< Hosea 9 >

1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
May not you rejoice O Israel - to rejoicing like the peoples for you have prostituted yourself from with God your you have loved [the] hire of a prostitute on all threshing floors of grain.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
Threshing floor and wine-press not it will feed them and new wine it will fail it.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
Not they will remain in [the] land of Yahweh and he will return Ephraim Egypt and in Assyria unclean [food] they will eat.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
Not they will pour out to Yahweh - wine and not they will be pleasing to him sacrifices their [will be] like bread of mourning to them all [those who] eat it they will make themselves unclean for bread their [will be] for self their not it will go [the] house of Yahweh.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
What? will you do to [the] day of an appointed feast and to [the] day of [the] festival of Yahweh.
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
For there! they have gone from [the] devastation Egypt it will gather them Memphis it will bury them treasure of silver their nettle[s] it will take possession of them thorn[s] [will be] in tents their.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
They have come - [the] days of punishment they have come [the] days of retribution let them know Israel [is] a fool the prophet [is] mad [the] person of the spirit on [the] greatness of iniquity your and great animosity.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
[was] a watchman Ephraim with God my a prophet a trap of a fowler [is] on all ways his animosity [is] in [the] house of God his.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
They have made deep they have dealt corruptly like [the] days of Gibeah he will remember iniquity their he will punish sins their.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
Like grapes in the wilderness I found Israel like early fig[s] on a fig tree at beginning its I saw ancestors your they they came Baal Peor and they devoted themselves to shame and they were detestable things as loved they.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
Ephraim like bird it will fly away glory their from child bearing and from womb and from conception.
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
That except they will bring up children their and I will bereave them from everyone for also woe! to them when depart I from them.
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Ephraim just as I have seen to Tyre [is] planted in pastureland and Ephraim to bring out to [one who] kills children his.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Give to them O Yahweh what? will you give give to them a womb [which] miscarry and breasts [which] dry up.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
All wickedness their [is] in Gilgal for there I hated them on [the] wickedness of deeds their from house my I will drive out them not I will repeat to love them all leaders their [are] rebellious.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
He has been struck Ephraim root their it has dried up fruit (not *Q(K)*) they will produce! also if they [masc] will give birth! and I will put to death [the] precious things of [masc] womb their.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
He will reject them God my for not they have listened to him so they may be wanderers among the nations.

< Hosea 9 >