< Isaya 5 >
1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
Permettez-moi de chanter pour mon bien-aimé un chant de mon bien-aimé sur sa vigne. Mon bien-aimé avait un vignoble sur une colline très fructueuse.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
Il l'a déterrée, a rassemblé ses pierres, l'a planté de la vigne la plus précieuse, a construit une tour en son milieu, et j'y ai aussi découpé un pressoir à vin. Il a cherché à ce qu'elle produise des raisins, mais elle a donné des raisins sauvages.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
« Maintenant, habitants de Jérusalem et hommes de Juda, s'il te plaît, juge entre moi et ma vigne.
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
Que pouvait-on faire de plus à ma vigne, que je n'ai fait en elle? Pourquoi, alors que j'attendais qu'il produise des raisins, a-t-il produit des raisins sauvages?
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
Maintenant, je vais vous dire ce que je vais faire à ma vigne. J'enlèverai sa haie, et elle sera dévorée. J'abattrai son mur, et il sera piétiné.
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
Je la réduirai en désert. Il ne sera ni taillé ni biné, mais il poussera des ronces et des épines. J'ordonnerai aussi aux nuages de ne pas faire pleuvoir sur elle. »
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
Car la vigne de l'Éternel des armées, c'est la maison d'Israël, et les hommes de Juda sa plante agréable. Il a cherché la justice, mais voici l'oppression, pour la justice, mais voici un cri de détresse.
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Malheur à ceux qui joignent une maison à une autre, qui s'étendent de champ en champ, jusqu'à ce qu'il n'y ait plus de place, et on te fait habiter seul au milieu du pays!
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
A mes oreilles, Yahvé des armées dit: « Certainement, beaucoup de maisons seront désolées, même grande et belle, inoccupée.
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
Car dix arpents de vigne donneront un bath, et un homer de semence donnera un épha. »
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Malheur à ceux qui se lèvent tôt le matin, pour suivre des boissons fortes, qui restent tard dans la nuit, jusqu'à ce que le vin les enflamme!
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
La harpe, la lyre, le tambourin et la flûte, avec le vin, sont à leurs fêtes; mais ils ne respectent pas l'œuvre de Yahvé, Ils n'ont pas non plus considéré l'opération de ses mains.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
C'est pourquoi mon peuple va en captivité par manque de connaissance. Leurs hommes honorables sont affamés, et leurs multitudes sont assoiffées.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
C'est pourquoi le séjour des morts a élargi son désir, et a ouvert sa bouche sans mesure; et leur gloire, leur multitude, leur faste, et celui qui se réjouit parmi eux, y descendent. (Sheol )
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
Ainsi l'homme est abaissé, l'humanité est humiliée, et les yeux des arrogants sont humiliés;
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
mais le Yahvé des armées est élevé dans la justice, et Dieu le Saint est sanctifié dans la justice.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
Alors les agneaux paîtront comme dans leur pâturage, et les étrangers mangeront les ruines des riches.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Malheur à ceux qui tirent l'iniquité avec des cordes de mensonge, et la méchanceté comme avec une corde de charrette,
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
qui disent: « Qu'il se hâte, qu'il hâte son œuvre, afin que nous la voyions; que le conseil du Saint d'Israël s'approche et vienne, pour que nous le sachions! »
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Malheur à ceux qui appellent le mal bien, et le bien mal; qui a mis l'obscurité pour la lumière, et la lumière pour les ténèbres; qui ont mis de l'amer pour du sucré, et le doux pour l'amer!
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Malheur à ceux qui sont sages à leurs propres yeux, et prudents à leurs propres yeux!
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Malheur à ceux qui ont la force de boire du vin, et des champions de la préparation de boissons fortes;
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
qui acquittent les coupables contre un pot-de-vin, mais refuser la justice pour les innocents!
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
C'est pourquoi, comme la langue de feu dévore le chaume, et comme l'herbe sèche s'enfonce dans la flamme, et leur racine sera comme de la pourriture, et leur fleur s'envolera en poussière, parce qu'ils ont rejeté la loi de Yahvé des Armées, et ont méprisé la parole du Saint d'Israël.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
C'est pourquoi la colère de Yahvé s'enflamme contre son peuple, il a étendu sa main contre eux et les a frappés. Les montagnes tremblent, et leurs cadavres sont comme des déchets au milieu des rues. Pour autant, sa colère ne s'éteint pas, mais sa main est toujours tendue.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
Il élèvera une bannière pour les nations lointaines, et il les sifflera jusqu'au bout de la terre. Voici, ils viendront rapidement et promptement.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
Personne ne se lassera ni ne trébuchera parmi eux; personne ne sommeillera ni ne dormira, et la ceinture de leur taille ne sera pas détachée, ni la courroie de leurs sandales ne sera brisée,
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
dont les flèches sont acérées, et tous leurs arcs pliés. Les sabots de leurs chevaux seront comme du silex, et leurs roues comme un tourbillon.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
Leur rugissement sera comme celui d'une lionne. Ils rugiront comme de jeunes lions. Oui, ils rugiront, et saisissent leur proie et l'emportent, et il n'y aura personne pour le faire.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
En ce jour-là, ils rugiront contre eux comme le grondement de la mer. Si l'on regarde la terre, voici l'obscurité et la détresse. La lumière est obscurcie dans ses nuages.