< Isaya 15 >

1 Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
[the] oracle of Moab that in a night [which] it was devastated Ar of Moab it was destroyed that in a night [which] it was devastated Kir of Moab it was destroyed.
2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
It has gone up the house and Dibon the high places for weeping on Nebo and on Medeba Moab it is wailing [is] on all heads its baldness every beard [is] diminished.
3 Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
In streets its they have girded on sackcloth on roofs its and in open places its all of it it is wailing going down in weeping.
4 Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
And it has cried out Heshbon and Elealeh to Jahaz it has been heard voice their there-fore [the] armed [men] of Moab they are shouting being its it is trembling to it.
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
Heart my for Moab it cries out fugitives its [are] to Zoar Eglath Shelishiyah for - [the] ascent of Luhith with weeping it is going up on it that [the] road of Horonaim a cry of shattering they rouse.
6 Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
That [the] waters of Nimrim wastes they are for it has dried up grass it has wasted away vegetation greenery not it is.
7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
There-fore [the] wealth [which] it has made and store their over [the] wadi of the poplars they carry off them.
8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
For it has gone around the cry [the] territory of Moab to Eglaim wailing its and Beer Elim wailing its.
9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.
That [the] waters of Dimon they are full blood that I will put on Dimon added [things] [will be] for [the] escaped remnant of Moab a lion and for [the] remainder of [the] land.

< Isaya 15 >