< Isaya 65 >
1 “Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakuniulizia. Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Kwa taifa lile ambalo halikuliita Jina langu, nilisema, ‘Niko hapa, niko hapa.’
« Je suis interrogé par ceux qui n'ont pas demandé. Je suis trouvé par ceux qui ne m'ont pas cherché. J'ai dit: « Voyez-moi, voyez-moi », à une nation qui n'était pas appelée par mon nom.
2 Mchana kutwa nimeinyoosha mikono yangu kwa watu wakaidi, wanaokwenda katika njia ambazo si nzuri, wafuatao mawazo yao wenyewe:
J'ai étendu mes mains tout le jour vers un peuple rebelle, qui marchent d'une manière qui n'est pas bonne, selon leurs propres pensées;
3 taifa ambalo daima hunikasirisha machoni pangu, wakitoa dhabihu katika bustani na kufukiza uvumba juu ya madhabahu za matofali;
un peuple qui me provoque continuellement en face, les sacrifices dans les jardins, et de brûler de l'encens sur des briques;
4 watu waketio katikati ya makaburi na kukesha mahali pa siri, walao nyama za nguruwe, nazo sufuria zao zina mchuzi wa nyama zilizo najisi,
qui sont assis parmi les tombes, et passer des nuits dans des endroits secrets; qui mangent de la viande de porc, et un bouillon de choses abominables est dans leurs vases;
5 wasemao, ‘Kaa mbali; usinikaribie, kwa maana mimi ni mtakatifu mno kwako!’ Watu wa aina hiyo ni moshi katika pua zangu, ni moto uwakao mchana kutwa.
qui disent: « Reste seul, ne vous approchez pas de moi, car je suis plus saint que vous. C'est de la fumée dans mon nez, un feu qui brûle toute la journée.
6 “Tazama, jambo hili hubakia limeandikwa mbele zangu: sitanyamaza, bali nitalipiza kwa ukamilifu; nitalipiza mapajani mwao:
« Voici, c'est écrit devant moi: Je ne garderai pas le silence, mais il remboursera, oui, je rembourserai dans leur sein
7 dhambi zenu na dhambi za baba zenu,” asema Bwana. “Kwa sababu walitoa dhabihu za kuteketezwa juu ya milima na kunichokoza mimi juu ya vilima, nitawapimia mapajani mwao malipo makamilifu kwa matendo yao ya zamani.”
tes propres iniquités et les iniquités de tes pères ensemble », dit Yahvé, « qui ont brûlé de l'encens sur les montagnes, et m'ont blasphémé sur les collines. C'est pourquoi je mesurerai d'abord leur travail dans leur sein. »
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile divai mpya ingali bado inapatikana katika kishada cha zabibu, nao watu husema, ‘Usikiharibu, kwa kuwa bado kuna kitu kizuri ndani yake,’ hivyo ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.
Yahvé dit, « Comme le vin nouveau se trouve dans la grappe, et l'un d'eux dit: « Ne le détruis pas, car il contient une bénédiction ». ainsi je ferai pour l'amour de mes serviteurs, pour que je ne les détruise pas tous.
9 Nitawaleta wazao kutoka kwa Yakobo, na kutoka kwa Yuda wale watakaomiliki milima yangu, nao watu wangu wateule watairithi, nako huko wataishi watumishi wangu.
Je ferai sortir une descendance de Jacob, et de Juda un héritier de mes montagnes. Mes élus en hériteront, et mes serviteurs y habiteront.
10 Sharoni itakuwa malisho kwa ajili ya makundi ya kondoo, na Bonde la Akori mahali pa kupumzikia kwa makundi ya ngʼombe, kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.
Sharon sera un berceau de troupeaux, et la vallée d'Acor, un endroit où les troupeaux peuvent se coucher, pour mon peuple qui m'a cherché.
11 “Bali kwenu ninyi mnaomwacha Bwana na kuusahau mlima wangu mtakatifu, ninyi mnaoandaa meza kwa ajili ya Bahati, na kujaza mabakuli ya mvinyo uliochanganywa kwa ajili ya Ajali,
« Mais vous, qui abandonnez Yahvé, qui oublient ma montagne sainte, qui préparent une table pour la Fortune, et qui remplissent de vin mélangé jusqu'au Destin;
12 nitawaagiza mfe kwa upanga, nanyi nyote mtainama chini ili kuchinjwa; kwa kuwa niliwaita lakini hamkuitika, nilisema lakini hamkusikiliza. Mlitenda maovu machoni pangu, nanyi mkachagua mambo yale yanayonichukiza.”
Je vous destine à l'épée, et vous vous prosternerez tous devant l'abattoir; parce que quand j'ai appelé, tu n'as pas répondu. Quand j'ai parlé, tu n'as pas écouté; mais tu as fait ce qui était mal à mes yeux, et choisi ce qui ne me plaisait pas. »
13 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtaona njaa; watumishi wangu watakunywa lakini ninyi mtaona kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mtaona haya.
C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit, « Voici que mes serviteurs vont manger, mais vous aurez faim; voici, mes serviteurs vont boire, mais vous aurez soif. Voici que mes serviteurs vont se réjouir, mais vous serez déçu.
14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ya mioyo yao, lakini ninyi mtalia kutokana na uchungu wa moyoni, na kupiga yowe kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.
Voici, mes serviteurs chanteront de joie de cœur, mais vous pleurerez de chagrin d'amour, et gémiront pour l'angoisse de l'esprit.
15 Mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa watu wangu waliochaguliwa; Bwana Mwenyezi atawaua ninyi, lakini watumishi wake atawapa jina jingine.
Tu laisseras ton nom comme une malédiction pour mes élus, et le Seigneur Yahvé te tuera. Il appellera ses serviteurs par un autre nom,
16 Yeye aombaye baraka katika nchi atafanya hivyo kwa Mungu wa kweli; yeye aapaye katika nchi ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za zamani zitasahaulika na kufichwa kutoka machoni pangu.
afin que celui qui se bénit dans la terre se bénisse dans le Dieu de vérité; et celui qui jure sur la terre jurera par le Dieu de la vérité; parce que les anciens problèmes sont oubliés, et parce qu'ils sont cachés à mes yeux.
17 “Tazama, nitaumba mbingu mpya na dunia mpya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa, wala hayatakuja akilini.
« Car voici, je crée de nouveaux cieux et une nouvelle terre; et on ne se souviendra plus des choses passées, ni ne viennent à l'esprit.
18 Lakini furahini na kushangilia daima katika hivi nitakavyoumba, kwa kuwa nitaumba Yerusalemu uwe wa kupendeza, nao watu wake wawe furaha.
Mais soyez heureux et réjouissez-vous à jamais de ce que j'ai créé; car voici, je crée Jérusalem pour qu'elle soit un délice, et son peuple une joie.
19 Nami nitaifurahia Yerusalemu na kuwafurahia watu wangu; sauti ya maombolezo na ya kilio haitasikika humo tena.
Je me réjouirai à Jérusalem, et je me réjouis de mon peuple; et la voix des pleurs et la voix des cris ne sera plus entendu en elle.
20 “Kamwe hatakuwepo tena ndani yake mtoto mchanga atakayeishi siku chache tu, au mzee ambaye hataishi akatimiza miaka yake. Yeye atakayekufa akiwa na umri wa miaka mia moja atahesabiwa kwamba ni kijana tu, yeye ambaye hatafika miaka mia moja, atahesabiwa kuwa amelaaniwa.
« Il n'y aura plus de nourrisson qui ne vit que quelques jours, ni un vieil homme qui n'a pas rempli ses jours; car l'enfant mourra à cent ans, et le pécheur âgé de cent ans sera maudit.
21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake; watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
Ils construiront des maisons et les habiteront. Ils planteront des vignes et mangeront leurs fruits.
22 Hawatajenga nyumba, nao watu wengine waishi ndani yake, au kupanda mazao na wengine wale. Kwa kuwa kama zilivyo siku za mti, ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, wateule wangu watafurahia kwa siku nyingi kazi za mikono yao.
Ils ne construiront pas et un autre habitera. Ils ne vont pas planter et un autre manger; car les jours de mon peuple seront comme les jours d'un arbre, et mes élus jouiront longtemps du travail de leurs mains.
23 Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa watoto ili wapatwe na majanga, kwa kuwa watakuwa taifa lililobarikiwa na Bwana, wao na wazao wao pamoja nao.
Ils ne travailleront pas en vain ni donner naissance à une calamité; car ils sont la descendance des bénis de Yahvé et leurs descendants avec eux.
24 Kabla hawajaita, nitajibu, nao wakiwa katika kunena, nitasikia.
Il arrivera qu'avant qu'ils n'appellent, je répondrai; et pendant qu'ils parlent encore, j'entendrai.
25 Mbwa mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, naye simba atakula nyasi kama maksai, lakini mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote,” asema Bwana.
Le loup et l'agneau paîtront ensemble. Le lion mangera de la paille comme le bœuf. La poussière sera la nourriture du serpent. Ils ne feront ni mal ni destruction sur toute ma montagne sainte ». dit Yahvé.