass away from on you for wickedness your then you will rejoice.
16 Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi ulio na matunda mazuri kwa sura. Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu atautia moto, nayo matawi yake yatavunjika.
An olive tree luxuriant beautiful of fruit of form he called Yahweh name your to [the] sound of - a rainstorm great he has kindled a fire on it and they are bad branches its.
17 Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.
And Yahweh of hosts who planted you he has spoken on you evil on account of [the] evil of [the] house of Israel and [the] house of Judah which they have done for themselves to provoke to anger me by making smoke to Baal.
18 Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.
And Yahweh he made known to me and I knew! then you showed me deeds their.
19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema, “Sisi na tuuangamize mti na matunda yake; nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.”
And I [had been] like a lamb a tame one [which] it is led to slaughter and not I knew that on me - they had planned plans let us destroy [the] tree with bread its and let us cut off him from [the] land of [the] living and name his not may it be remembered again.
20 Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki, nawe uchunguzaye moyo na akili, wacha nione ukiwalipiza wao kisasi, kwa maana kwako nimeweka shauri langu.
And O Yahweh of hosts [who] judges righteousness [who] tests kidneys and heart let me see vengeance your from them for to you I have made known case my.
21 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’:
Therefore thus he says Yahweh on [the] people of Anathoth who are seeking life your saying not you must prophesy in [the] name of Yahweh and not you will die by hand our.
22 kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.
Therefore thus he says Yahweh of hosts here I [am] about to visit [judgment] on them the young men they will die by the sword sons their and daughters their they will die by famine.
23 Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’”
And a remnant not it will belong to them for I will bring calamity to [the] people of Anathoth [the] year of punishment their.

< Yeremia 11 >