< Isaya 49 >

1 Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
Listen O islands to me and pay attention O peoples from a distance Yahweh from [the] womb he called me from [the] inward parts of mother my he has brought to remembrance name my.
2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
And he made mouth my like a sword sharp in [the] shadow of hand his he hid me and he made me an arrow polished in quiver his he concealed me.
3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
And he said to me [are] servant my you Israel whom by you I will get glory for myself.
4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
And I I said to emptiness I have labored to nothingness and futility strength my I have caused to fail nevertheless justice my [is] with Yahweh and recompense my [is] with God my.
5 Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
And now - he says Yahweh [who] formed me from [the] womb a servant of him to bring back Jacob to him and Israel (to him *Q(K)*) it will be gathered and I may be honored in [the] eyes of Yahweh and God my he has been strength my.
6 yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
And he said it is [too] trifling for being you of me servant to raise up [the] tribes of Jacob (and [the] preserved [ones] of *Q(K)*) Israel to bring back and I will make you a light of [the] nations to be salvation my to [the] end of the earth.
7 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
Thus he says Yahweh [the] redeemer of Israel holy [one] its to despise life to [one who] abhors a nation to a servant of rulers kings they will see and they will stand up princes so they may bow down on account of Yahweh who [is] faithful [the] holy [one] of Israel and he has chosen you.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
Thus - he says Yahweh in a time of favor I will answer you and on a day of salvation I will help you and I will watch over you and I will make you a covenant of [the] people to raise up [the] land to give as inheritance inheritances desolate.
9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
To say to [the] prisoners come out to [those] who [are] in darkness reveal yourselves on roads they will graze and [will be] on all bare heights pasture their.
10 Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
Not they will be hungry and not they will be thirsty and not it will strike them burning heat and sun for [one who] has compassion on them he will guide them and to springs of water he will lead them.
11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
And I will make all mountains my into road and highways my they will be lifted up!
12 Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
Here! these from a distance they will come and here! these from [the] north and from [the] west and these from [the] land of Sinim.
13 Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
Shout for joy O heaven and be glad O earth (and break forth *Q(K)*) O mountains a shout of joy for he has comforted Yahweh people his and afflicted [people] his he has compassion on.
14 Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
And it said Zion he has forsaken me Yahweh and [the] Lord he has forgotten me.
15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
¿ Will she forget a woman sucking child her from having compassion on [the] child of womb her also these they will forget and I not I will forget you.
16 Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
Here! on palms of hands I have inscribed you walls your [are] before me continually.
17 Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
They have made haste children your [those who] tear down you and [those who] make desolate you from you they will go out.
18 Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
Lift up all around eyes your and see all of them they have gathered together they have come to you [by] [the] life of me [the] utterance of Yahweh that all of them like ornament[s] you will put on and you will tie on them like bride.
19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
For waste places your and desolate [places] your and [the] land of destruction your for now you will be [too] cramped for [the] inhabitant[s] and they will be far away [those who] swallowed up you.
20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
Yet they will say in ears your [the] children of bereavement your it is cramped for me the place draw near! for me so let me dwell.
21 Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
And you will say in heart your who? did he father for me these [children] and I [was] bereaved and barren gone into exile - and thrust away and these [children] who? did he bring up here! I I remained to alone me these [children] where? [are] they.
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
Thus he says [the] Lord Yahweh here! I will lift up to [the] nations hand my and to peoples I will raise standard my and they will bring sons your in a bosom and daughters your on a shoulder they will be carried.
23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
And they will be kings foster-fathers your and princesses their suckling-nurses your faces ground they will bow down to you and [the] dust of feet your they will lick up and you will know that I [am] Yahweh whom not they will be ashamed [those who] wait for me.
24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
¿ Will it be taken from a warrior booty and or? [the] captive[s] of [the] righteous will it escape.
25 Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
For thus - he says Yahweh also a captive of a warrior he will be taken and [the] booty of a ruthless [person] it will be delivered and opponent your I I will oppose and children your I I will save.
26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
And I will cause to eat [those who] maltreat you own flesh their and like sweet wine own blood their they will become drunk! and they will know all flesh that I [am] Yahweh deliverer your and redeemer your [the] mighty one of Jacob.

< Isaya 49 >