< Hosea 5 >

1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Hear this O priests and pay attention - O house of Israel and O house of the king give ear for [belongs] to you the judgment for a trap you have been to Mizpah and a net spread out over Tabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
And slaughtering rebels they have made deep and I [am] discipline to all of them.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
I I know Ephraim and Israel not it is hidden from me for now you have prostituted yourself O Ephraim it has made itself unclean Israel.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
Not they permit deeds their to return to God their for a spirit of prostitution [is] in inner being their and Yahweh not they know.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
And it testifies [the] pride of Israel in face its and Israel and Ephraim they will stumble on iniquity their it will stumble also Judah with them.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
With flock[s] their and with herd[s] their they will go to seek Yahweh and not they will find [him] he has withdrawn from them.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
With Yahweh they have dealt treacherously for children strange they have borne now it will devour them a new moon with portions their.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
Blow a horn in Gibeah a trumpet in Ramah sound an alarm Beth Aven after you O Benjamin.
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Ephraim a waste it will become on [the] day of rebuke among [the] tribes of Israel I make known [something] trustworthy.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
They have become [the] leaders of Judah like [those who] displace a boundary on them I will pour out like water wrath my.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
[is] oppressed Ephraim [is] crushed of judgment for he was determined he walked after a command.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
And I [am] like moth to Ephraim and like rottenness to [the] house of Judah.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
And he saw Ephraim sickness his and Judah wound his and he went Ephraim to Assyria and he sent to king Jareb and he not he is able to heal you and not it will depart from you [the] wound.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
For I [will be] like lion to Ephraim and like young lion to [the] house of Judah I I I will tear to pieces and I may go I will carry off and there not [will be] a deliverer.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
I will go I will return to place my until that they will be held guilty and they will seek face my when it is distress to them they will seek earnestly me.

< Hosea 5 >