< Mwanzo 8 >

1 Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
And he remembered God Noah and every animal and all the livestock which [were] with him in the ark and he made to pass God a wind over the earth and they subsided the waters.
2 Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
And they were shut up [the] springs of [the] deep and [the] floodgates of the heavens and it was restrained the rain from the heavens.
3 Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
And they turned back the waters from on the earth going and turning back and they decreased the waters from [the] end of fifty and one hundred day[s].
4 katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
And it rested the ark in the month seventh on [the] seven-teen day of the month on [the] mountains of Ararat.
5 Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
And the waters they were going and decreasing until the month tenth in the tenth [month] on [day] one of the month they were seen [the] tops of the mountains.
6 Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
And it was from [the] end of forty day[s] and he opened Noah [the] window of the ark which he had made.
7 na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
And he sent out the raven and it went out continuously and returned until dried up the waters from on the earth.
8 Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
And he sent out the dove from with him to see ¿ were they abated the waters from on [the] surface of the ground.
9 Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
And not found the dove a resting place for [the] sole of foot its and it returned to him into the ark for water [was] on [the] surface of all the earth and he stretched out hand his and he took it and he brought it to him into the ark.
10 Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
And he waited again seven days other and he repeated to send out the dove from the ark.
11 Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
And it came to him the dove to [the] time of evening and there! a leaf of olive freshly plucked [was] in mouth its and he knew Noah that they were abated the waters from on the earth.
12 Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
And he waited again seven days other and he sent out the dove and not it repeated to return to him again.
13 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
And it was in one and six hundred year in the first [month] on [day] one of the month they were dried up the waters from on the earth and he removed Noah [the] covering of the ark and he saw and there! they were dried up [the] surface of the ground.
14 Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
And in the month second on [the] seven and twenty day of the month was dry the earth.
15 Ndipo Mungu akamwambia Noa,
And he spoke God to Noah saying.
16 “Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
Go out from the ark you and wife your and sons your and [the] wives of sons your with you.
17 Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
Every animal which [is] with you some of all flesh among the bird[s] and among the livestock and among every creeping thing which creeps on the earth (bring out *Q(k)*) with you and they will swarm on the earth and they will be fruitful and they will multiply on the earth.
18 Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
And he went out Noah and sons his and wife his and [the] wives of sons his with him.
19 Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
Every animal every creeping thing and every bird every creeping [thing] on the earth to families their they went out from the ark.
20 Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
And he built Noah an altar to Yahweh and he took some of all - the livestock clean and some of every bird clean and he offered up burnt offerings on the altar.
21 Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
And he smelled Yahweh [the] odor of soothing and he said Yahweh to heart his not I will repeat to curse again the ground for sake of humankind for [the] inclination of [the] heart of humankind [is] evil since youth his and not I will repeat again to strike down every living [thing] just as I have done.
22 “Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”
Again all [the] days of the earth seed and harvest and cold and heat and summer and winter and day and night not they will cease.

< Mwanzo 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark