< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Thus he says Yahweh the heavens [are] throne my and the earth [is] [the] footstool of feet my where? this [is the] house which you will build for me and where? this [is the] place rest my.
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
And all these [things] hand my it made and they were all these [things] [the] utterance of Yahweh and to this one I will look to an afflicted [person] and a [person] stricken of spirit and a [person] trembling on word my.
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
[one who] slaughters Ox [one who] strikes down a person [one who] sacrifices lamb [one who] breaks [the] neck of a dog [one who] offers up a grain offering [the] blood of a pig [one who] offers as a memorial frankincense [one who] blesses wickedness also they they have chosen own ways their and detestable things their self their it has delighted.
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
Also I I will choose punishments their and fears their I will bring to them because I called and there not [was one who] answered I spoke and not they listened and they did the evil in view my and [that] which not I desired they chose.
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
Hear [the] word of Yahweh O [people] trembling to word his they have said relatives your [who] hate you [who] exclude you for [the] sake of name my will be honored Yahweh so we may look on joy your and they they will be ashamed.
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
A sound of an uproar from [the] city a sound from [the] temple [the] sound of Yahweh repaying recompense to enemies his.
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
Before she was in labor she gave birth before it came labor-pain[s] to her and she delivered a male.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Who? has he heard like this who? has he seen like these ¿ will it be brought forth a land in a day one or? will it be born a nation a time one for she was in labor also she gave birth to Zion children her.
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
¿ I do I bring to [the] birth and not I cause to bring forth he says Yahweh or? [am] I the [one who] causes to bring forth and do I restrain? he says God your.
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
Rejoice with Jerusalem and be glad in it O all [those who] love it exult with it exultation O all those [who] mourn on it.
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
So that you may suck and you will be satisfied from [the] breast of consolations its so that you may suck and you will take delight from [the] nipple of abundance its.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
For thus - he says Yahweh here I [am] about to extend to it like a river peace and like a torrent overflowing [the] abundance of nations and you will suck on a hip you will be carried and on knees you will be fondled.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
Like a person whom mother his she comforts him so I I will comfort you and in Jerusalem you will be comforted.
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
And you will see and it will exult heart your and bones your like grass they will sprout and it will be made known [the] hand of Yahweh with servants his and he will be indignant enemies his.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
For there! Yahweh in fire he will come and [will be] like the storm-wind chariots his to bring back with rage anger his and rebuke his with flames of fire.
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
For by fire Yahweh [will] enter into judgment and by sword his with all flesh and they will be many [those] slain of Yahweh.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
Who consecrate themselves and who purify themselves to the gardens after (one *Q(K)*) in the middle [those who] eat [the] flesh of the pig and the detestable thing and the mouse all together they will come to an end [the] utterance of Yahweh.
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
And I deeds their and thoughts their [is] coming to gather all the nations and the languages and they will come and they will see glory my.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
And I will perform among them a sign and I will send of them - survivors to the nations Tarshish Pul and Lud [those who] draw a bow Tubal and Javan the islands distant which not they have heard report my and not they have seen glory my and they will declare glory my among the nations.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
And they will bring back all relatives your from all the nations - an offering - to Yahweh on horses and in chariot[s] and in wagons and on mules and on camels to [the] mountain of holiness my Jerusalem he says Yahweh just as they will bring [the] people of Israel the grain offering in a vessel pure [the] house of Yahweh.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
And also some of them I will take to priests to Levites he says Yahweh.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
For just as the heavens new and the earth new which I [am] about to make [will] endure before me [the] utterance of Yahweh so it will endure offspring your and name your.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
And it will be as often as a new moon in new moon its and as often as a sabbath in sabbath its it will come all flesh to bow down before me he says Yahweh.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
And they will go out and they will look on [the] corpses of the people who rebelled against me for worm their not it will die and fire their not it will be extinguished and they will be an abhorrence to all flesh.

< Isaya 66 >