< Isaya 18 >
1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
Ah! le pays du bruissement des ailes, qui est au delà des fleuves de l'Éthiopie;
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
qui envoie des ambassadeurs par la mer, dans des vaisseaux de papyrus sur les eaux, en disant: « Allez, messagers rapides, vers une nation grande et douce, vers un peuple redoutable dès son origine, une nation qui mesure et qui foule, dont le pays est divisé par les fleuves! ».
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
Vous tous, habitants du monde, et vous, habitants de la terre, quand une bannière est levée sur les montagnes, regardez! Quand on sonne de la trompette, écoutez!
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
Car l'Éternel m'a dit: « Je me tiendrai tranquille, et je verrai dans ma demeure, comme une chaleur claire au soleil, comme un nuage de rosée dans la chaleur de la moisson. »
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
Car avant la moisson, quand la floraison est terminée et que la fleur devient un raisin mûr, il coupera les brins avec des serpes, il abattra et enlèvera les branches étalées.
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
On les laissera ensemble pour les oiseaux de proie des montagnes et pour les animaux de la terre. Les oiseaux de proie les mangeront en été, et tous les animaux de la terre les mangeront en hiver.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
En ce temps-là, on apportera un présent à l'Éternel des armées, de la part d'un peuple grand et lisse, d'un peuple impressionnant dès son origine, d'une nation qui mesure et foule, dont le pays est partagé par les fleuves, au lieu du nom de l'Éternel des armées, la montagne de Sion.